Ushauri: Haki za mtoto baada ya mama kufariki

Ushauri: Haki za mtoto baada ya mama kufariki

Mayu

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2010
Posts
7,621
Reaction score
12,505
Wakuu kwema

Enzi sijafunga ndoa nilizaa mtoto wa kiume na binti mmoja wa kiislam kutoka Tanga. Hatukua na mpango wa kuoana hivyo mtoto alipofikisha umri wa miaka miwili kasoro nikamchukua na kuishi naye mimi, na sasa ana miaka 12

Mama yake alifanikiwa kupata kazi serikali lakini hakubahatika kuolewa wala kupata mtoto tena. Kwa bahati mbaya sana Mungu amemuita, amefariki.

Ikabidi nimchukue niambatane na mwanangu kwenda mazishini Tanga. Mambo nilio yakuta huko sina hamu kabisa.

Kikao cha ukoo kikakaa kikateua msimamizi wa mirathi na wakati wa kikao ikaonekana kwakuwa marehemu ana mtoto mmoja tu na hana mume wala wazazi hivyo mali za Marehemu (mafao, Nyumba na kiwanja kigamboni) sehemu zitakua za mtoto wa marehemu BALAA LIKAANZIA HAPO.

Ikaonekana mimi nimeenda na mtoto makusudi ili turithi mali za marehemu, ndugu wakagoma kabisaaa.

Kuepusha shari nikasema jamani sisi tumekuja kuzika tu mali za marehemu fanyeni mnavyo weza ninyi, kuna baadhi ya ndugu wakagoma wakasema nikosa na mtoto akikua atakuja kudai mali za mama yake

Baada ya kujadiliana sana wakaja na agenda ya kwamba nimuache mtoto chini ya usimamizi wao ili sasa maliziwe chini yao na watamsomeaha hadi hatakapokuwa mkubwa. SIKUKUBALIANA NAO KABISA.

Msimamizi mwenye ni kaka yake mkubwa mtata balaa eti yeye ndio asimamie mali za marehemu na mtoto akae naye huko Tanga tena kijijini.

Mzozo ukawa mkwabwa nikaanza kutishwa hadi kurogwa, kesho yake asubuhi nikapanda basi nikatudi zangu Dar.

Bado natafakari nifanyeje. Akili inaniambia niwapotezee lakini nikimuangalia mwanangu naona ana haki na mali za mama yake

Ili kusiwepo na mzozo wataalamu wa sheria hii niende nayo vipi?
 
Kama ulivyomchukua mwanao mwanzo basi endelea kumtunza bila kuwabughudhi ndugu wa marehemu mzazi mwenzio.

Sioni kama ana haki kubwa unayohisi anaikosa, kama ulivyokosea wewe kumpa haki ya kuishi na mama yake kwenye utoto wake. Wewe ulianza kumnyima mwanao haki yake kubwa na ya msingi, hao ndugu wanamalizia tu.

Tulia ulee mwanao, wao waache na maisha yao...naamini mtoto alimuhitaji zaidi mama kuliko Mali za mama.
 
Kama ulivyomchukua mwanao mwanzo basi endelea kumtunza bila kuwabughudhi ndugu wa marehemu mzazi mwenzio.

Sioni kama ana haki kubwa unayohisi anaikosa, kama ulivyokosea wewe kumpa haki ya kuishi na mama yake kwenye utoto wake. Wewe ulianza kumnyima mwanao haki yake kubwa na ya msingi, hao ndugu wanamalizia tu.

Tulia ulee mwanao, wao waache na maisha yao...naamini mtoto alimuhitaji zaidi mama kuliko Mali za mama.

Nilitaka ushauri wa kisheria na sio hadithi za mtaani zisizo na logic za kisheria, na ndio maana kuna mambo sijataka kwenda deep sana.

Kiufupi ni kwamba marehemu alikuja na kumuacha mtoto kwa mama yangu na kutokomea, nisinge weza kumnyang’anya mtoto ambaye bado alikua ananyonya.

Alikuja ku-regret baadae sana na mtoto akawa anakwenda likizo kwa mama yake kila mwezi wa 12
 
Sababu umri bado mdogo, hatapewa mali yoyote, mali zitakuwa chini ya msimamizi wa mali atayeteuliwa hadi pale mtoto atapofikisha miaka 18

Ila kwa jumla hizo mali zishapotea

Nenda mahakamani uone watakuambiaje kabla hujafungua shauri la mirathi

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Mimi nashauri uwaache hao ndugu wa marehemu waaamue vile wapendavyo kwenye umiliki wa hizo mali. Wala usiingie kwenye mgogoro wa kutaka kuwa msimamizi wa mirathi, na wakati hukuwa mume halali wa marehemu.
Wasimamizi sahihi wa mirathi ni ndugu zake.

