Ushauri: Bajaji zilizozuiwa kubeba abiria Mbezi Luisi ziruhusiwe kutokana na wingi wa abiria

Ushauri: Bajaji zilizozuiwa kubeba abiria Mbezi Luisi ziruhusiwe kutokana na wingi wa abiria

Rodwell mTZ

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2012
Posts
1,455
Reaction score
1,621
Ninayo heshima kubwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ya kukuandikia barua hii fupi.

Kwanza kabisa hongera sana kwa kazi nzuri ya kuijenga taifa.

Lengo la barua hii ni kuhusu marufuku uliyoitoa dhidi ya bajaji zinazobeba abiria kutoka kituo cha Mbezi Luisi zikiwapeleka mjini, Manzese na kwingineko

Mimi nina ombi kwako nakuomba kama inawezekana uziruhusu ziendelee kubeba abiria kwa sababu zifuatazo:

(1) Mabasi ya mwendo Kasi hayana uwezo wa kumudu uwingi wa abiria waliopo katika barabara hii. Haswa wakati wa rush hours.

(2) Serikali yako tukufu ni hivi majuzi imetangaza,wananchi tuepuke misongamano isiyo na lazima ili kujikinga na ugonjwa wa COVID-19,kusema kweli Mheshimiwa bajaji zimepunguza sana misongamano kwenye Mabasi.

(3) Mheshimiwa, Mabasi ya mwendonkasi yanasimamisha kutoa huduma inapofika saa tano usiku,hii inanikimbusha ule usemi unaosemwa "ngoma ya kitoto haikeshi" yaani wakati ambapo shughuli za hili jiji zinaendelea Hadi usiku wa manane wao wanalaza Mabasi yao,nadhani wanakua wameishaingiza hesabu inayotakiwa,huwa kuna Mabasi ya mikoani huwa yamechelewa kufika pale kwenye stendi kubwa ya Mbezi,wageni wenye uwezo mdogo wa kukodi texi,bajaji hua zinawasaidia sana.

Mwisho Mheshimiwa Rais nakushukuru kwa kutumia muda wako kuisoma barua hii, naomba nikutakie mafanikio makubwa sana katika shughuli zako zote za kutuongoza.

Asante sana.
 
Ninayo heshima kubwa Mheshimiwa Raisi wa jamhuri ya muungano ya Tanzania ya kukuandikia barua hii fupi.
Kwanza kabisa hongera sana kwa kazi nzuri ya kuijenga taifa.
Lengo la barua hii ni kuhusu marufuku uliyoitoa dhidi ya bajaji zinazobeba abiria kutoka kituo cha Mbezi luisi zikiwapeleka mjini,Manzese na kwingineko,mimi Nina ombi kwako nakuomba kama inawezekana uziruhusu ziendelee kubeba abiria kwa sababu zifuatazo:
(1) Mabasi ya mwendo Kasi hayana uwezo wa kumudu uwingi wa abiria waliopo katika barabara hii. Haswa wakati wa rush hours.
(2) Serikali yako tukufu ni hivi majuzi imetangaza,wananchi tuepuke misongamano isiyo na lazima ili kujikinga na ugonjwa wa COVID-19,kusema kweli Mheshimiwa bajaji zimepunguza sana misongamano kwenye Mabasi.
(3) Mheshimiwa,Mabasi ya mwendonkasi yanasimamisha kutoa huduma inapofika saa tano usiku,hii inanikimbusha ule usemi unaosemwa "ngoma ya kitoto haikeshi" yaani wakati ambapo shughuli za hili jiji zinaendelea Hadi usiku wa manane wao wanalaza Mabasi yao,nadhani wanakua wameishaingiza hesabu inayotakiwa,huwa kuna Mabasi ya mikoani huwa yamechelewa kufika pale kwenye stendi kubwa ya Mbezi,wageni wenye uwezo mdogo wa kukodi texi,bajaji hua zinawasaidia sana.
Mwisho Mheshiwa Raisi nakushukuru kwa kutumia mda wako kuisoma barua hii,nomba nikutakie mafanikio makubwa sana katika shughuli zako zote za kutuongoza.
Asante sana Mheshimiwa Raisi wa jamhuri ya muungano ya Tanzania.
Umeweka maoni mazuri kabisa
 
Ona ss anavyokosesha watu vipato.
Na pia anahamasisha ukabaji, hii itatokea pale abiria wakutoka mikoani wanapokosa usafiri wa uhakika kwenda maeneo mengine ya jiji.
OVA...!
 
Badala boda boda zipigwe marufuku kwa sababu ndizo zinaongoza kwa ajali wao wanapiga marufuku bajaji ambazo zimerahisisha usafiri kutoka terminal kwenda sehemu zingine za jiji
 
[emoji38][emoji23][emoji1787] Nchi ngumu sana hii..
Duuh!!
Route ya mbez to maeneo mengine ya jiji ndo ilikuwa inalipa hatari...ss sjajua anatutakia nn wananchi wake...NAJIULIZA !!??

AU KWAKUWA SERIKALI YA CCM HAITEGEMEI KURA ZA WANANCHI NDIYO WANATUFANYIA HIVI!!!!
 
Duuh ..zile bajaji Kama zimepigwa marufuku Ni pigo kubwa Sana..zinarahisisha Sana usafiri, yaan no stress ya usafiri saiv...Mwendokasi tabu tupu kwanza unasimama,Mara sometimes mshuke kimara,Mara foleni ndefu za kupanda..

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
RAISI NI KILAZA TU.
ANGEFANYA UCHUNGUZI KABLA YA KUTAMKA AMA KUTOA KAULI YAKE.
Ova.
Haya ndiyo madhara ya nchi kuongozwa na mtu mmoja. Hili siyo jukumu wala kero ya kufikisha kwa rais hata kidogo. Tunarudi kule kule. Bila katiba mpya ni bure. Matatizo kama haya yanadhihirisha kabisa kuwa ngazi za chini hazifanyi kazi na kila mtu anasubiri kusikia kutoka kwa rais.
 
Back
Top Bottom