Ushauri: Katika kuhamasisha matumizi ya barakoa, Rais Magufuli, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, mkijitokeza hadharani ni vizuri muwe mmevaa barakoa

Ushauri: Katika kuhamasisha matumizi ya barakoa, Rais Magufuli, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, mkijitokeza hadharani ni vizuri muwe mmevaa barakoa

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Nashauri katika kupambana na ugonjwa corona, viongozi wakuu wa kitaifa kwa maana ya Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, wawe wanavaa barakoa kila wanapojitokeza hadharani iwe ni katika mikutano na waandishi wa habari ingawa mikutano hii nayo inapaswa kuepekuwa au waendapo kusali katika nyumba za Ibada.

Vile vile ikitokea wanaenda kufanya manunuzi basi wavae mask ili kuhamasisha wananchi wengine kuvaa mask.

Na ikiwezekana, mfano Rais, anaweza kufanya shopping ya makusudi tu huku akiwa amevaa barakoa lengo likiwa ni kuhamasisha wananchi watumie barakoa (hata kuigiza kwa aina hii kuna tija).

Vile vile haitakuwa na maana kuwataka wananchi wavae barakoa huku viongozi wakionekana hadharani au kwenye vyombo vya habari wakiwa hawajaavaa barakoa.

Uongozi ni kuonyesha njia.

Ni ushauri katika kupambana na corona.
 
Nampongeza sana yule katibu wa bunge ambaye huvaa Barakoa Bungeni tangu bunge hili la bajeti lilipoanza

Binafsi namchukulia kama mtu makini zaidi miongoni mwa watendaji wanaosaidia kuendesha shughuli za bunge kwa sababu anajijali mwenyewe na kuwajali wengine.

Juzi kati bunge zima la Botswana liliwekwa katika Karantini ya siku 14 baada ya mhudumu mmoja wa bunge kugundulika ana maambukizi ya Covid 19.

Vitakasa mikono na social distancing pekee hazitoshi Barakoa ni muhimu.

Maendeleo hayana vyama!
 
Haya mkuu!!
Wazo zuri sana hili. Chagamoto ni wazo linawafikiaje wahusika wakuu wa kuhamasisha. Mkulu akilianzisha hapo kama ulivyosema itapendeza sana. Kisha Hata wale wasanii ambao ni vioo vya jamii au wachezaji.

kina manara waposti kwenye account zao na hata ya simba ambayo ina wafuasi wengi wao wakiwsisitiza na wakiwa wamevaa barakoa, kina mo dewji etc...kwenye mitandao wachukue hatua ya kuhamasisha nao wakiwa wamevaa.
 
Wazo zuri sana hili. Chagamoto ni wazo linawafikiaje wahusika wakuu wa kuhamasisha. Mkulu akilianzisha hapo kama ulivyosema itapendeza sana. Kisha Hata wale wasanii ambao ni vioo vya jamii au wachezaji, kina manara waposti kwenye account zao na hata ya simba ambayo ina wafuasi wengi wao wakiwsisitiza na wakiwa wamevaa barakoa, kina mo dewji etc...kwenye mitandao wachukue hatua ya kuhamasisha nao wakiwa wamevaa.
Unamzungumzia nani wa kupokea ushauri huo? Huyo anayesema sishauriki?
Labda "Barakoa" zibadilishwe jina ziitwe "Hapa kazi tuu" na aitwe kuna kuzindua ndio ushauri hip utapokelewa.
Kwa nini hamtaki kumuelewa MTU huyo siku zote hizi?
 
Janga halijafikia level ya Makamu wa Rais au Rais kuanza kutoa up-to-date

Bado lipo level ya Waziri Mkuu

Tulieni serkali ipo kazini ,Nchi haiendeshwi kwa mihemuko yenu km mnavyodhani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nashauri katika kupambana na ugonjwa corona, viongozi wakuu wa kitaifa kwa maana ya Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, wawe wanavaa barakoa kila wanapojitokeza hadharani iwe ni katika mikutano na waandishi wa habari ingawa mikutano hii nayo inapaswa kuepekuwa au waendapo kusali katika nyumba za Ibada.

Vile vile ikitokea wanaenda kufanya manunuzi basi wavae mask ili kuhamasisha wananchi wengine kuvaa mask.

Na ikiwezekana, mfano Rais, anaweza kufanya shopping ya makusudi tu huku akiwa amevaa barakoa lengo likiwa ni kuhamasisha wananchi watumie barakoa (hata kuigiza kwa aina hii kuna tija).

Vile vile haitakuwa na maana kuwataka wananchi wavae barakoa huku viongozi wakionekana hadharani au kwenye vyombo vya habari wakiwa hawajaavaa barakoa.

Uongozi ni kuonyesha njia.

Ni ushauri katika kupambana na corona.
Umemtaja makamu hapo, Nina muda sijamsikia, au yeye hayupo kwenye usemaji wa Corona?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Salary Slip,
Ukitulizaga akili, una mawazo mazuri sana.
Naunga mkono hoja!
@barafuyamoto,ukweli ni kwamba sote tu Watanzania na naamini hao mnaowaita wapinzani wanaitakia mema sana Tanzania,tatizo la wewe na wenzako mliopo upande wa watawala mnaona kama "upinzani" ni usaliti.
Naamini kama upande wa watawala wataweka siasa za hovyo pembeni ni kuchukua kila wazo la wapinzani na kulifanyia analysis vyema,kuna mambo mengi ya msingi watagundua yanaweza kufanikiwa kuipeleka Tanzania mbele kwenye yale wanayoshauri hao wapinzani.
Acheni kujenga chuki wandugu.
 
Nashauri katika kupambana na ugonjwa corona, viongozi wakuu wa kitaifa kwa maana ya Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, wawe wanavaa barakoa kila wanapojitokeza hadharani iwe ni katika mikutano na waandishi wa habari ingawa mikutano hii nayo inapaswa kuepekuwa au waendapo kusali katika nyumba za Ibada.

Vile vile ikitokea wanaenda kufanya manunuzi basi wavae mask ili kuhamasisha wananchi wengine kuvaa mask.

Na ikiwezekana, mfano Rais, anaweza kufanya shopping ya makusudi tu huku akiwa amevaa barakoa lengo likiwa ni kuhamasisha wananchi watumie barakoa (hata kuigiza kwa aina hii kuna tija).

Vile vile haitakuwa na maana kuwataka wananchi wavae barakoa huku viongozi wakionekana hadharani au kwenye vyombo vya habari wakiwa hawajaavaa barakoa.

Uongozi ni kuonyesha njia.

Ni ushauri katika kupambana na corona.
hii ni kumpigia mbuzi gitaa mkuu.
 
Vaa kwa usalama wako kwa sababu Corona utaipata mwenyewe. Acha kuwa na mawazo mgando.
 
Back
Top Bottom