Elections 2010 Ushahidi wa Video na Picha za kampeni ya Kikwete Bilal na Shein kabla ya wakati

Elections 2010 Ushahidi wa Video na Picha za kampeni ya Kikwete Bilal na Shein kabla ya wakati

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Link hii inaonyesha Shein na Bilal wakipita kwenye mitaa ya Zanzibar na Pemba

"http://www.youtube.com/v/fw3L02j_lGM"

Link hii inaonyesha Kikwete na Makamba wakimtaja kwa jina mgombea fulani kuwa hawezi kitu, fuatilia mwenyewe.....

"http://www.youtube.com/v/kmrz9ZmkNUg"

Zifuatazo ni picha walipokuwa wanahutubia wananchi katika viwanja vya Jamhuri Dodoma tarehe 12 July 2010.

Kama hizi si kampeni ni nini!!!!!Hivi Chadema haina wanasheria, Lissu , Marando mpo?

8E9U3650.jpg

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiingia katika uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma trh. 12/07/2010.


8E9U3763.jpg

Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwahutubia wananchi katika uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma wakati wa kuwatambulisha mgombea mwenza na mgombea Urais wa Zanzibar .Trh. 12/07/2010.



Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha mgombea mwenza Dr.Mohamed Gharib Bilal kwa wananchi wa mji wa Dodoma katika hafla fupi iliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Jamhuri.Trh. 12/07/2010.
 
Waache na fikra zao fupi ambazo hazikumbuki jana wala hazifikirii kesho.wao wanawaza leo tu.

Sema wanajua kwamba wako juu ya mahakama,kama wameweza kuzuia mgombea binafsi watashindwa kumzuia dr kugombea kama akili zao za kibabe zikiwatuma?
 
Mkuki mtamu kwa nguruwe lakini mchungu kwa binadamu

Makamba anamponda Dr. Slaa hana cha kuonyesha Watazania alichokifanya lakini kwa uelewa wake finyu hata haelewi kuwa hiyo ni kampeni ya kumnadi Kikwete.

Mara nyingi kwa manufaa na ustawi wa taifa lolote dunia mtu anaepewa any public post anatakiwa awe na certain minimum education ili aweze kwanza kujitambua mwenyewe kuwa ana wajibu gani kwa jamii bila kujali mwelekeo wake kisiasa, awe na uwezo wa kupima yale anayotamka na yana athari gani kwa jamii inayomzunguka, na vile awe na scientific challenge kwa yale yanayotamkwa na watu wengine.

Kwa misingi hiyo bila hata kuuliza elemu ya ndugu yetu makamba, hafai kuwa na any public post. Tunamshauri akalee wajukuu ili kutoa nafasi kwa watu wenye vision kuongoza CCM
 
Waache na fikra zao fupi ambazo hazikumbuki jana wala hazifikirii kesho.wao wanawaza leo tu.

Sema wanajua kwamba wako juu ya mahakama,kama wameweza kuzuia mgombea binafsi watashindwa kumzuia dr kugombea kama akili zao za kibabe zikiwatuma?
kwa NEC hii ya Makame lolote linaweza kutokea mkuu. Tabu ni kwamba hata hao Nyoka (Usalama soma uhasama wa taifa) hawazi kuwshauri juu ya timbwili litalo timuka. NEC hii inaweza kabisa kama walivyofanya uchaguzi mdogo wa Mbeya vijijini kwa Sambwee Shitambala
 
supporters.jpg


Jamani hata wanasheria wa CCM akili zao ni sawa na za bosi wao Makamba, hizi t-shirt zenye maandishi ya CHAGUA KIKWETE CHAGUA CCM hadi leo hii ziko mitaani hawazioni na je si kampmeni ya wazi wazi. Ushahidi kama huu hata mahakama huwa haina kazi ya ziada.

Tujiulize zingekuwa zimeandikwa CHAGUA SLAA CHAGUA CHADEMA ingekuwaje, nafikiri Makamba na Msekwa wangezivaa kabisa na kwenda nazo NEC kushitaki. Ndiyo maana Slaa aliwaambia wanasheria wa CCM na viongozi wao hawajui sheria za uchaguzi zinasemaje kama wanajua basi wanafanya hivyo kwa makusudi yao.

Nawashauri CCM fanyeni kampeni za kistaarabu acheni kutafuta visingizio vinavyoashiria uvunjifu wa amani, msifikiri Chadema haina wanasheria wanaoweza kuendesha mambo kama hayo, inao tena waliobobea lakini Chadema imeweka ustaarabu mbele kwanza mengine baadaye kama yatajitokeza.
 
kwa NEC hii ya Makame lolote linaweza kutokea mkuu. Tabu ni kwamba hata hao Nyoka (Usalama soma uhasama wa taifa) hawazi kuwshauri juu ya timbwili litalo timuka. NEC hii inaweza kabisa kama walivyofanya uchaguzi mdogo wa Mbeya vijijini kwa Sambwee Shitambala

