Ushahidi wa Daniel Yesu alizaliwa mwaka 4BC na kusulubiwa 31AD

Ushahidi wa Daniel Yesu alizaliwa mwaka 4BC na kusulubiwa 31AD

hamis77

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
13,628
Reaction score
20,992
UNABII WA DANIEL UNAONESHA VZR ATABATIZWA,KUUWAWA KATIKA MIAKA 27B.C NA 31B.C, HIVO UTAWEZA KUJUA PIA ALIZALIWA LINI

Danieli 9:25 “Basi ujue na kufahamu, ya kuwa amri ya kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu hata zamani zake masihi aliye mkuu; kutakuwa na majuma saba; na katika majuma sitini na mawili utajengwa tena pamoja na njia kuu zake…”

Yerusalemu ulianza kujengwa upya katika mwaka 457 KK kwa amri ya mfalme Artashasta

Unabii unasema kutakuwa na wiki 7 kujumlisha wiki 62 jumla 69 kutoka kujengwa Yerusalemu mwaka 457K.K. hadi kuja kwa masihi. Katika unabii siku moja ni sawa na mwaka mmoja (angalia Ezekieli 4:6 na Hesabu 14:34), hivyo wiki 69 ambazo ni sawa na siku 483 zinamaanisha miaka 483 halisi; ambayo ingepita tangu kujengwa upya kwa Yerusalemu hadi kuja kwa Masihi.

Hivyo ukichukua miaka 483 ukaijumlisha katika mwaka -457 KK ambao Yerusalemu ulianza kujengwa, utapata mwaka 27 BK (-457 483 = 27); ambao Masihi angetiwa mafuta.

images.png



Je Mashi alitiwa mafuta mwaka 27 BK?

Matendo 10:38 “habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.”

Masihi = aliyetiwa mafuta.

Hivyo kulingana na unabii Yesu alibatizwa au kutiwa mafuta katika mwaka 27 BK mwishoni mwa wiki 69, na Luka anatuambia Yesu alikuwa na umri wa miaka 30 wakati anabatizwa 27 BK.

Luka 3:21, 23 “Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka; Roho Mtakatifu akashuka juu yake…Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa amepata umri wake kama miaka thelathini, akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusufu, wa Eli,”

Hii ni kwa sababu Yesu hakuzaliwa 1 BK; kwani kalenda ilikosewa kama miaka 4.

Historia inasema Herode alikufa 4 KK, na tunajua Herode alitaka kumuua Yesu, hivyo Yesu alizaliwa 4 KK na katika 27 BK alipobatizwa alikuwa na umri wa miaka 30.

MWAKA -4 30 1 = Unapata hadi miaka 27 ya YESU anapobatizwa (Namba “1” ipo kwa ajiri ya mwaka “0”)

Hivyo Yesu alibatizwa mwaka 27BK. (majuma 69 au miaka 483) kutoka mwaka 457KK hadi 27BK. Hivyo unabii ulitimia kwa ukamilifu, kama ulivyotabiliwa kuwa tangu kujengwa Yerusalemu mwaka 457KK mpaka kuja kwake masihi kungekuwa na majuma 69 au miaka 483.

Kwa hakika Yesu mwenyewe alisema wazi kwamba unabii ulikuwa umetimia kikamilifu.

Marko 1:9, 14, 15 “Ikawa siku zile, Yesu alikuja kutoka Nazareti ya Galilaya, akabatizwa na Yohana katika Yordani…Hata baada ya Yohana kutiwa gerezani, Yesu akaenda Galilaya, akiihubiri Habari Njema ya Mungu, akisema, Wakati umetimia…”

Yesu alijua kwamba mwaka 27BK. unabii wa Danieli ulikuwa umetimia.

JE YESU ALIKUFA LINI?

T
UMSIKILIZE TENA NABII DANIEL

Danieli 9:27 “Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja;…”

Yesu alipobatizwa ilikuwa ni wiki ya 69, hivyo katika wiki 70 zilizotolewa kwa ajili ya taifa la Israeli ilikuwa imebaki wiki moja tu muda wa rehema ya taifa lao uishe. Hivyo kwa muda wa juma hili moja lililobaki Yesu na wanafunzi wake waliitangaza Injili ya Mungu kwa Waisraeli pekee yao. Hawakutangaza Injili mahali pengine popote tofauti na Israeli. Yesu mwenyewe aliwaamru wanafunzi wake SOMA...
Mathayo 10:5, 6

Tumejua kwamba kwa juma moja Yesu angefanya agano na watu wengi, lakini Injili ingehubiriwa kwanza kwa Israeli pekee. Sasa Je juma moja linamaanisha nini?
Juma moja = siku 7. Katika unabii siku = mwaka, hivyo juma moja = miaka 7. Muda huu ulianzia mwaka 27BK alipobatizwa Yesu, na unaendelea mpaka 34BK (27+7 = 34).
Katikati ya juma.

