Usambazaji wa Maji ya Bomba Musoma Vijijini

Usambazaji wa Maji ya Bomba Musoma Vijijini

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

USAMBAZAJI WA MAJI YA BOMBA MUSOMA VIJIJINI

Jimbo la Musoma Vijijini lenye vijiji 68 linayo miradi ya usambazaji wa maji ya bomba ndani ya vijiji vyote 68 - tunaishukuru sana Serikali yetu

Mradi wa Kata za Busambara & Kiriba:

Tenki la ujazo wa lita 500,000 limejengwa Kijijini Mwiringo kwa ajili ya usambazaji wa maji ya bomba ndani ya vijiji vyote sita (6) vya Kata hizo mbili.

DC wa Wilaya ya Musoma, Mhe Juma Chikoka anaufutalia mradi huu na mingine ya Jimboni mwetu kwa ukaribu sana. Mkuu huyo wa Wilaya ataenda kuzindua utumiaji wa maji ya bomba ya mradi huo mwezi ujao - msikilize kwenye CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa.

RUWASA inaendelea kupongezwa kwa kazi nzuri inazozifanya Jimboni mwetu - kila kijiji kupata maji ya bomba kutoka Ziwa Victoria au/na kuchimbiwa kisima kirefu cha maji - hongereni sana!

CLIP/VIDEO 2 zilizoambatanishwa hapa zinaelezea utekelezaji wa mradi wa maji ya bomba ya Kata za Busambara na Kiriba - tafadhali zifungue!

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6
Musoma

Tarehe:
Jumamosi, 15 Feb 2025
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2025-02-15 at 11.55.03.mp4
    39 MB
Back
Top Bottom