Ushauri kwa Mbowe: Vunja kitengo cha mawasiliano cha CHADEMA, kisuke upya

Ushauri kwa Mbowe: Vunja kitengo cha mawasiliano cha CHADEMA, kisuke upya

Petition

Senior Member
Joined
May 28, 2014
Posts
139
Reaction score
212
Wapendwa wakuu humu jamvini:

Huu ni wakati wa Kampeni na Uchaguzi mkuu. Nguzo kubwa ya ushindi katika uchaguzi ni communication (mawasiliano). Kwa maana ya kwamba lazima wapiga kura wafikiwe kwa ujumbe na ilana ya chama kwa ufasaha na kwa haraka, na ujumbe huu urudiwe mara kwa mara kwenye media zinazowezekana ili mambo hayo yaeleweke vizuri kwa wapiga kura.

Sasa tunajua kuwa CCM ina access au imeshaweka mfukoni media zote (esp. TV na magazeti) na lengo lao ni kuhakikisha wapinzani sera zao hazisikiki na hazieleweki.

Sasa nilitaraji vyama vya upinzani vyenye akili, ikiwemo Chadema vingewekeza nguvu nyingi kwenye mass communication ya messages na habari za mgombea uraisi na wagombea wengine. LAKINI MAMBO YAMEKUWA TOFAUTI SANA, kitengo cha ICT cha Chadema kimelala sana na bado kinafanya mambo yake kizamani na KIZEMBE sana.

Mfano: inashindikana vipi kurusha LIVE kwenye mikutano ya LISSU na wagombea wengine na kuweka pia recorded messages? Wanashindwa vipi kuwa na special Channel au website ambapo kutakuwa na links kwenda kwenye information resources mbalimbali zinazohusu uchaguzi. Vile vile nilitegemea kutengenezwe jumbe mbalimbali fupifupi za ahadi na sera ya chama na kusambazwa kwa wingi kwenye mitandao.

Hii haiitaji fedha nyingi, ni kiasi cha kuchukua vijana ambao walio smart wa ICT wa kutengeneza brief online contents na kusambaza kila mahali mitandaoni. Hii ni pamoja na kutengeneza fliers au vipepereshi vingi vye picha ya Lissu na jumbe mbalimbali fupi za sera na ahadi na kuzigawa kila sehemu mfano kwenye traffick lights, masokoni, vijiwe vya bodaboda, vituo vya mabasi, n.k n.k

MBOWE, MNYIKA na CHADEMA, bado hamjachelewa, VUNJENI HICHO KITENGO CHA MAWASILIANO na kisukwe upya kwa kuweka vijana smart chini ya kiongozi mwenye weledi. Ikiwezekana ACHANA NA TUMAINI MAKENI AMBAYE BADO ANAFANYA MAMBO KWA MAZOEA NA KIGOIGOI SANA.

Mfano: hotuba na mkutano wa LISSU Arusha ulikuwa na nondo na maelezo fasaha sana ya ilani na sera za CHADEMA lakini ilikuwa shida sana kupata sehemu unayoweza kuangalia Live au hata walau kuangalia ambayo iko recorded. KAMA HAMWEZI KUWA NA EFFECTIVE COMMUNICATION MECHANISM BASI NA IKULU HAMTAIWEZA.

Nawasilisha
 
Wapendwa wakuu humu jamvini:

Huu ni wakati wa Kampeni na Uchaguzi mkuu. Nguzo kubwa ya ushindi katika uchaguzi ni communication (mawasiliano). Kwa maana ya kwamba lazima wapiga kura wafikiwe kwa ujumbe na ilana ya chama kwa ufasaha na kwa haraka, na ujumbe huu urudiwe mara kwa mara kwenye media zinazowezekana ili mambo hayo yaeleweke vizuri kwa wapiga kura.

Sasa tunajua kuwa CCM ina access au imeshaweka mfukoni media zote (esp. TV na magazeti) na lengo lao ni kuhakikisha wapinzani sera zao hazisikiki na hazieleweki.

Sasa nilitaraji vyama vya upinzani vyenye akili, ikiwemo Chadema vingewekeza nguvu nyingi kwenye mass communication ya messages na habari za mgombea uraisi na wagombea wengine. LAKINI MAMBO YAMEKUWA TOFAUTI SANA, kitengo cha ICT cha Chadema kimelala sana na bado kinafanya mambo yake kizamani na KIZEMBE sana.

Mfano: inashindikana vipi kurusha LIVE kwenye mikutano ya LISSU na wagombea wengine na kuweka pia recorded messages? Wanashindwa vipi kuwa na special Channel au website ambapo kutakuwa na links kwenda kwenye information resources mbalimbali zinazohusu uchaguzi. Vile vile nilitegemea kutengenezwe jumbe mbalimbali fupifupi za ahadi na sera ya chama na kusambazwa kwa wingi kwenye mitandao. Hii haiitaji fedha nyingi, ni kiasi cha kuchukua vijana ambao walio smart wa ICT wa kutengeneza brief online contents na kusambaza kila mahali mitandaoni. Hii ni pamoja na kutengeneza fliers au vipepereshi vingi vye picha ya Lissu na jumbe mbalimbali fupi za sera na ahadi na kuzigawa kila sehemu mfano kwenye traffick lights, masokoni, vijiwe vya bodaboda, vituo vya mabasi, n.k n.k

MBOWE, MNYIKA na CHADEMA, bado hamjachelewa, VUNJENI HICHO KITENGO CHA MAWASILIANO na kisukwe upya kwa kuweka vijana smart chini ya kiongozi mwenye weledi. Ikiwezekana ACHANA NA TUMAINI MAKENI AMBAYE BADO ANAFANYA MAMBO KWA MAZOEA NA KIGOIGOI SANA.

Mfano: hotuba na mkutano wa LISSU Arusha ulikuwa na nondo na maelezo fasaha sana ya ilani na sera za CHADEMA lakini ilikuwa shida sana kupata sehemu unayoweza kuangalia Live au hata walau kuangalia ambayo iko recorded. KAMA HAMWEZI KUWA NA EFFECTIVE COMMUNICATION MECHANISM BASI NA IKULU HAMTAIWEZA.

Nawasilisha
Hili Jambo limesha ongelewa sana hapa na kwingineko mtandaoni lakini halifanyiwi kazi
Hapa ndio nikaanza kuidharau Chadema, hawajajipanga kabisa. Wamekuwa tu maarufu sababu ya udhaifu wa CCM.
 
Hicho kitengo ni Cha kubadilisha mara moja ndio maana Lowassa alikuwa na kitengo chake, Lisu anzisha kitengo Cha ushauri nje ya hiki Cha chama huko wamejaa mazuzu wanafanya kazi kwa mazoea,
Kwanza huyu Tumaini yawezekana siyo mwanachama wa chadema atakuwa wa kule mke wake alikotangulia kwenda anasubiria muda naye asepe huyu siyo wa kuamini,,,,,Mh Lisu anzisha kitengo chako Cha vijana wa IT Mara moja Kama mzee Lowassa,,
 
Kama huwa wanapata ruzuku ya mil 300 kila mwezi kwa miaka 5 iliyopita lakini hata ofisi ndogo tu ya milioni kama 50 wameshindwa kujena ni kupanga tu sasa wewe unategemea nini wao kuwekeza kwenye social media.Chadema kwa kweli bado haijakaa kama taasis na wana shida kubwa kuhusiana matumizi yao ya hela.wana watu ambao nadhani bado wanapata kauzibe toka kwa Mbowe na wenzake.Mbowe inaabidi awaachie damu mpya
 
Back
Top Bottom