Danieli 9:27 “…Na kwa nusu ya juma hiyo ataikomesha sadaka na dhabihu;…”

Juma zima = miaka 7, hivyo nusu ya juma ni miaka 3 na nusu (7 / 2 = 3.5). Ukihesabu miaka mitatu na nusu kutoka katika mwaka 27BK. aliobatizwa Yesu utapata mwaka 31BK. Hivyo Yesu angekomesha sadaka na dhabihu, au angesulubiwa msalabani, au “angekatiliwa mbali,” Dan. 9:26 katika mwaka 31BK. Kwa hiyo Yesu alifanya kazi yake ya utumishi kwa muda wa miaka 3 na nusu, tangu 27BK hadi 31BK aliposulubishwa msalabani.

Mathayo 27:50-51 “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake. Na tazama pazia la hekalu lakapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;”
Pazia lilichanika kuonesha kwamba hatupaswi kutoa tena sadaka wala dhabihu kwa ajili ya msamaha wa dhambi na upatanisho; bali tunapaswa kumwangalia Yesu pekee kwa ajili ya vitu vyote hivyo.

Rehema kwa taifa la Israeli yaisha.

Juma moja la mwisho ambalo lilianza 27 BK lingeisha mwaka 34 BK, nusu ya juma ni miaka 3.5 ambayo Yesu alifanya kazi yake tangu 27 BK alipobatizwa hadi 31 BK aliposulubishwa. Hivyo katika juma la mwisho (la 70), ilikuwa imebaki nusu juma (miaka 3 na nusu) pekee ambayo ingeishia 34 BK; kwa ajili ya Wayahudi. Kama Wayahudi wangendelea kumkataa Mwana wa Mungu hadi 34 BK, ndipo Mungu angeuondoa ufalme kwao na kuwapa watu wa mataifa. Je Wayahudi walimkubali Yesu kabla ya mwaka 34 BK au waliendelea kuwa wakaidi? Wayahudi walithibitisha kuikataa kabisa rehema yao ya majuma 70 kwa kumwua Stefano katika 34 BK!

Matendo 7:56-59 “Akasema, Tazama? naona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama mkono wa kuume wa Mungu. Wakapiga kelele kwa sauti kuu, wakaziba masikio yao, wakamrukia kwa nia moja, wakamtoa nje ya mji, wakampiga kwa mawe…stefano, naye akiomba, akisema , Bwana Yesu, pokea roho yangu.”

Yesu alipopaa mbinguni wanafunzi wake waliendelea kuhubiri Injili kwa Wayahudi. Lakini majuma 70 yalipoisha katika mwaka 34BK, Wayahudi waliukataa wazi wazi ujumbe wa Injili kwa kitendo cha kumuua Stefano. Hivyo unabii wa Yesu ulitimia, Wakanyanganywa ufalme wa Mungu nao wakapewa watu wa mataifa.

Mathayo 21:43 “Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.”
Unabii ulitimia majuma 70 kwa ajili ya Wayahudi yalipoisha nao wakathibitisha kuikataa Injili, Mitume wakageukia kuhubiri kwa watu wa mataifa.

.
072b2404aad31d9a1fffa47da48f447f.jpg



HITIMISHO;
YESU KAZALIWA MWAKA 4K.K, KABATIZWA MWAKA 27B.K AKIWA NA MIAKA 30,KAFA MSALABANI MWAKA 31B.K


Marejeo:
1. Kwa ushahidi kuhusu tarehe 457KK, ni mwaka wa saba wa kutawala kwake mfalme Artashasta, ambaye katika mwaka 457KK aliamuru mji wa Yerusalemu ujengwe; angalia, S.H. Horn na L.H. Wood, The Chronology of Ezra 7 (Washington, D.C.: Review and Herald association, 1953); na E.G.Kraeling, The Brooklyn Museum Aramaic Papyri (New Haven or London, 1953,) ukr. 191-193
 
Kwa kigezo cha "Herode kufa 4kk na alitaka kumuua yesu hivyo yesu kazaliwa 4kk" Tutakuaminije hapo je kama Herode alitaka kumuua letsay 6kk je?
 
Hii habari yakusema kwamba siku moja ni sawa na mwaka mmoja si ndo jamaa yule alitumia kutabili mwisho wa Dunia kwamba ni mwaka 1884 mwisho wa siku akajikuta amedanganya?
 
