Naanza mada hii kwa kujadili hatua mbalimbali, ingawaje hatua moja inaweza isiwe na umuhimu kwa mwingine lakini ikawa chachu ya kujitathimini hatua uliyopo.
Wakati Upo Chuo.
Kwa sie masikini hatua hii ni muhimu sana katika kuandaa maisha yetu ya mtaani baada kumaliza chuo. Ukichanga karata zako vizuri kwenye hatua hii, unaweza kupunguza makali ya mtaa pale utakapochelewa kupata ajira. Hata hivyo, hapa nawalenga wale wanaopata posho ya chakula na malazi, maarufu kama "boom"!
Wakati upo chuo, hakikisha unaweka akiba ya angalau 50% ya “boom” kila unapota. Weka akiba kwa njia itakayokufanya ushindwe kuichukua kirahisi. Njia nzuri ni kufungua Akaunti ya Muda Maalumu (Fixed Deposit Account) kila unapopata “boom”! Kama una utalaamu kwenye bitcoin basi wekeza kwenye bitcoin kwa kutumia Cryptocurrency Exchange Markets zinazokuwa regulated na nchi za Magharibi.
Acha kutumia boom kwa kununua vitu kama tv, subwoofer au kufanya ndio mtaji wa kufanyia betting au forex trading. Vyote hivyo havitakusaidia mtaani. Na vitu kama betting ni kujitafutia uraibu (addiction) utakaokutafuna bila huruma hata kama utabahatika kupata kazi nzuri hapo baadae.
Jiepushe na pombe na anasa zisizo na tija. Hizo anasa utapiga sana ukishakuwa na maisha yako mtaani! Acha kuiga wanachofanya wenzako kwa sababu hujui maisha ya kwao yapo vipi. Sie wengine tumeshawahi kufanya kazi na watu ambao kila mwezi wanatumia pesa na wazazi wao ingawaje tayari wana mshahara wao!! Wakati nipo chuo nilikuwa na washikaji wawili ambao walikuwa hawajui hata boom ni kiasi gani na linaingizwa wakati gani!!
Wewe mwenzangu mimi, wakati upo chuo ni hatua ya kuweka akiba itakayokusaidia kuanzia maisha mtaani.
Baada ya Kumaliza Chuo.
Kwa ulimwengu wa leo ni kosa la kiufundi kumaliza chuo na kuingia mtaani wakati huna kompyuta. Hivyo, matumizi ya awali ya akiba uliyoweka kutokana na boom ni kununua PC yenye angalau RAM 4GB, HDD 500GB. Kwa wale wanaoishi Dar es salaam kwa kupanga, unatakiwa kuchagua eneo linaloendana na maisha yako ya kuwa "jobless" lakini usipange mahali kwa mazoea!
Katika hatua hii, hakikisha unachagua maeneo ambayo vyumba ni bei nafuu, na pia ni rahisi kwenda mjini hata kwa mguu pale unapokuwa umeishiwa kabisa. Pia hapo mtaani hakikisha unatengeneza mahusiano ya karibu na muuza bucha na mwenye duka linalopatikana bidhaa zote muhimu! Kama ulikuwa na Fixed Deposit Account (FDR), huu ndio wakati wa pesa iliyokuwa humo kuihamishia kwenye Akaunti ya Akiba! Kama ulikuwa na FDR zaidi ya moja, usikombe zote kwa pamoja!
Acha pesa yako kwenye Akaunti ya Akiba na sio kwenye simu! Achana na mambo ya Mobile Banking; yaani usijisajiri kabisa! Kwenye simu weka pesa ya matumizi madogo madogo tu! Kama una akiba ya kutosha, basi lipa kodi ya mwaka mzima. Kama umepanga chumba mahali ambapo wapangaji mnachanga kulipa umeme, basi lipa angalau wa miezi 6 kwa mkupuo. Vile vile unachotakiwa kufanya kila mwezi ni kupiga mahesabu ya chakula (unga na mchele), maharage, na nyama!! Kama unatarajia kwa mwezi utakula kilo 2 za nyama, basi mwachie rafiki yako muuza bucha (mshirikishe na mmiliki wa bucha) pesa ya mwezi mzima! Fanya hivyo hivyo kwa rafiki yako wa dukani.
Ukifanya hayo hapo juu itakusaidia kupangilia maisha yako bila ya "stress" kwa sababu umelipa kodi mwaka mzima, na pia unao uhakika wa mlo! Na kama huwezi kupika, jifunze sasa!
Sio hivyo tu, kitanda na godoro vinakutosha sana! Kingine unachotakiwa kuwa nacho ni meza ya PC na kiti! Acha gheto lako lionekane halina kitu kwa sababu hiyo huenda itakusaidia kuona aibu kuleta watoto wa kike ghetto! Watoto wa kike nao ni vimeo tu kwa mtu anayetafuta maisha!! Ni kimeo sio tu katika kumgharamia hata kwa vitu vidogo, bali mnaweza hata kutiana ujauzito; kitu ambacho ni "luxury" isiyohitajika kabisa katika harakati zako za kujipanga!
