Usalama barabarani, Tanroad fanyeni ubunifu kudhibiti Bodaboda na Bajaji kwenye mataa

Usalama barabarani, Tanroad fanyeni ubunifu kudhibiti Bodaboda na Bajaji kwenye mataa

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Ni kama vile imekuwa ni vigumu kukabiliana na changamoto ambazo Wenzetu huko nje hawana shida nazo, na kwa kuwa wameshakuja na matumizi ya taa za kuongozea Magari wakaishia hapo nasi tumebaki hapo hapo ili hali sisi tuna shida zaidi ya hiyo.

Huwa najiuliza hivi vyuo vyetu kama NIT wana nafasi gani kutafuta suluhu ya baadhi ya matatizo ya nchi?

Si wapewe assignment kama hizo waumize vichwa maana ndio field zao?

MAONI YANGU:- Kama inawezekana mita kadhaa kufika kwenye taa kutenganishwe kwa kuweka borders ambapo Bodaboda na Bajaji zikae kwenye lane yao kushoto ambako kutakuwa na kigingi mbele kitakachozuia Pikipiki na Bajaji kupita, kigingi ambacho kitakuwa kinafanya kazi sambamba na taa zile, ikiwaka nyekundu kinainuka, na sehemu ile ya kulia ambako Magari yanatumia kubuniwe namna ya kuweka vigingi vitakavyomfanya Bajaji au Boda asichague kwenda, kwa kuwa tairi la Bajaji au Boda si sawa na yale ya Gari hivyo nadhani haitokosekana namna ya kufanya Boda ashindwe kutumia kipande kile cha mita 50 au 100 kufikia kwenye taa.

Nakumbuka iliwahi kuongelea suala la camera, sidhani kama tutafanikiwa maana tuna changamoto ya rasilimali Watu, hapa ni machinery tu ndio itatuondoa kwenye hili janga.
 
Ma~Afisa Usafirishaji Wa CCM, Hao Ndiyo Mtaji Wao Siku Zote
Kuwazuia Wanawaogopa Maana Kura Zao
 
Yaa niwe na pikipiki nisubiri taa? Nikiwa na pikipiki naangalia usalama kulia na na kushoto kama hakuna anayekuja nachomoka Kama risasi shwaaaa
 
Yaa niwe na pikipiki nisubiri taa? Nikiwa na pikipiki naangalia usalama kulia na na kushoto kama hakuna anayekuja nachomoka Kama risasi shwaaaa
Ipo siku utajua umuhimu wa kusimama kwenye mataa.
 
Wajinga hawa wanasababisha hata zile dakika za kuvuka zinaisha huku Watu hawajamaliza kuvuka maana inabidi usubiri wapite huku Magari yamesimama.

Yaa niwe na pikipiki nisubiri taa? Nikiwa na pikipiki naangalia usalama kulia na na kushoto kama hakuna anayekuja nachomoka Kama risasi shwaaaa
 
Wajinga hawa wanasababisha hata zile dakika za kuvuka zinaisha huku Watu hawajamaliza kuvuka maana inabidi usubiri wapite huku Magari yamesimama.
Mjinga ni wewe ambaye hata kuandika hujui.
 
Back
Top Bottom