Ushairi

Ushairi

George J Minja

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2013
Posts
289
Reaction score
203
Wakuu ni muda sasa tokea niache kutunga na kusoma mashairi ila naamini hiki ni kipaji ndani yangu naomba wote wenye uwezo wa kutunga na kuimba mashairi tujitokeze hapa kuweka mashairi yetu ili jamii ya JF pia ijifunze kwa njia hii leo naanza hivi


Tunakoelekea

Tulikotoka twajua,tuendako giza nene
Tujiulize kwa sala,yajayo twayaonaje
Tulianza kwa pamoja,bila kuwa na upande
Wapi tunaelekea,Yarabi utujalie


Ee mola utujalie,tuijue yako nia
Maisha tuyapatie,tusije poteza nia
Waliyoweka wazee,kutupa maisha mema
Wapi tunaelekea ,yarabi utujalie..............................;;


Nimejaribu tuu kuona kama kale kauwezo kapo au la,ila nikirudi nitakuja malizia hili shairi,karibuni washairi tuendelee sio lazima ya Kimapokea kama lanu(yenye Vina na Mizani) la hasha hata la kisasa weka tuendelee kuburudika

Ahsanteni
 
Wakuu ni muda sasa tokea niache kutunga na kusoma mashairi ila naamini hiki ni kipaji ndani yangu naomba wote wenye uwezo wa kutunga na kuimba mashairi tujitokeze hapa kuweka mashairi yetu ili jamii ya JF pia ijifunze kwa njia hii leo naanza hivi


Tunakoelekea

Tulikotoka twajua,tuendako giza nene
Tujiulize kwa sala,yajayo twayaonaje
Tulianza kwa pamoja,bila kuwa na upande
Wapi tunaelekea,Yarabi utujalie


Ee mola utujalie,tuijue yako nia
Maisha tuyapatie,tusije poteza nia
Waliyoweka wazee,kutupa maisha mema
Wapi tunaelekea ,yarabi utujalie..............................;;


Nimejaribu tuu kuona kama kale kauwezo kapo au la,ila nikirudi nitakuja malizia hili shairi,karibuni washairi tuendelee sio lazima ya Kimapokea kama lanu(yenye Vina na Mizani) la hasha hata la kisasa weka tuendelee kuburudika

Ahsanteni

lalalalala lalalalalalaaaaaaaaaa
lalalalala lalalalalalalalaaaaaaaaaaaa


vina na mizani,uko juu mkuu mimi siwezi wacha wenyewe kina MM na KK Kahigi waje kuweka yao
 
lalalalala lalalalalalaaaaaaaaaa
lalalalala lalalalalalalalaaaaaaaaaaaa


vina na mizani,uko juu mkuu mimi siwezi wacha wenyewe kina MM na KK Kahigi waje kuweka yao

MM Mulokozi na KK Kahigi umenikumbusha ST Anthony Mbagala ndiko nilikowasoma hawa MAGURU wa fasihi,Ahsante sana kamanda.
 
Wakuu ni muda sasa tokea niache kutunga na kusoma mashairi ila naamini hiki ni kipaji ndani yangu naomba wote wenye uwezo wa kutunga na kuimba mashairi tujitokeze hapa kuweka mashairi yetu ili jamii ya JF pia ijifunze kwa njia hii leo naanza hivi


Tunakoelekea

Tulikotoka twajua,tuendako giza nene
Tujiulize kwa sala,yajayo twayaonaje
Tulianza kwa pamoja,bila kuwa na upande
Wapi tunaelekea,Yarabi utujalie


Ee mola utujalie,tuijue yako nia
Maisha tuyapatie,tusije poteza nia
Waliyoweka wazee,kutupa maisha mema
Wapi tunaelekea ,yarabi utujalie..............................;;


Nimejaribu tuu kuona kama kale kauwezo kapo au la,ila nikirudi nitakuja malizia hili shairi,karibuni washairi tuendelee sio lazima ya Kimapokea kama lanu(yenye Vina na Mizani) la hasha hata la kisasa weka tuendelee kuburudika

Ahsanteni

weweweeeeeee wa wapi weweeee watu siku hizi wanasikiliza mabongo flava ma RnB wewe unaleta mambo ya Radio Tanzania hapa hakuna anayejua hizi now days

Ila mkuu umejipanga,haya madude nilisomaga skulini long time mambo yakina Shaaban Robert na Kusadikika poa kip ap
 
weweweeeeeee wa wapi weweeee watu siku hizi wanasikiliza mabongo flava ma RnB wewe unaleta mambo ya Radio Tanzania hapa hakuna anayejua hizi now days

Ila mkuu umejipanga,haya madude nilisomaga skulini long time mambo yakina Shaaban Robert na Kusadikika poa kip ap

Nawewe umeongea nini sasa ukubwa sio mdomo ni akili
 
Nililisoma ngumbaru, shairi langu sikia
Kijiji Nangurukuru,Mbaazi kupalilia,
Bila kusahau Masuguru, kwa bibi binti Rupia.
Lima Mkulima lima , lima upate mradi.

Lima lima mwana kwetu, lima mkulima lima,
Lima uupate utu, ukamilishe huduma
Lima bila gutugutu,njaa isipate dhima,
Lima lima mwana kwetu , lima Mkulima lima


lima Tanga na Tabora, lima Mbeya na Ruvuma
Lima tusije dorora, lima Singida mapema,
Morogoro na Mtwara , msichelewe kulima
Lima mkulima lima , lima upate mradi.

Lima Arusha Manyara,Iringa pia Tunduma.
Lima Mwanza na Kagera,Lima ulie Kigoma,
Limeni Mazao bora, Kilimanjaro Dodoma
Lima Mkulima lima ,lima upate mradi.

Lima Geita na Njombe,Lima mazao Mtama,
Simiyu shikeni Jembe,msidharau kulima.
Wa Pwani pia mtambe,kama Mzee Mwilima.
Lima lima mwana kwetu , lima mkulima lima.

Katavi Rukwa na Mara,acheni kurudi nyuma,
Kumbe hasira hasara,mmesahau kulima,
Msije pata hasara, Mvua itaja goma,
Lima mkulima lima, lima upate mradi.

Lima Mahindi Mpunga,chai Miwa Maharage,
Nyanya Matunda Karanga,Lima kahawa Mkonge,
Choroko Njegere panga, sokoni bei wapange.
Lima mkulima lima, lima upate mradi.

Kaditama na tamati, hapa ninamalizia,
Nalifunga langu Shati, Makobazi kuvalia,
Bila kusahau Koti,Babu aloniachia.
Lima mkulima lima, lima upate mradi.





 
Back
Top Bottom