Ushauri kuhusu namna ya kutanua masoko na kukuza mtaji

encyclopaedia Tanzaree

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2017
Posts
515
Reaction score
405
Mimi ni mfanyabiashara wa dagaa za Mwanza za kukaanga pamoja na samaki kutoka Mwanza, nimeanza biashara hiyo nina mwezi mmoja.

Changamoto kubwa ninayokutana nayo ni gharama kubwa za uendeshaji. Mtaji mdogo na soko la uhakika.

Naomba ushauri wenu namna gani naweza kupanua masoko, kupata mtaji na kupunguza gharama za uendeshaji hasa usafirishaji. kwa sasa natumia njia ya mabasi kufikisha bidhaa huku Dar.

Pia kama kuna mdau anaweza kunisaidia namna gani naweza kupata mkopo kwa kutumia cheti cha usajili cha BRELA nitashukuru sana kwan bado sina leseni ya biashara kwa sababu sina ofisi.

NATANGULIZA SHUKRANI ZA DHATI!
 
BIASHARA YA DAGAA KWANZA TAMBUA KWAMBA INAFANYWA NA KILA MTU.

Yanii watu wengi wanaifanya hivyo unacho takiwa kufanya ni kuja na mbinu mpya.

Nina uhakika Dagaa zako hazina tofauti na za mwingine na mwingine hivyo lazima ujiulize swali hili.
JE NI KWA NINI WATEJA WA NUNUE KWAKO NA SI KWA WENGINE ILIHALI KUNA UFANANO WA 100%

Sasa fanyoa kazi sababu ya kwa nini wanunue wako.

1. Unaweza jitofautisha na wenzako kwenye packeging ingawa in long run na wenzako wataiga tu.

2. Kuja na ainanyofauti au Radha tofauti.

3. Distribution Chanel mpaya

KWENYE KUPUNGUZA GHARAMA

Fanya vitu vingi wewe mwenyewe, jitoe ufahamu.

2. Tumia familia yako wao wawe kama ndo labour au ndugu na jamaa

3. Kama huwa unakaanga mwenyewe unaweza tafuta product ya kusapoti hiyo kwa gharama.

Yaani mfano unakaanga Mandazi, au unapikaga vitu vingine so vinakuwa vina share cost za Nishati kama mkaa au gesi.

Wengine watakushauri zaidi.

NB: Unaweza tafuta masoko ambayo hayajafikiwa kabisa
 
Asante sana ndugu yangu kwa kunifanya ufaham wangu upanuke zaid, mimi kwasasa nipo chuon mwaka wa kwanza naingia wa pili... katika short run naweza kusema kwa kias fulan najitahid kutumia weaknesses za competitors wangu kupata advantage, lakin kinachoniumiza kichwa ni long run ambapo najua baadh ya watu wataiga packaging zetu, radha n.k
sasa swali ni je, nifanye mambo gan saiz ili nipate uhakika wa faida katika long run?
 
Kuna jamaa yangu katapeliwa katika biashara hiyo, Mtaji wa mil 3 umeliwa na mjanja falani. Fanya kwa kiasi mpaka utapokuwa tayari au acha chuo kama inakulipa.
 
Ili wassiige lazima utumia Techinolojia utakayo wachukua pesa nyingi au muda mwingi ku copy.
 
Ili wassiige lazima utumia Techinolojia utakayo wachukua pesa nyingi au muda mwingi ku copy.
Mkuu nakuelewaga San katik aha mambo na UA nakufuatilia San kweny thread zako ,,,upo vizur San BT Nina maswql mengi San kuhus wew naiman utaniongezea mawazo +ve
 
Hivi wadau kwa laki nne hapa Dsm unaweza fanya Biashara Gani ukakeep Mtaji na kupata hela ya kula na kuzuga ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…