Usaliti kwenye Ndoa: Jambo baya sana ambalo jamii inalichukulia kuwa la kawaida

Usaliti kwenye Ndoa: Jambo baya sana ambalo jamii inalichukulia kuwa la kawaida

KikulachoChako

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2013
Posts
19,185
Reaction score
37,239
Sabal kheri waungwana.

Nyakati fulani nilikuwa kwenye kijiwe kimoja tukibadilishana mawili matatu ya maisha na changamoto zake na kuangalia namna gani tunazikabili.

Katika maongezi hayo likaibuka suala mambo ya ndoa kama ilivyo kawaida kuwa na yenyewe ni sehemu ya changamoto kwenye maisha yetu ya kila siku.

Mada kuu ilikuwa namna gani usaliti kwenye NDOA ulivyo kithiri

Wakati tukijaribu kutafakari jambo hilo ndipo jamaa mmoja akaibuka na hoja kuwa mbona hayo sasa hivi ni mambo ya kawaida tu kwenye jamii zetu, kwamba hayo mambo (ya kutoka nje ya ndoa) ni ya kawaida tu isipokuwa kikubwa ni heshima tu akiwa anamaanisha kuwa ni kukufanya usijue tu au afanyie mbali yaani heshima ni kutokukuonyesha.

Maongezi yakiwa yanayoyoma lakini fikra zangu zikaganda kwenye haya maswali kadhaa. Inakuwaje kawaida kwa mke au mume wa mtu kufanya uchafu. Nini maana ya ndoa? Ina maana gani mtu kuingia gharama za kufunga ndoa ikiwa bado atayafanya yale aliyokuwa akiyafanya kipindi hajaoa. Lakini kinachotia hofu ni kwamba jamii imeshaliona kuwa ni jambo kawaida na hakuna anayeshtuka as long as long wewe hujui.

Wanasema kikubwa heshima tu, ni heshima ipi wanayoimaanisha? Utasemaje unamheshimu mtu unayemsaliti? Utasemaje unamheshimu mtu unamuibia mali zake. Utasemaje unamheshimu mtu unayemfanyia unafiki.

Kwa kweli tuendapo si kuzuri na tumeshafikia hatua mbaya. Ndio maana mioyo ya watu inapata ukakasi linapokuja suala la kufunga ndoa, maana haileti mantiki ya wewe kumhudumia ng'ombe lakini mazao ya huyo ng'ombe unavuna na wengine.
 
Usaliti ni neno pana sana, ila wanandoa wengi wanachukuliaga simple!
Mbaya zaidi tupo mwisho wa mwaka, ndoa nyingi zitapangaranyika!
Adui halali mpaka amalize, kuchinja na kuharibu.

Isaya 54:17
"Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa BWANA, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema BWANA."
 
Sipendai maisha ya msongo wa mawazo eti mke wangu anagawa uroda kwa mwingine nje na mimi. Kwa amani tu nitamuacha aende huko anakopapenda, yaani nitajitenga naye bila vurugu wala kusababisha madhara
Sijakuelewa...... unamaanisha utamuacha aendelee huko huku na wewe ukiendelea naye....??
 
Kuna jamii moja huku,wanawake wanachapika sana tu lakin hakuna mwanaume ambae niliwah kumuona kamuacha mkewe

Kuna jamaa mmoja aliwah kuchapiwa nae akaenda kumchapia jamaa aliemchapia na maisha yakaendelea vzur tu
 
Mambo yanabadirika,.. kwasasa utakuwa MPUMBAVU kuamini kuwa mpenzi wako, mume au mkeo hachepuki nawala hawezi kuchepuka....
 
Mtu ni mke wa mtu, na isitoshe ana mimba, lakini bado anqtombwa na njemba za nje.

Ref video ya Balthazar
 
Mtu ni mke wa mtu, na isitoshe ana mimba, lakini bado anqtombwa na njemba za nje.

Ref video ya Balthazar
Huyo lazima atakua ni muuza k aliye jificha kwenye ndoa!!
 
Back
Top Bottom