Gesi huchangia watoto kulia sana kwani wanapata maumivu katika tumbo- Azingatie anapomnyonyesha mtoto ahakikishe weusi wa ziwa umeingia katika mdomo wa mtoto yaani mtoto asinyonyeshwe chuchu tuu hii itasaidia kuepuka gesi kuingia tumboni kupitia mdomoni
Pili Kila mtoto akinyonya ahakikishe amebeua amweke begani amtikise taratibu mpaka abeue,
Joto linachangia mtoto kulia mpunguzie nguo mambo ya kumvika sweta,kanga,babyshow,shuka,blanketi hapana hii itachangia kumpa mtoto nimonia
Tatu: Mwambie Mungu akulele mtoto muombee mara zote mtoto wako kuna vitu vya rohoni huwa vinaendelea watoto wadogo wanauwezo wa kuona YESU pekee ndiye amfunike
Nne:Mtoto hashibi una maziwa mepesi ambayo muda mfupi tuu mtoto anapata njaa hivyo kuna wajumbe wamechangia juu namna ya ulaji wako uji ,mtori ,uji wa mchele nk.
Mwisho sio mbaya kumpa maji ya vugu vugu mtoto hata vijiko viwili .Japo wanasema maziwa ya mama yana maji lakini hata vichanga ni binadamu jamani.