Ushauri kuhusu kampuni kupata mkopo benki kabla haijaanza operations

Ushauri kuhusu kampuni kupata mkopo benki kabla haijaanza operations

DaPilly

Senior Member
Joined
Mar 2, 2012
Posts
181
Reaction score
68
ndugu wanajamii.
Ninaomba ushauri, nimeanzisha biashara ambayo haijaanza kufanya kazi. Nilikopa SACCOS nikaanza kujenga eneo la ofisi, na mahitaji mengine yanayohitajika katika kuuza bidhaa ninayotaka kuuza. Sijamaliza maandalizi ya ninachotaka kuuza pesa imekata, je naweza kurejister kampuni nikapata mkopo benki kama kampuni mauzo ya kitu ninachotaka kuuza ni kama 30000 kwa siku. Please advise
 
Unakazi ngum sana kwenye hili na changamoto zake ni kubwa sana.
Kwanza nawasiwasi wa Uelewa wako wa Biashara za kupitia mitaji ya mikopo.

Unapotaka kukopa ni lazima uwe na mipango ya nini unafanya na kiasi gani kinatakiwa.
Sasa wewe unajenga Ofisi halafu pesa ya Bidhaa huna.
Then unasema kwamba una uhakika wa kuingiza elf 30,000 kama faida kwa siku.Hii ikimaanisha kwamba ni biashara yenye kuhitaji mtaji mkubwa kiasi.

Ungekuwa hujakopa ningekushauri kwamba usingekopa kwanza mpaka mchango wako kwenye Saccoss ufikie malengo yako.
Tatizo ulikurupuka kwa Tamaa,sasa ngoma imakaba shingo.
Tafuta mtu umpe wazo kisha mchangie mtaji,peke yako ni ngum sana na huwezi kupata pa kukopa labda uweke dhamana ya nyumba.

Na hata ukisajili kama kampuni kuna taratibu za watoa mikopo kuangalia mradi na mwaka gani umeanza na umezalisha kitu gani mpaka hapo au Bank statement na pia dhamana za Nyumba amabazo hupendelewa sana na mabank.So,sio Rahisi kabisa
 
ndugu wanajamii.
Ninaomba ushauri, nimeanzisha biashara ambayo haijaanza kufanya kazi. Nilikopa SACCOS nikaanza kujenga eneo la ofisi, na mahitaji mengine yanayohitajika katika kuuza bidhaa ninayotaka kuuza. Sijamaliza maandalizi ya ninachotaka kuuza pesa imekata, je naweza kurejister kampuni nikapata mkopo benki kama kampuni mauzo ya kitu ninachotaka kuuza ni kama 30000 kwa siku. Please advise

Kwa uzoefu wangu Akiba commercial bank(ACB) wanaweza kutoa mkopo kwa RIBA ya 27% p.a ambayo ni solidarity loan inayotoka kwa speed group ya watu 5 Watano wanao weka self guarantee within themselves with no collateral na unaweza benefit kwa kukopa mpaka 20m ila ni lazima uanzie na kiwango cha chini.
•Mkopo ni kwa biashara zinazoendelea
•Payment schedules ni za mwezi kwa mwezi
•Sio lazima uwe na kampuni waweza sajili business name au hata ukiwa na biashara isiyo Rasmi pia unakuwa considered
•Uwe na permanent residence hii ni muhimu Kama biashara yako siyo Rasmi

Hope ntakuwa nimesaidia kidogo


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Unaweza kukopa ila kuna ugumu kidogo. Jaribu kutembelea wale wanaotoa mikopo na kuongea nao.

Biashara ingeshaanza ingekuwa rahisi ila sasa utapata vikwazo kidogo!
 
Unakazi ngum sana kwenye hili na changamoto zake ni kubwa sana.
Kwanza nawasiwasi wa Uelewa wako wa Biashara za kupitia mitaji ya mikopo.

Unapotaka kukopa ni lazima uwe na mipango ya nini unafanya na kiasi gani kinatakiwa.
Sasa wewe unajenga Ofisi halafu pesa ya Bidhaa huna.
Then unasema kwamba una uhakika wa kuingiza elf 30,000 kama faida kwa siku.Hii ikimaanisha kwamba ni biashara yenye kuhitaji mtaji mkubwa kiasi.

Ungekuwa hujakopa ningekushauri kwamba usingekopa kwanza mpaka mchango wako kwenye Saccoss ufikie malengo yako.
Tatizo ulikurupuka kwa Tamaa,sasa ngoma imakaba shingo.
Tafuta mtu umpe wazo kisha mchangie mtaji,peke yako ni ngum sana na huwezi kupata pa kukopa labda uweke dhamana ya nyumba.

Na hata ukisajili kama kampuni kuna taratibu za watoa mikopo kuangalia mradi na mwaka gani umeanza na umezalisha kitu gani mpaka hapo au Bank statement na pia dhamana za Nyumba amabazo hupendelewa sana na mabank.So,sio Rahisi kabisa

Asante kwa majibu maridhawa ila umekuwa mkaliiiiiii!!!!
 
kama umeshindwa kubalance mkopo wako na ukajikuta umeishia kwenye maandalizi ya ofisi nina wasiwasi hata mchanganuo wa hiyo biashara kwamba inaingiza faida ya elfu 30 kwa siku itakuwa na utata
ndugu kwa utaratibu ulioutumia inaweza ikakugharim baadae
ila kama una dhamana unaweza ukajitosa kwa mara nyingine kwenda kukopa, ila inatakiwa uandae A-Z matumizi na marejesho bora ya ya huo mkopo
 
Back
Top Bottom