Ushauri: Matumizi sahihi ya Mswaki

Ushauri: Matumizi sahihi ya Mswaki

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Kuna baadhi ya tabia hupaswa kufuatwa ili afya ya kinywa na meno iweze kubaki imara siku zote.

9E88A18F-F67F-4530-B40A-1D06BF15A0F3.jpeg


Kwa mujibu wa Kituo Cha Udhibiti na Kinga ya Magonjwa cha Marekani (CDC), haya ndiyo mambo ya msingi kuzingatia unapokuwa unatumia mswaki wako.
  • Unashauriwa kubadili mswaki wako kila baada ya miezi 3-4, au muda wowote ule kabla ya hapo ikiwa tu utahisi kuwa ubora wake umepungua. Miswaki iliyopungua ubora wake hupunguza ufanisi wa kazi.
  • Usifunike mswaki wako kwenye chombo chochote baada ya kuutumia. Kitendo hiki husababisha kuzaliana kwa bakteria.
  • Hauhitaji kutakasa mswaki wako kwa sanitizer, spirit, kemikali zozote kali au kwa kutumia mionzi ili kuua bakteria wake. Vitendo hivi siyo salama kwa afya ya mtumiaji.
  • Safisha mswaki wako kwa maji tiririka, kisha uhifadhi kwa kuusimanisha. Kama sehemu husika ina zaidi ya mswaki mmoja, hakikisha haigusani.
  • Mswaki unaweza kusabambaza magonjwa. Hata kama ni ndugu, au mnapendana kiasi gani, kila mtu atumie mswaki wake.

Chanzo: CDC
 
Asante sana kwa taarifa..

Ila inashangaza wapendanao wasitumie mswaki mmoja ila French kiss ruksa.

Anyway tutunze afya ya vinywa vyetu kwa kusafisha si chini ya mara 2 kwa siku...kwakutumia mswaki na dawa nzuri ya meno.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom