Ushauri kwa wanaotaka kuwekeza kwenye kilimo cha papai

Ushauri kwa wanaotaka kuwekeza kwenye kilimo cha papai

Mkulima na Mfugaji

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2013
Posts
1,047
Reaction score
1,832
Habari wakulima na wafugaji wenzangu, kumekuwa na malalamiko mwengi siku hizi kwa wakulima wanaotaka kuwekeza kwenye kilimo cha papai kwamba wanakutana na mipapai dume mingi pindi wanaponunua miche ya mipapai kutoka kwa wazalishaji wa vitalu ya miche hiyo.

Siku hizi watu wamekuwa sio waaminifu, mtu anaweza kununua papai sokoni bila kujua aina ya mbegu akaja akaotesha miche kisha akaipachika jina lolote analojua yeye halafu akauzia watu, papai likishachakachuliwa mara nyingi lazima lipungue ubora na pia lazima upate mipapai dume mingi hata 50 kwa 50 kwani mbegu hybrid lazima ipatikane mbegu yenye sifa ya kike na ya kiume kwa hiyo kama itachakachuliwa sana inarudi kwenye sifa zake za awali.

NINI CHA KUFANYA?
Kama unataka kuwekeza kwenye kilimo cha papai na uwezo wako ni mdogo, nenda kwenye duka la pembejeo linaloeleweka nunua mbegu chotara inayojulikana hata ya Tsh 15,000 kisha otesha miche yako mwenyewe uitunze kwa uangalifu, ikishaanza kuzaa hapo unaweza kuchagua mipapai bora ukaotesha kitalu chako unachohitaji na idadi ya miche yoyote unayotaka. Hapo miche yako itakuwa ni bora kwani huo ni uzazi wa kwanza hivyo inakuwa haijapoteza ubora wake kwa kiasi kikubwa.

Kwa leo inatosha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari wakulima na wafugaji wenzangu, kumekuwa na malalamiko mwengi siku hizi kwa wakulima wanaotaka kuwekeza kwenye kilimo cha papai kwamba wanakutana na mipapai dume mingi pindi wanaponunua miche ya mipapai kutoka kwa wazalishaji wa vitalu ya miche hiyo.

Siku hizi watu wamekuwa sio waaminifu, mtu anaweza kununua papai sokoni bila kujua aina ya mbegu akaja akaotesha miche kisha akaipachika jina lolote analojua yeye halafu akauzia watu, papai likishachakachuliwa mara nyingi lazima lipungue ubora na pia lazima upate mipapai dume mingi hata 50 kwa 50 kwani mbegu hybrid lazima ipatikane mbegu yenye sifa ya kike na ya kiume kwa hiyo kama itachakachuliwa sana inarudi kwenye sifa zake za awali.

NINI CHA KUFANYA?
Kama unataka kuwekeza kwenye kilimo cha papai na uwezo wako ni mdogo, nenda kwenye duka la pembejeo linaloeleweka nunua mbegu chotara inayojulikana hata ya Tsh 15,000 kisha otesha miche yako mwenyewe uitunze kwa uangalifu, ikishaanza kuzaa hapo unaweza kuchagua mipapai bora ukaotesha kitalu chako unachohitaji na idadi ya miche yoyote unayotaka. Hapo miche yako itakuwa ni bora kwani huo ni uzazi wa kwanza hivyo inakuwa haijapoteza ubora wake kwa kiasi kikubwa.

Kwa leo inatosha

Sent using Jamii Forums mobile app
Swali. Kuna mipapai inachukua miezi 3 toka kupandwa hadi kuanza kuvunwa?
 
IMG_1044.jpg

Malikia f1 imepigwa dawa ya ukungu mara 1tu mbolea samadi haikuwah kumwagiliwa maji papai moja kubwa shambani nauza 1000/=singida
 
Hio miti ina muda gani? Kwa hio unatuthibitishia dawa sio lazima.
Vipi soko halisumbui?

Ukizingatia usafi shambani na kuwepo na mvu za wastani haishambuliwi na wadudu ila siwezi kudhibitisha hilo maana nyakati zinabadilika ila hapa kwangu sikuwahi kupiga dawa kuhusu soko kidogo nichangamoto nilitafuta wanauza matunda sokoni na magengeni kadha nikawa nawapelekea ilisaidia kidogo japokuwa wengine walinikopa nahawakulipa ila nilikifunza kwa vitendo
 
Back
Top Bottom