Usajili wetu (Yanga SC) msimu huu

Usajili wetu (Yanga SC) msimu huu

MO11

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2014
Posts
19,057
Reaction score
39,387
Foward hatari wa kimataifa fox in the box aliyepachika magoli ya kutosha kwenye mechi chache takwimu zake ni hatari amekuja nchini kutusaidia kimataifa mwite Lazarous Kambole mechi 46 magoli 2. Mengine hawajayahesabu mazoezini.

Winga hatari winga wa kuingia nyo kwenye box aliyelitumikia bechi la mnyama ndani ya misimu miwili amepachika mabao matatu yote ya kideo kumbukumbu kubwa aliyotuachia kigoma ni kushangilia ubingwa huku akivua bukta na kubaki na chupi.

Mwite wakili msomi aliyetusumbua CAS huku tukitumia hela nyingi Benard Morrison mtoto wa efua wa tatu ni hatari huyu amecheza newcastle ya kwa malkia pale pale st james park baada ya hapo akatumikia vilabu vingi nchini scotland na kuamua kuwa store keeper huyu si mwingine Midfield ya kazi dalali wa kaze aliyeamua kuisaidia yanga aliyechagua kuacha kuuza bia kuja kucheza mpira

Si mwingine ni Gael Bigirimana tangu aanze kucheza mpira ana magoli ya kutosha kuliko Juma Kaseja yaani magoli matatu mechi 728

Pia hatupo mbali kuwaunga mkono timu yetu ya wanawake tumeamua kusajili Joyce

itaendelea
 
Kuna yule wa usiku anaitwa joyce naskia saa 00:01 anatambulishwa straiker mwingine tetesi zinadai ni ashura
 
Mbona Nassoro Kapama na Habib Kiyombo huwataji?
 
Hivi Aziza tayari ameshatambulishwa?
Kuhusu aziza bado kuna sintofahamu inaonekana kataja dau kubwa na boss yupo njia panda kujitia kwenye kitanzi

Maana kila akifikiria kupiga chini huo usajili anakumbuka tayari kuna mashabiki wanaamini Aziza kashatia wino anasuburiwa kutangazwa tu.

Kusambaza picha zinazomuonesha akiwa mezani wanaandikishana na huyo mcgezaji lilikuwa ni kosa alofanya mwanzoni kwa lengo la ku catch attention za mashabiki.

Sasa yuko katika wakati mgumu anafikiria aki terminate huu mchongo atawaeleza nini wananchi wakamuelewa?
 
Kuhusu aziza bado kuna sintofahamu inaonekana kataja dau kubwa na boss yupo njia panda kujitia kwenye kitanzi

Maana kila akifikiria kupiga chini huo usajili anakumbuka tayari kuna mashabiki wanaamini Aziza kashatia wino anasuburiwa kutangazwa tu.

Kusambaza picha zinazomuonesha akiwa mezani wanaandikishana na huyo mcgezaji lilikuwa ni kosa alofanya mwanzoni kwa lengo la ku catch attention za mashabiki.

Sasa yuko katika wakati mgumu anafikiria aki terminate huu mchongo atawaeleza nini wananchi wakamuelewa?
Akikaa nchale akisimama nchale kudadadeq
 
Kiukweli 80% mashabiki wa simba hawajaridhika na usajili wa club wamebaki kujifariji kujifananisha na young African.
Tunarudia tena ligi ikianza hatutaki kusikia mkilalamika kuhusu bahasha za khaki
 
Back
Top Bottom