Ushauri: Kuku wangu wamepunguza kutaga

Ushauri: Kuku wangu wamepunguza kutaga

Joined
Dec 8, 2012
Posts
31
Reaction score
8
Habari za kazi wana JF. Mimi nina kuku wa kisasa takribani 300. Ni wale wekundu na ni wa mayai. Tangu mwezi huu wa sita uanze, kuku hao wameacha kutaga kabisa. Ni leo tu nimeokota yai moja na lenyewe ni kadogo kama ka yai ka njiwa. Sielewi ni sababu gani hasa , kwani hapo nyuma walikuwa wanataga vizuri. Wana miezi 2 tangu waanze kutaga. Naomba ushauri wenu ndugu zangu kwani imenichanganya ukizingatia chakula cha kuku kila leo kinapanda bei. Ninaishi Mbeya eneo linaitwa ITUHA. AU je , kwa vile hivi sasa ni kipindi cha baridi, inaweza kuwa sababu? Mbona nina kuku wa kienyeji wana enda vizuri? Wana JF , NAOMBA USHAURI WENU, na MUNGU AWABARIKI SANA.
 
kwanza kabisa mkuu angalia aina ya chakula unachowalisha, lkn pia unafugia mkoa gani?? kama ni mikoa ya baridi kutaga kwa hao kuku kutakuwa ni kwa shida sana as chakula kingi wanachokula kinakwenda kutengeneza nguvu na joto mwilini zaid ya kutengeneza mayai.
 
Nashukuru kwa ushauri wako mzuri. Niko MBEYA. Chakula nawapa mchanganyo wa siku zote kwa namna alivyo nishauri mtaalam. Au labda kuna chakula mbadala? Nikiwa nawatoa nje kwenye jua itaathiri?
 
mkuu msimu n wa baridi huu kama unachumba kinacho weza kuwapatia joto la zaidi unge waweka pia unashauriwa uwape vyakula vya kuongeza joto kama mashudu na dam hapo mambo yanaweza kwenda vizuri
 
mkuu msimu n wa baridi huu kama unachumba kinacho weza kuwapatia joto la zaidi unge waweka pia unashauriwa uwape vyakula vya kuongeza joto kama mashudu na dam hapo mambo yanaweza kwenda vizuri
NDUGU YANGU, NASHUKURU KWA USHAAURI MZURI, NITAZINGATIA NA NITATOA FEEDBACK KWA WANA JF. Asante sana.
 
PIA NAPENDA KUMSHUKURU MAMA JAMES WA EXTERNAL UBUNGO KWA USHAURI WAKE KUPITIA SIMU YA MKONONI. Mama Asante sana umenipa mwanga mkubwa. Mungu akubariki katika biashara zako, AMEN
 
kwanza kabisa mkuu angalia aina ya chakula unachowalisha, lkn pia unafugia mkoa gani?? kama ni mikoa ya baridi kutaga kwa hao kuku kutakuwa ni kwa shida sana as chakula kingi wanachokula kinakwenda kutengeneza nguvu na joto mwilini zaid ya kutengeneza mayai.

hapo kwa red, nimekubali kweli dada yangu we ni biologist, umenikumbusha ile dhana kwamba watu wanaoishi sehemu za baridi wanakula sana!
 
Leonard
Mimi nina kuku 496 na wana wiki 26 walianza kutaga vizuri lakini katika wiki ya 26 na 27 wameanza kupunguza kutaga kutoka tray 12 mpaka tray 10 na wakati mwingine wanarudi tray 11 .nipo Dar es Salaam na sijawahi kubadiri chakula tatizo linaweza kuwa nn
 
Back
Top Bottom