Ushahidi wa Rushwa niupeleke wapi niwe salama!

Ushahidi wa Rushwa niupeleke wapi niwe salama!

leipzig

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2013
Posts
2,766
Reaction score
1,708
Nimeifanya hii kazi kwa muda mrefu ya kurekodi matukio ya rushwa katika polisi wa kawaida na wale wa barabarani. Katika ushahidi wangu nimefanikiwa kuwa na video zenye sauti na picha zikionyesha polisi barabarani wakichukua rushwa mchana kweupee. Wakati mwingine huwa najiuliza hawa polisi wameruhusiwa na serikali kufanya uchafu huu kwa raia?

Uzoefu nilioupata unaonyesha kila mara serikali inapoongeza adhabu kwa makosa ya barabarani ndio furaha na neema kwa polisi. Polisi hawa wala rushwa wakati fulani hutafuta makosa kwa tochi ili mradi wanufaike wao binafsi.

Kuna wanaoamini kuwa ni bora ulipe faini badala ya kutoa rushwa lakini nataka niwaambie polisi akikusimamisha anajitahidi kukujengea mazingira ya kukuchelewesha ili mradi upate nia aliyokusudia. Unakuta wewe dereva ndio unawahi ofisini lakini yeye hata hana habari ndio kwanza atakuhoji ili awe huru kuchukua rushwa kutoka kwako.

Naomba kumuuliza kamanda Mohamed Mpinga yuko tayari kunilinda nimpatie ushahidi huu yeye mwenyewe ofisini kwake? Nasema hivyo kwa sababu miaka ya nyuma kidogo Jerry Muro alipata msukosuko mkubwa baada ya kufichua uovu wa polisi barabarani. Pia afande Mpinga anaweza kuniahidi ni lini nitaona mabadiliko ktk polisi baada ya kumpatia ushahidi?

Kwa kumalizia,nashauri serikali itengeneze mfumo rasmi wa ukaguzi wa magari na madereva ili kuondoa uchafu huu ndani ya jeshi la polisi.

NAWASILISHA.
 
Jerry Muro alisimamisha vita ya wazi dhidi ya Rushwa lakini alipotezwa. Kama serikali yetu inania ya dhati ya kupambana na Rushwa, Jerry Muro alitakiwa apewe mpaka walinzi wa kumlinda, Kinyume chake alipotezwa kabisa na hakuna mtu aliyejaribu kumtetea.

Wewe Bora uumpe huyo unae mwamini hiyo Video, tena atashukuru sana na kuiweka kapuni kisha atakupa na hela kidogo Baadae atawaita vijana wake na kuwaambia waongeze umakini kwenye kazi.

We Tafakari mara kumi kumi Taswira ya Rushwa hapa nchini Halafu jiulize ni nani anayelinda wala Rushwa hapa nchini, JIPU USINIPE MIMI...
 
Umefanya kazi nzur kwa wapenda haki ila kwa ma mwera uko haliya hatari.

Hivi unaamini kabisa kwamba wakubwa hawajui kama kuna rushwa.

Unaamini kabisa mpinga hakuwa kama hao naye alikuwa anapaga dili kama hao.

Kimsingi me nakuomba umtafte mtu ambaye ana nguvu kwenye jamii umpe akusaidie maana ww utazimwa ka kiberiti yaani fuuuuuuu.
 
utapotea kijana the world is not fair, achana na mambo hayo nimepoteza kama watu kumi waliokuwa wanapambana na rushwa....kuna msanii anaitwa maembe msome vzuri na harakati zake za rushwa akaishia segerea
 
Iweke hapa hata kamanda mpinga ataiona kutoka hapa so utakuwa salama salimini,vinginevyo mods waiindoe,but watakaobahatika kuiona wataisambaza kwenye mitandao ya kijamii mingine hivyo kuonwa na watu wengi zaidi na ujumbe utakuwa umefika kwa wahusika
 
Polisi na wala rushwa wote tangu rais Mwinyi afungulie bomba la rushwa hawaiogopi serikali BALI wanachokiogopa ni Kulogwa tu.

IGP wa zamani Mahita aliwahi waambia vijana wake (polisi) unapong'ang'ania rushwa ya mamilioni wakati mtoa rushwa anakupa laki ujue hapo unatafuta KULOGWA.

Hivyo,jua kuwa polisi hawaogopi system wao wanaogopa kulogwa.
 
Iweke Youtube kama alivyoweka bukoba Boy then tupia link Jamii Forums nadhani ndio utakuwa salama zaidi,maana Jerry Muro aliyoyapata ni zaidi ya majanga yaani waalade.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom