Ushauri: Bima kwa wote iendane na utoaji wa elimu. Kuna "Lightness" wengi sana wasio na sauti

Ushauri: Bima kwa wote iendane na utoaji wa elimu. Kuna "Lightness" wengi sana wasio na sauti

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Jana waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu alitoa maelekezo kwa Lightness Shirima (22), mwanafunzi wa Chuo Cha Serikali za Mitaa (LGTI), Hombolo - Dodoma kufika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kuchukua kitambulisho chake kilicho zuiwa kutolewa kutokana na kushindwa kulipa deni la tsh 9M la matibabu ya baba yake aliye fariki dunia July 4 mwaka huu.

Kwenye andiko lake, Mh. Waziri anakiri uwepo wa gharama kubwa kwenye upatikanaji wa huduma za afya kwenye zama hizi cha maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Aidha, uhalisia wa gharama za kupata bima za kawaida kwa watanzania ni mkubwa sana. Mfano, gharama za kukata kifurushi cha chini kabisa cha bima kutoka NHIF ni tsh 192,000/= kwa mtu mmoja ambapo huduma nyingi hauwezi kuzipata. Kifurushi hiki huitwa Najali afya.

Vifurushi vingine pia vya ngazi ya chini kabisa ambavyo huitwa wekeza na timiza huwa na gharama za tsh 384,000/= na 516,000/= mtawalia, vyote vikihusisha mtu mmoja pekee. Pesa hii huongezeka kulingana na idadi ya watu, utegemezi wao pamoja na aina ya matibabu.

Ni pesa ndogo kwa wenye nacho, ni kubwa sana kwa namba kubwa ya watanzania hasa inapotolewa mara moja.

Lazima tukiri kuwa siyo watu wote hawana uwezo wa kukata bima hizi. Changamoto nyingine kubwa ni elimu ambayo haijatolewa kwenye jamii kuhusu umuhimu wa watu kuwa na bima za afya.

Sheria ya bima ya afya kwa kila mtu iletwe haraka. Hii imekuwa ni ahadi ya serikali kwa muda mrefu sasa. Itasaidia kuepusha adha kubwa inayojitokeza kwa sasa ambapo wanachi wengi wamekuwa wanashindwa kumudu gharama za sasa.

Utaratibu huo ambao utaruhusu kuchangiana kidogo kidogo kwa manufaa ya umma kwa ujumla utakuwa ni mwarobaini katika kuokoa jahazi hili ambalo linaelekea kuzama sasa.

Nashauri pia gharama za bima hiyo pindi itakapo huishwa iwe ni ndogo na rafiki, pia iweke utaratibu utakaopunguza ukakasi, kero na urasimu wa sasa uliopo katika kupata huduma za afya kwa watu wenye bima.

Kuna kina Lightness wengi sana mtaani wasio na sauti. Tumemsaidia huyu mmoja, vipi kwa wale wengine wenye changamoto hii wasio na sauti?

Turekebishe sera zetu za afya sasa ili ziwe na manufaa kwa kila mtu.

Elimu inayohusu umuhimu wa watu kuwa na bima ya afya utolewe sasa, pia sheria ya bima kwa wote iletwe haraka.

===

Kuhusu Lightness Soma Waziri wa Afya, tunakuomba usiishie kwa Lightness tuu, tupo lukuki ambao vitambulisho vyetu vya NIDA vimeshikiliwa Mloganzila Hospitali
 
Jana waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu alitoa maelekezo kwa Lightness Shirima (22), mwanafunzi wa Chuo Cha Serikali za Mitaa (LGTI), Hombolo - Dodoma kufika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kuchukua kitambulisho chake kilicho zuiwa kutolewa kutokana na kushindwa kulipa deni la tsh 9M la matibabu ya baba yake aliye fariki dunia July 4 mwaka huu.

Kwenye andiko lake, Mh. Waziri anakiri uwepo wa gharama kubwa kwenye upatikanaji wa huduma za afya kwenye zama hizi cha maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Aidha, uhalisia wa gharama za kupata bima za kawaida kwa watanzania ni mkubwa sana. Mfano, gharama za kukata kifurushi cha chini kabisa cha bima kutoka NHIF ni tsh 192,000/= kwa mtu mmoja ambapo huduma nyingi hauwezi kuzipata. Kifurushi hiki huitwa Najali afya.

Vifurushi vingine pia vya ngazi ya chini kabisa ambavyo huitwa wekeza na timiza huwa na gharama za tsh 384,000/= na 516,000/= mtawalia, vyote vikihusisha mtu mmoja pekee. Pesa hii huongezeka kulingana na idadi ya watu, utegemezi wao pamoja na aina ya matibabu.

Ni pesa ndogo kwa wenye nacho, ni kubwa sana kwa namba kubwa ya watanzania hasa inapotolewa mara moja.

Lazima tukiri kuwa siyo watu wote hawana uwezo wa kukata bima hizi. Changamoto nyingine kubwa ni elimu ambayo haijatolewa kwenye jamii kuhusu umuhimu wa watu kuwa na bima za afya.

Sheria ya bima ya afya kwa kila mtu iletwe haraka. Hii imekuwa ni ahadi ya serikali kwa muda mrefu sasa. Itasaidia kuepusha adha kubwa inayojitokeza kwa sasa ambapo wanachi wengi wamekuwa wanashindwa kumudu gharama za sasa.

Utaratibu huo ambao utaruhusu kuchangiana kidogo kidogo kwa manufaa ya umma kwa ujumla utakuwa ni mwarobaini katika kuokoa jahazi hili ambalo linaelekea kuzama sasa.

Nashauri pia gharama za bima hiyo pindi itakapo huishwa iwe ni ndogo na rafiki, pia iweke utaratibu utakaopunguza ukakasi, kero na urasimu wa sasa uliopo katika kupata huduma za afya kwa watu wenye bima.

Kuna kina Lightness wengi sana mtaani wasio na sauti. Tumemsaidia huyu mmoja, vipi kwa wale wengine wenye changamoto hii wasio na sauti?

Turekebishe sera zetu za afya sasa ili ziwe na manufaa kwa kila mtu.

Elimu inayohusu umuhimu wa watu kuwa na bima ya afya utolewe sasa, pia sheria ya bima kwa wote iletwe haraka.

===

Kuhusu Lightness Soma Waziri wa Afya, tunakuomba usiishie kwa Lightness tuu, tupo lukuki ambao vitambulisho vyetu vya NIDA vimeshikiliwa Mloganzila Hospitali
Ukiishusha vhini ya hapo, basi jua NHIF itakufa maana wanaoingia huingia wakiwa tayari ni wagonjwa hivyo huenda sio kwa lengo la kuweka pesa bali kutumia pesa zaidi ya alizoweka hivyo hutumia pesa za wengine. Mwishowe huwa sio kinga bali ni sehemu ya kufuata matibabu wakishashindwa kumudu. NHIF inajiendesha yenyewe pasipo ruzuku ya serikari na usijesema inatoa 3%,hiyo 3% ni ya mtumishi maana wamekupunguzia kutoka kukatwa 6% mpaka 3%. Usifikiri mfuko unayumbishwa na watumishi,nope. Watu wengi ambao sio watumishi huingia wakishaona matibabu ni makubwa hivyo kufanya mfuko sio wakuwekeza bali ni wamatumizi straight. Bima mtu huwekeza kwanza kwaajili ya kinga ila sio straight matumizi ya 200,000/= ambapo hata pesa uliochangia hata haijafanya kitu. Pia jua, wengi wakishamaliza matibabu either kwa matibabu au kwa bahati mbaya kifo, badi huanza kudelay kuchangia na mwishowe huacha. Inafika hatua mfuko unaelemewa maana watanzania wenyewe huuangamiza. Pili hizi bima za 50,400 hutoboa mfuko vibaya sana ila serikari huiwezi kuipinga na ndio maana mfuko ukawa wa serikari. Ungekuwa wa private, gharama zake usingezimudu. Ndio maana wengi wenye private insurance, mwaajiri ndio hulipia sio yeye kama yeye.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom