Ushauri kwa Serikali juu ya kazi za Sensa

Ushauri kwa Serikali juu ya kazi za Sensa

Tafakari yetu

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2021
Posts
1,505
Reaction score
4,427
Kwa wote wanaohusika,

Awali napenda kuipongeza Serikali kwa kuja na wazo la maombi ya kazi za Sensa kufanyika ONLINE na katika hili Urasimu umepungua Sana kutofautisha na njia iliyotumika kwenye ANUANI ZA MAKAZI NA POSTIKODI ambapo ilifanya nafasi zitolewe kwa kujuana na hivyo wenye sifa kuenguliwa na wasio na sifa kupewa nafasi.

Ni ukweli usiosemwa lakini mchakato uliotumika kupata watu wa kwenye zoezi la ANUANI za makazi liligubikwa na utata usioelezeka na tulipoona application za ajira hizi za sensa zitafanyika ONLINE tukashukuru na kusema tatizo limetatuliwa lakini yanaenda yanaenda kujirudia yale yanayoumiza.

Kitendo Cha kuruhusu mchakato wa ajira za sensa kwa hatua ya mchujo kufanywa na watendaji wa kata/mtaa ni kuruhusu yaliyotokea kwenye ANUANI ZA MAKAZI NA POSTIKODI kujirudia, hivyo tunaomba Serikali itazame mchakato huu.

Kwa kuwa kila mtu aliyeomba nafasi hizo anajua ni mkazi wa eneo husika na fomu ya maombi inajieleza hakuna haja ya kutumia watendaji ili kuthibitisha ukazi wa muombaji. Yanayofanywa na watendaji yanaumiza maana bila koneksheni ni ngumu kupita kwao.

Mapendekezo:

1. Kama mnataka watendaji wawe sehemu ya mchujo basi msitumie watendaji wa eneo hilo kuchuja watu walioomba eneo hilohilo na badala yake kwa mfano watendaji wa wilaya ya masasi wanaweza kufanya mchujo wa waombaji wa tanga hii itapelekea Usawa ilhali hujuma haziwezi kukosekana.

2. Wakati wa usaili ,kwa kuwa tumeamua kutumia njia za kisasa wakati wa kufanya application basi twende na usasa huohuo kwa interview kufanyika ONLINE. Kufanya interview hiyo online itasaidia kupunguza upendeleo

Katika kufanya usaili online pia inaweza kuboreshwa watu wasailiwa wanaweza kukutana ofisi ya kata kwa ajili ya interview na unaweza kutengenezwa mfumo wa maswali ya interview ambao ili kuingia kwenye mfumo kushiriki interview lazima uwe na password na password hiyo inatolewa ofisini tu. Hii itafanya watu watumie simu zao kwa ajili ya interview lakini muda wa interview mfumo usiowaruhusu kutoka nje ya mfumo na wakifanya hivyo watakuwa wamejiondoa.
 
USHAURI NI MZURI SANA JAPO UNA MAREKEBISHO KIDOGO KATIKA MASUALA MBALIMBALI.

NANI WA KUUFIKISHA?

NANI WA KUUFANYIA KAZI?

JE, MUDA UNATOSHA!!?

MNAMFAHAMU VIZURI ANNA MAKINDA?
 
Kwa wote wanaohusika,

Awali napenda kuipongeza Serikali kwa kuja na wazo la maombi ya kazi za Sensa kufanyika ONLINE na katika hili Urasimu umepungua Sana kutofautisha na njia iliyotumika kwenye ANUANI ZA MAKAZI NA POSTIKODI ambapo ilifanya nafasi zitolewe kwa kujuana na hivyo wenye sifa kuenguliwa na wasio na sifa kupewa nafasi.

Ni ukweli usiosemwa lakini mchakato uliotumika kupata watu wa kwenye zoezi la ANUANI za makazi liligubikwa na utata usioelezeka na tulipoona application za ajira hizi za sensa zitafanyika ONLINE tukashukuru na kusema tatizo limetatuliwa lakini yanaenda yanaenda kujirudia yale yanayoumiza.

Kitendo Cha kuruhusu mchakato wa ajira za sensa kwa hatua ya mchujo kufanywa na watendaji wa kata/mtaa ni kuruhusu yaliyotokea kwenye ANUANI ZA MAKAZI NA POSTIKODI kujirudia, hivyo tunaomba Serikali itazame mchakato huu.

Kwa kuwa kila mtu aliyeomba nafasi hizo anajua ni mkazi wa eneo husika na fomu ya maombi inajieleza hakuna haja ya kutumia watendaji ili kuthibitisha ukazi wa muombaji. Yanayofanywa na watendaji yanaumiza maana bila koneksheni ni ngumu kupita kwao.

Mapendekezo:

1. Kama mnataka watendaji wawe sehemu ya mchujo basi msitumie watendaji wa eneo hilo kuchuja watu walioomba eneo hilohilo na badala yake kwa mfano watendaji wa wilaya ya masasi wanaweza kufanya mchujo wa waombaji wa tanga hii itapelekea Usawa ilhali hujuma haziwezi kukosekana.

2. Wakati wa usaili ,kwa kuwa tumeamua kutumia njia za kisasa wakati wa kufanya application basi twende na usasa huohuo kwa interview kufanyika ONLINE. Kufanya interview hiyo online itasaidia kupunguza upendeleo

Katika kufanya usaili online pia inaweza kuboreshwa watu wasailiwa wanaweza kukutana ofisi ya kata kwa ajili ya interview na unaweza kutengenezwa mfumo wa maswali ya interview ambao ili kuingia kwenye mfumo kushiriki interview lazima uwe na password na password hiyo inatolewa ofisini tu. Hii itafanya watu watumie simu zao kwa ajili ya interview lakini muda wa interview mfumo usiowaruhusu kutoka nje ya mfumo na wakifanya hivyo watakuwa wamejiondoa.
Hao watendaji wenyewe asilimia 80 zoezi la sensa jipya kwao wengi wao kipindi zoezi hili linafanyika mwaka 2012 wengi walikuwa shule tena sekondari hawana uelewa wowote zoezi lilivyo zaidi ya kujua ni zoezi la kuhesabu watu so kuwatumia hao kufanya usaili ni kama kuwatwisha mzigo tu, maana hata wao wanaitaji elekezwa hawajui ugumu wa zoezi hili lilivyo

Ushauri wangewatumia watu ambao ni watumishi katika kata zao ambao Wana uzoefu wa zoezi hili na walilifanya mwaka 2012, ambao hawajasahau ugumu wa kushedi😂😂😂 so watumiwe hawa kuwepo kwenye jopo usaili

Japo naamini sensa ya mwaka huu itakuwa kitigital zaidi na namini changamoto za network hazitaepukika so watu wa TEHAMA jiandaeni kisaikolijia kukesha mkingiza data
 
Nimeishia hapo unasema mtendaji wa Mtwara akathibitishe wakazi wa Tanga, nini maana ya kuthibitisha makazi?

Hii nchi uhuru wa maoni umezidi sasa.
 
Nimeishia hapo unasema mtendaji wa Mtwara akathibitishe wakazi wa Tanga, nini maana ya kuthibitisha makazi?

Hii nchi uhuru wa maoni umezidi sasa.
Ungesoma tangazo la ajira kwanza kabla ya kunijibu.
 
Back
Top Bottom