Kwa kigezo cha "Herode kufa 4kk na alitaka kumuua yesu hivyo yesu kazaliwa 4kk" Tutakuaminije hapo je kama Herode alitaka kumuua letsay 6kk je?
Soma kwa makini yeye ameleta maneno ya mtakatifu Daniel. We unabisha maneno ya mtakatifu Daniel wewe yaliyoandikwa chini ya ufunuo wa Mungu?
 
Sijabisha kuhusu Mtakatifu Danieli hapo, jitahidi kuwa na akili ya uelewa mkuu!
 
UNABII WA DANIEL UNAONESHA VZR ATABATIZWA,KUUWAWA KATIKA MIAKA 27B.C NA 31B.C, HIVO UTAWEZA KUJUA PIA ALIZALIWA LINI

Danieli 9:25 “Basi ujue na kufahamu, ya kuwa amri ya kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu hata zamani zake masihi aliye mkuu; kutakuwa na majuma saba; na katika majuma sitini na mawili utajengwa tena pamoja na njia kuu zake…”

Yerusalemu ulianza kujengwa upya katika mwaka 457 KK kwa amri ya mfalme Artashasta

Unabii unasema kutakuwa na wiki 7 kujumlisha wiki 62 jumla 69 kutoka kujengwa Yerusalemu mwaka 457K.K. hadi kuja kwa masihi. Katika unabii siku moja ni sawa na mwaka mmoja (angalia Ezekieli 4:6 na Hesabu 14:34), hivyo wiki 69 ambazo ni sawa na siku 483 zinamaanisha miaka 483 halisi; ambayo ingepita tangu kujengwa upya kwa Yerusalemu hadi kuja kwa Masihi.

Hivyo ukichukua miaka 483 ukaijumlisha katika mwaka -457 KK ambao Yerusalemu ulianza kujengwa, utapata mwaka 27 BK (-457 483 = 27); ambao Masihi angetiwa mafuta.

images.png



Je Mashi alitiwa mafuta mwaka 27 BK?

Matendo 10:38 “habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.”

Masihi = aliyetiwa mafuta.

Hivyo kulingana na unabii Yesu alibatizwa au kutiwa mafuta katika mwaka 27 BK mwishoni mwa wiki 69, na Luka anatuambia Yesu alikuwa na umri wa miaka 30 wakati anabatizwa 27 BK.

Luka 3:21, 23 “Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka; Roho Mtakatifu akashuka juu yake…Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa amepata umri wake kama miaka thelathini, akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusufu, wa Eli,”

Hii ni kwa sababu Yesu hakuzaliwa 1 BK; kwani kalenda ilikosewa kama miaka 4.

Historia inasema Herode alikufa 4 KK, na tunajua Herode alitaka kumuua Yesu, hivyo Yesu alizaliwa 4 KK na katika 27 BK alipobatizwa alikuwa na umri wa miaka 30.

MWAKA -4 30 1 = Unapata hadi miaka 27 ya YESU anapobatizwa (Namba “1” ipo kwa ajiri ya mwaka “0”)

Hivyo Yesu alibatizwa mwaka 27BK. (majuma 69 au miaka 483) kutoka mwaka 457KK hadi 27BK. Hivyo unabii ulitimia kwa ukamilifu, kama ulivyotabiliwa kuwa tangu kujengwa Yerusalemu mwaka 457KK mpaka kuja kwake masihi kungekuwa na majuma 69 au miaka 483.

Kwa hakika Yesu mwenyewe alisema wazi kwamba unabii ulikuwa umetimia kikamilifu.

Marko 1:9, 14, 15 “Ikawa siku zile, Yesu alikuja kutoka Nazareti ya Galilaya, akabatizwa na Yohana katika Yordani…Hata baada ya Yohana kutiwa gerezani, Yesu akaenda Galilaya, akiihubiri Habari Njema ya Mungu, akisema, Wakati umetimia…”

Yesu alijua kwamba mwaka 27BK. unabii wa Danieli ulikuwa umetimia.

JE YESU ALIKUFA LINI?

T
UMSIKILIZE TENA NABII DANIEL

Danieli 9:27 “Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja;…”

Yesu alipobatizwa ilikuwa ni wiki ya 69, hivyo katika wiki 70 zilizotolewa kwa ajili ya taifa la Israeli ilikuwa imebaki wiki moja tu muda wa rehema ya taifa lao uishe. Hivyo kwa muda wa juma hili moja lililobaki Yesu na wanafunzi wake waliitangaza Injili ya Mungu kwa Waisraeli pekee yao. Hawakutangaza Injili mahali pengine popote tofauti na Israeli. Yesu mwenyewe aliwaamru wanafunzi wake SOMA...
Mathayo 10:5, 6

Tumejua kwamba kwa juma moja Yesu angefanya agano na watu wengi, lakini Injili ingehubiriwa kwanza kwa Israeli pekee. Sasa Je juma moja linamaanisha nini?
Juma moja = siku 7. Katika unabii siku = mwaka, hivyo juma moja = miaka 7. Muda huu ulianzia mwaka 27BK alipobatizwa Yesu, na unaendelea mpaka 34BK (27+7 = 34).
Katikati ya juma.