Wakati Upo Chuo.
Kwa sie masikini hatua hii ni muhimu sana katika kuandaa maisha yetu ya mtaani baada kumaliza chuo. Ukichanga karata zako vizuri kwenye hatua hii, unaweza kupunguza makali ya mtaa pale utakapochelewa kupata ajira. Hata hivyo, hapa nawalenga wale wanaopata posho ya chakula na malazi, maarufu kama "boom"!
Wakati upo chuo, hakikisha unaweka akiba ya angalau 50% ya “boom” kila unapota. Weka akiba kwa njia itakayokufanya ushindwe kuichukua kirahisi. Njia nzuri ni kufungua Akaunti ya Muda Maalumu (Fixed Deposit Account) kila unapopata “boom”! Kama una utalaamu kwenye bitcoin basi wekeza kwenye bitcoin kwa kutumia Cryptocurrency Exchange Markets zinazokuwa regulated na nchi za Magharibi.
Acha kutumia boom kwa kununua vitu kama tv, subwoofer au kufanya ndio mtaji wa kufanyia betting au forex trading. Vyote hivyo havitakusaidia mtaani. Na vitu kama betting ni kujitafutia uraibu (addiction) utakaokutafuna bila huruma hata kama utabahatika kupata kazi nzuri hapo baadae.
Jiepushe na pombe na anasa zisizo na tija. Hizo anasa utapiga sana ukishakuwa na maisha yako mtaani! Acha kuiga wanachofanya wenzako kwa sababu hujui maisha ya kwao yapo vipi. Sie wengine tumeshawahi kufanya kazi na watu ambao kila mwezi wanatumia pesa na wazazi wao ingawaje tayari wana mshahara wao!! Wakati nipo chuo nilikuwa na washikaji wawili ambao walikuwa hawajui hata boom ni kiasi gani na linaingizwa wakati gani!!
Wewe mwenzangu mimi, wakati upo chuo ni hatua ya kuweka akiba itakayokusaidia kuanzia maisha mtaani.
Baada ya Kumaliza Chuo.
Kwa ulimwengu wa leo ni kosa la kiufundi kumaliza chuo na kuingia mtaani wakati huna kompyuta. Hivyo, matumizi ya awali ya akiba uliyoweka kutokana na boom ni kununua PC yenye angalau RAM 4GB, HDD 500GB. Kwa wale wanaoishi Dar es salaam kwa kupanga, unatakiwa kuchagua eneo linaloendana na maisha yako ya kuwa "jobless" lakini usipange mahali kwa mazoea!
Katika hatua hii, hakikisha unachagua maeneo ambayo vyumba ni bei nafuu, na pia ni rahisi kwenda mjini hata kwa mguu pale unapokuwa umeishiwa kabisa. Pia hapo mtaani hakikisha unatengeneza mahusiano ya karibu na muuza bucha na mwenye duka linalopatikana bidhaa zote muhimu! Kama ulikuwa na Fixed Deposit Account (FDR), huu ndio wakati wa pesa iliyokuwa humo kuihamishia kwenye Akaunti ya Akiba! Kama ulikuwa na FDR zaidi ya moja, usikombe zote kwa pamoja!
Acha pesa yako kwenye Akaunti ya Akiba na sio kwenye simu! Achana na mambo ya Mobile Banking; yaani usijisajiri kabisa! Kwenye simu weka pesa ya matumizi madogo madogo tu! Kama una akiba ya kutosha, basi lipa kodi ya mwaka mzima. Kama umepanga chumba mahali ambapo wapangaji mnachanga kulipa umeme, basi lipa angalau wa miezi 6 kwa mkupuo. Vile vile unachotakiwa kufanya kila mwezi ni kupiga mahesabu ya chakula (unga na mchele), maharage, na nyama!! Kama unatarajia kwa mwezi utakula kilo 2 za nyama, basi mwachie rafiki yako muuza bucha (mshirikishe na mmiliki wa bucha) pesa ya mwezi mzima! Fanya hivyo hivyo kwa rafiki yako wa dukani.
Ukifanya hayo hapo juu itakusaidia kupangilia maisha yako bila ya "stress" kwa sababu umelipa kodi mwaka mzima, na pia unao uhakika wa mlo! Na kama huwezi kupika, jifunze sasa!
Sio hivyo tu, kitanda na godoro vinakutosha sana! Kingine unachotakiwa kuwa nacho ni meza ya PC na kiti! Acha gheto lako lionekane halina kitu kwa sababu hiyo huenda itakusaidia kuona aibu kuleta watoto wa kike ghetto! Watoto wa kike nao ni vimeo tu kwa mtu anayetafuta maisha!! Ni kimeo sio tu katika kumgharamia hata kwa vitu vidogo, bali mnaweza hata kutiana ujauzito; kitu ambacho ni "luxury" isiyohitajika kabisa katika harakati zako za kujipanga!