Usajili wa wasanii Fiesta 2016

Page 94

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2015
Posts
5,204
Reaction score
15,207
Kama ilivyozoeleka radio ya Clouds Fm chini ya Clouds Media Group huleta Tamasha la Burudani kila mwaka maarufu kama "FIESTA".

Baada ya kutofanyika Mwaka Jana kutokana na nchi yetu kuwa na Uchaguzi Mkuu,basi mwaka huu 2016 Tamasha litafanyika kama kawaida iliyopewa kama "TigoFiesta" yenye kauli Mbiu "IMOOOO" kuzinduliwa Mkoani Mwanza tar 20.08.2016.

Katika Usajili wa Wasanii watakaotumbuiza,list ya Kwanza ilitajwa pale B.O.B Kinondoni na Jumla ya Wasanii watano walitajwa na kusainishwa Mikataba pia kukabidhiwa jezi zao Maalum za Fiesta 2016.

Wasanii waliotajwa mpaka sasa ni;
1. Ben Paul
2. Maua Sama
3. Bill Nass
4. Rubby
5. Mr Blue
6. Christian Bella

Wengine Waliosajiliwa Mwenge ni hawa Wafuatao;
1. Navy Kenzo
2. Fid Q
3. Weusi
4. Ommy Dimpoz
5. Baraka Da Prince
6. Nandy

Updates: 11-08-2016
Usajili unaendelea kama kawaida. Wasanii Leo watasainishwa mikataba katika Maskani ya TIP-TOP CONNECTION pale Magomeni.
Wasanii waliosajiliwa Leo na kusainishwa mikataba ni hawa wafuatao;
1. Raymond wa WCB.
2. Shilole aka "Shishi Baby"
3. Dogo Nigga
4. Dayna Nyange
5. Tip-Top Connection "Madee,Dogo Janja na Tundaman"

Pamoja na hayo yote, Clouds Media ikishirikiana na Tigo wanakuletea kifurushi Maalum cha Fiesta kinachoenda kwa jina la "FIESTA OFFER" ambacho wateja wa kanda husika watakuwa wakipata GB 1 kwa sh 1000 tu.

 
Ruge na mimi niweke
 
Ruby akimaliza nyimbo zake 2 anashuka jukwaani??
Kama unakumbuka Rubby alishinda kinyang'anyiro cha Fiesta Super Diva 2014 iliyosimamiwa na Dj Fetty hivyo katika moja ya vipengele vya mkataba wake,kinawataka Clouds Media Group kumtembeza katika mikoa yote patakapofanyika tamasha la Fiesta. Hivyo yeye ataenda mikoa yote 15.

Na vyovyote vile naona ataperform. Labda patokee emergence.

Hizo nyimbo zake mbili na pia alizoshirikishwa ataziperform.
 
show ya bure na allowance ya msosi na accommodation.
asiyefunzwa na mamaye atafunzwa na mutahaba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…