Kuna mtu yupo kijijini anahitaji matairi ya magari yaliyotumika lakini sio makukuu kwa ajili ya kutengenezea mikokoteni. Ameniambia size 16. Kwa hiyo naulizia upatikanaji wake hapa mjini Dar.
Idadi hajaniambia, swala ni je yanapatikana wapi? Unayo? Unauza sh ngapi moja au vyoyte vile? Condition ya matairi hayo ikoje? Kama utampelekea mpaka aliko, nadhani ndio utataka kujua kijiji gani, lakini nadhani atasafirisha kwa njia zake mwenyewe.
Biashara yake inaweza kuwa endelevu, kwa maana kwamba atakuwa mteja wako wa kudumu.