Binafsi nakuunga mkono sehemu moja tu ya kukataa kumuacha mtoto wako alelewe kijijini, kisa kuna mali za urithi wa mama yake. All in all, pole sana kwa changamoto uliyopitia.
 
Nilitaka ushauri wa kisheria na sio hadithi za mtaani zisizo na logic za kisheria, na ndio maana kuna mambo sijataka kwenda deep sana

Kiufupi ni kwamba marehemu alikuja na kumuacha mtoto kwa mama yangu na kutokomea....... nisinge weza kumnyang’anya mtoto ambaye bado alikua ananyonya

Alikuja ku regret baadae sana na mtoto akawa anakwenda likizo kwa mama yake kila mwezi wa 12
Watakuja wanasheria. Ila Kwa hali uliyoelezea ni busara usijishughulishe na Mali za marehemu. Ndugu ndio wataamua. Lea mtoto wako. Pole Kwa changamoto.
 
Mimi nashauri uwaache hao ndugu wa marehemu waaamue vile wapendavyo kwenye umiliki wa hizo mali. Wala usiingie kwenye mgogoro wa kutaka kuwa msimamizi wa mirathi, na wakati hukuwa mume halali wa marehemu.
Wasimamizi sahihi wa mirathi ni ndugu zake.

Binafsi nakuunga mkono sehemu moja tu ya kukataa kumuacha mtoto wako alelewe kijijini, kisa kuna mali za urithi wa mama yake. All in all, pole sana kwa changamoto uliyopitia.

Mkuu nashukuru kwa ushauri. Ofcoz wasimamizi watakua wao.

Hofu yao kubwa ni kwamba watakapo kwenda mahakamani na kutaja marehemu kaacha mtoto mahakama LAZIMA itaamuru mali ziwe za mtoto chini ya msimamizi wa mirathi, hapo sasa kaka mtu atakosa uhuru wa kuuza nyumba na kiwanja.

Ndio maana wanata akae naye yeye mtoto ili ku justify kuuza mali kwa mgongo wa matumiza na ada za mtoto
Maana walisha leta hoja mali ziuzwe zote (hofu yao ni mahakama na sio mimi). Na mimi sigombanii mali ila napinga kujustfy kwa kumchukua mwanangu waishi naye.

Mimi sikujua kabisa kama marehemu ana nyumba na kiwanja hivyo wakati nakwenda huko sikufikiria kabisa mambo ya mali zaidi ya kudhani labda wakifatilia mafao wanaweza kuamua tu kindugu mtoto watampa kidogo, aikua issue kabisa kichwani mwangu.

MSIMAMO WAO NI MTOTO AKAISHI TANGA
 
Mkuu nashukuru kwa ushauri

Ofcoz wasimamizi watakua wao,

Hofu yao kubwa ni kwamba watakapo kwenda mahakamani na kutaja marehemu kaacha mtoto mahakama LAZIMA itaamuru mali ziwe za mtoto chini ya msimamizi wa mirathi, hapo sasa kaka mtu atakosa uhuru wa kuuza nyumba na kiwanja

Ndio maana wanata akae naye yeye mtoto ili ku justify kuuza mali kwa mgongo wa matumiza na ada za mtoto
Maana walisha leta hoja mali ziuzwe zote(hofu yao ni mahakama na sio mimi)
Na mimi sigombanii mali ila napinga kujustfy kwa kumchukua mwanangu waishi nae


Mimi sikujua kabisa kama marehemu ana nyumba na kiwanja hivyo wakati nakwenda huko sikufikiria kabisa mambo ya mali zaidi ya kudhani labda wakifatilia mafao wanaweza kuamua tu kindugu mtoto watampa kidogo..... aikua issue kabisa kichwani mwangu

MSIMAMO WAO NI MTOTO AKAISHI TANGA
Nyumba ipo Tanga? Au ipo mkoa mwingine?
Muhimu linda sana uhai wa mtoto,kama wakiamua kumdhulumu mjukuu wao waache, muandalie mtoto wako kesho yake, baaasi
 
Back
Top Bottom