Ushauri: Kwenye matamasha hakuna haja kuleta wasanii wa nje

Singida ndio home

JF-Expert Member
Joined
Feb 23, 2012
Posts
3,188
Reaction score
3,370
Nawapongeza wasafi kwa jitihada za kuwaleta kina medd, wizkid na tiwa savage katika tamasha la wasafi ila kama ilivyo kawaida wahudhuriaji wa show wamebaki tu kushangaa shangaa ni nini kinaendelea uwanja ukiwa umepoa sana bila shangwe.

Sidhani kama wamepokelewa kama walivyodhani kwa sababu wahudhuriaji wameonekana kutojua chochote kinachoimbwa kwa kiingereza ambacho wengi kimewapita kushoto.

Si hawa tu bali hata kina rick ross, jay z, n.k waliwahi kuja fiesta watu wakabaki wanashangaa shangaa tu.

Ni ushauri tu kwamba aina hii ya wasanii wana gharama kubwa kukodishwa ila wakifika hapa ni heri angelipwa hata man fongo kupafomu hainaga ushemeji ].\\\[[[[
 
hamna biashara ya hasara hapo, acheni watu wafanye mapinduzi, sio fiesta hiyo
 
Hakuna haja kweli kule kutoka nje,leo wiz kakomea tatu tu akachemsha ikabidi aje diamond aamshe aamshe,kama uliingia kwa ajili ya wiz imekula kwako
 
Baada ya Mondi kurudia wimbo na mziki kukata, show ikapwayaaaaa balaaaa. Wajipange vizuri next time, walipoteza muda sana mwanzoni wakati watu hawajachoka. Show ndefu sana. Wizkid kwanini hakuja na Dj wake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…