CK Allan
JF-Expert Member
- Aug 14, 2013
- 2,781
- 6,139
Leo niwashauri wale ambao hamjaoa au kuolewa ila mpo kwenye mahusiano sijui uchumba au nini:
Onyesheni zile tabia zenu halisi, yaani usiigize chochote, kama wewe unakula sana, kula, kama wewe huwa unaoga kwa wiki mara moja tu basi fanya hivyo, kama huwa husalimii watu basi endelea. Yaani kila tabia yako muonyeshee huyo 'baby' wako.
Hata mkija kuoana mtaishi maisha yale yale tu, tena hutapata shida!
Kuna watu waliigiza kwenye uchumba, sasa kwenye ndoa ndiyo wapo nyuma ya pazia!
Narudia tena, kama unavuta bangi zako, basi vuta huyo mpenzi wako akiwepo au ajue kabisa unavuta bangi. Kama wewe huwa unatukana au kuchamba wamama watu wazima basi usijizuie eti kisa mpenzi wako yupo!
Narudia tena kila mtu na mtuwe! Usiigize wala kuigiza maana baadaye utakuja kupata shida sana kuishi katika uhalisia wako! Wacha ajue tabia yako mapema ili aamue kusuka au kunyoa.
Mkienda kwenye ndoa ni kwamba tayari mmekubaliana na jinsi mlivyo!
Onyesheni zile tabia zenu halisi, yaani usiigize chochote, kama wewe unakula sana, kula, kama wewe huwa unaoga kwa wiki mara moja tu basi fanya hivyo, kama huwa husalimii watu basi endelea. Yaani kila tabia yako muonyeshee huyo 'baby' wako.
Hata mkija kuoana mtaishi maisha yale yale tu, tena hutapata shida!
Kuna watu waliigiza kwenye uchumba, sasa kwenye ndoa ndiyo wapo nyuma ya pazia!
Narudia tena, kama unavuta bangi zako, basi vuta huyo mpenzi wako akiwepo au ajue kabisa unavuta bangi. Kama wewe huwa unatukana au kuchamba wamama watu wazima basi usijizuie eti kisa mpenzi wako yupo!
Narudia tena kila mtu na mtuwe! Usiigize wala kuigiza maana baadaye utakuja kupata shida sana kuishi katika uhalisia wako! Wacha ajue tabia yako mapema ili aamue kusuka au kunyoa.
Mkienda kwenye ndoa ni kwamba tayari mmekubaliana na jinsi mlivyo!