Upo sahihi kabisa. Kwa Tanzania: Mahakama, polisi, jeshi, na kila aina ya dola ikiwemo hiyo unayosema uhasama wa taifa, mimi nawaita usalama wa CCM. Kazi yao ni moja tu, kuilinda CCM. Na huyu Makame ni kama messenger wa CCM, sasa sijui kama inawezekana messenger akakataa anachotumwa na boss wake kukitenda. Iwapo CCM watafikisha kesi hiyo mbele yake, itakuwa ni sawa na kumwagiza Makame amfute Slaa katika kinyang'anyiro cha Urais. CCM hawa mara nyingi huwa wanaingilia hata uhuru wa mahakama, watashindwa nini kumwagiza Makame atekeleze wanalolitaka?
Sasa tunayo kazi moja tu watanzania, tunayo kazi moja. Ni kuiondoa CCM madarakani kwa njia yoyote ile. Wakimuondoa Slaa kwenye Kinyang'anyiro cha Urais, tutie mgomo kushiriki kwenye uchaguzi. Au tufanye maandamano yasiyo na kikomo ya kutaka uchaguzi uahirishwe. Wakilazimisha kufanya uchaguzi na wakamtangaza Rais wao, sisi tutamtangaza Slaa kuwa Rais wetu.
 
Upo sahihi kabisa. Kwa Tanzania: Mahakama, polisi, jeshi, na kila aina ya dola ikiwemo hiyo unayosema uhasama wa taifa, mimi nawaita usalama wa CCM. Kazi yao ni moja tu, kuilinda CCM. Na huyu Makame ni kama messenger wa CCM, sasa sijui kama inawezekana messenger akakataa anachotumwa na boss wake kukitenda. Iwapo CCM watafikisha kesi hiyo mbele yake, itakuwa ni sawa na kumwagiza Makame amfute Slaa katika kinyang'anyiro cha Urais. CCM hawa mara nyingi huwa wanaingilia hata uhuru wa mahakama, watashindwa nini kumwagiza Makame atekeleze wanalolitaka?
Sasa tunayo kazi moja tu watanzania, tunayo kazi moja. Ni kuiondoa CCM madarakani kwa njia yoyote ile. Wakimuondoa Slaa kwenye Kinyang'anyiro cha Urais, tutie mgomo kushiriki kwenye uchaguzi. Au tufanye maandamano yasiyo na kikomo ya kutaka uchaguzi uahirishwe. Wakilazimisha kufanya uchaguzi na wakamtangaza Rais wao, sisi tutamtangaza Slaa kuwa Rais wetu.
Makame anaweza kuwa na uwezo huo lakini kwa hili hawezi, unakumbuka hata uchaguzi wa 1995 CCM walipoona joto linapanda walienda kulia NEC, NEC ikawaambia hayo ni mambo ya kawaida katika uchaguzi si Tanzania tu hata mataifa yaliyoendelea rabsha za hapa na pale huwa hazizuiliki.
 
Ukiwa mwongo ni sharti uwe na kumbukumbu, naona hawa memory yao haifanyi vizuri. Watakiona mwaka huu, lazima walinywe.
 
JK ana ugonjwa wa kuanguka, na ugonjwa huu unaathiri ubongo na hivyo kufuta kumbukumbu.Wameshasahau kuwa walianza wao. Safari hii hawatoki majambazi wakubwa hawa
 
Kampeni ni akipiga Pangu Pakavu, akipiga Mbayuwayu anahutubia taifa
 
supporters.jpg


Jamani hata wanasheria wa CCM akili zao ni sawa na za bosi wao Makamba, hizi t-shirt zenye maandishi ya CHAGUA KIKWETE CHAGUA CCM hadi leo hii ziko mitaani hawazioni na je si kampmeni ya wazi wazi. Ushahidi kama huu hata mahakama huwa haina kazi ya ziada.

Tujiulize zingekuwa zimeandikwa CHAGUA SLAA CHAGUA CHADEMA ingekuwaje, nafikiri Makamba na Msekwa wangezivaa kabisa na kwenda nazo NEC kushitaki. Ndiyo maana Slaa aliwaambia wanasheria wa CCM na viongozi wao hawajui sheria za uchaguzi zinasemaje kama wanajua basi wanafanya hivyo kwa makusudi yao.

Nawashauri CCM fanyeni kampeni za kistaarabu acheni kutafuta visingizio vinavyoashiria uvunjifu wa amani, msifikiri Chadema haina wanasheria wanaoweza kuendesha mambo kama hayo, inao tena waliobobea lakini Chadema imeweka ustaarabu mbele kwanza mengine baadaye kama yatajitokeza.

Halafu hawa hawa tutawaona wanaandamana kwenda bodi ya mikopo, kaaazi kwel kwel
 
kwangu mimi mtu yoyote anaeipenda CCM, SIJUI NAMUONAJE, kama akili zake si....
 
Yaani ukiangalia hiyo video ya pili majibu yanajieleza!
 
Mimi nataka kuona tume ya uchaguzi inawachukulia Hatua Gani CCM na Chadema , maana woote wamefanya Kampeni kabla ya muda wakati wenzao wanasubiri kutangazwe...
 
Yaani ukiangalia hiyo video ya pili majibu yanajieleza!
Wanafanya kampeni za wazi kabisa ni kiburi tu cha kulewa madaraka miaka 50 si haba lazima ujione wananchi wote ni mali yako.
 
Mimi nataka kuona tume ya uchaguzi inawachukulia Hatua Gani CCM na Chadema , maana woote wamefanya Kampeni kabla ya muda wakati wenzao wanasubiri kutangazwe...

Kikwete na Dr. Slaa watafutwa wote, then tunaichagua CUF!
 
Back
Top Bottom