Danieli 9:27 “…Na kwa nusu ya juma hiyo ataikomesha sadaka na dhabihu;…”

Juma zima = miaka 7, hivyo nusu ya juma ni miaka 3 na nusu (7 / 2 = 3.5). Ukihesabu miaka mitatu na nusu kutoka katika mwaka 27BK. aliobatizwa Yesu utapata mwaka 31BK. Hivyo Yesu angekomesha sadaka na dhabihu, au angesulubiwa msalabani, au “angekatiliwa mbali,” Dan. 9:26 katika mwaka 31BK. Kwa hiyo Yesu alifanya kazi yake ya utumishi kwa muda wa miaka 3 na nusu, tangu 27BK hadi 31BK aliposulubishwa msalabani.

Mathayo 27:50-51 “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake. Na tazama pazia la hekalu lakapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;”
Pazia lilichanika kuonesha kwamba hatupaswi kutoa tena sadaka wala dhabihu kwa ajili ya msamaha wa dhambi na upatanisho; bali tunapaswa kumwangalia Yesu pekee kwa ajili ya vitu vyote hivyo.

Rehema kwa taifa la Israeli yaisha.

Juma moja la mwisho ambalo lilianza 27 BK lingeisha mwaka 34 BK, nusu ya juma ni miaka 3.5 ambayo Yesu alifanya kazi yake tangu 27 BK alipobatizwa hadi 31 BK aliposulubishwa. Hivyo katika juma la mwisho (la 70), ilikuwa imebaki nusu juma (miaka 3 na nusu) pekee ambayo ingeishia 34 BK; kwa ajili ya Wayahudi. Kama Wayahudi wangendelea kumkataa Mwana wa Mungu hadi 34 BK, ndipo Mungu angeuondoa ufalme kwao na kuwapa watu wa mataifa. Je Wayahudi walimkubali Yesu kabla ya mwaka 34 BK au waliendelea kuwa wakaidi? Wayahudi walithibitisha kuikataa kabisa rehema yao ya majuma 70 kwa kumwua Stefano katika 34 BK!

Matendo 7:56-59 “Akasema, Tazama? naona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama mkono wa kuume wa Mungu. Wakapiga kelele kwa sauti kuu, wakaziba masikio yao, wakamrukia kwa nia moja, wakamtoa nje ya mji, wakampiga kwa mawe…stefano, naye akiomba, akisema , Bwana Yesu, pokea roho yangu.”

Yesu alipopaa mbinguni wanafunzi wake waliendelea kuhubiri Injili kwa Wayahudi. Lakini majuma 70 yalipoisha katika mwaka 34BK, Wayahudi waliukataa wazi wazi ujumbe wa Injili kwa kitendo cha kumuua Stefano. Hivyo unabii wa Yesu ulitimia, Wakanyanganywa ufalme wa Mungu nao wakapewa watu wa mataifa.

Mathayo 21:43 “Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.”
Unabii ulitimia majuma 70 kwa ajili ya Wayahudi yalipoisha nao wakathibitisha kuikataa Injili, Mitume wakageukia kuhubiri kwa watu wa mataifa.

.
072b2404aad31d9a1fffa47da48f447f.jpg



HITIMISHO;
YESU KAZALIWA MWAKA 4K.K, KABATIZWA MWAKA 27B.K AKIWA NA MIAKA 30,KAFA MSALABANI MWAKA 31B.K


Marejeo:
1. Kwa ushahidi kuhusu tarehe 457KK, ni mwaka wa saba wa kutawala kwake mfalme Artashasta, ambaye katika mwaka 457KK aliamuru mji wa Yerusalemu ujengwe; angalia, S.H. Horn na L.H. Wood, The Chronology of Ezra 7 (Washington, D.C.: Review and Herald association, 1953); na E.G.Kraeling, The Brooklyn Museum Aramaic Papyri (New Haven or London, 1953,) ukr. 191-193
Mkuu
Naona umekuwa bingwa wa kujilisha upepo.

Haya yoote uliyoyaandika unalenga kufundisha ama kukosoa? For what extent?
 
Back
Top Bottom