ushauri na karipio kwa wajasiriamali

ushauri na karipio kwa wajasiriamali

Voice of Wisdom

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2011
Posts
537
Reaction score
240
wadau wa ujasiriamali poleni kwa majukumu ya kujenga uchumi wenu na taifa bila kusahau mafisadi.
Nimechukua hatua ya kuandika uzi huu baada ya kuona jambo hili linajirudia mara kwa mara na watu pengine hawajagundua kuwa ni TATIZO.
Nimekutana na post nyingi karibu kila mwezi post mpya yenye kichwa NINA MTAJI WA TSH .... NISHAURINI NIFANYE BIASHARA/KITU GANI?
Kiukweli hili swali si swali la kuulizwa na mjasiriamali.
Kwa nini?
Kwa sababu mjasiriamali yeyote mtaji si fursa ila wazo la nini cha kufanya ndiyo deal. Katika ujasiriamali watu hawaanzi kutafuta mtaji kwanza wanaanza na wazo la biashara yenyewe:
je ni biashara ya aina gani?
Soko lake likoje?
Upatikanaji wa bidhaa
washindani walioko sokoni (uwezo na udhaifu wao)
Jinsi ya kufika sokoni(miundombinu)
Sheria zikoje?
Mtaji utakaouhtaji? n.k
Mjasiriamali makini lazima afanye upembuzi wa biashara yake (business feasibility analysis).
Na katika upembuzi huo mtaji ni end product, mtaji si fursa, mtaji ni matokeo ya fursa uliyoiona na kuifanyia upembuzi. Tafuta fursa ndiposa utafute mtaji kulingana na fursa yenyewe.
Haihitaji elimu ya ujasiriamali kuona fursa ila moyo wa ujasiriamali.
Ujasiriamali huanzi na mtaji bali wazo la biashara
"NA HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU"
 
Mkuu si hili tu kuna thread nilianzisha ya njiza za kuweza kutumia kupata wazo borakabisa la Biashara, Tatizo watu ni wavivu wa kufikiri na wanzania Ujasirimai ni kitu simple, Belive or not kama kutafuta wo la bishara unahindwa hata biashara utashindwa kuendeha make haya mambo yanaendana pamoja,

uwezi ukatenganisha kuumiza kichw kutafuta wazo la baishara nakuendesha hiyo biashara,n badae mtu anarudu kuuliza sas niuze wapi? mara sijui nini,

ENTREPRENEURSHIP NI VERY COMPLICATED NA INAHITAJI UWAJIBIKJI WA KIWANGO CHA JUU KABISA
 
Mkuu si hili tu kuna thread nilianzisha ya njiza za kuweza kutumia kupata wazo borakabisa la Biashara, Tatizo watu ni wavivu wa kufikiri na wanzania Ujasirimai ni kitu simple, Belive or not kama kutafuta wo la bishara unahindwa hata biashara utashindwa kuendeha make haya mambo yanaendana pamoja,

uwezi ukatenganisha kuumiza kichw kutafuta wazo la baishara nakuendesha hiyo biashara,n badae mtu anarudu kuuliza sas niuze wapi? mara sijui nini,

ENTREPRENEURSHIP NI VERY COMPLICATED NA INAHITAJI UWAJIBIKJI WA KIWANGO CHA JUU KABISA

ukweli mchungu sawa na msumari wa moto kwenye kidonda. Watanzania tukubali kubadiliko.
Mtaji usikuamulie aina ya biashara ila aina ya biashara ikuamulie kiwango cha mtaji.
 
Wadau, kwanza me nadeclare interest; me ndo kwanza mgeni humu lakini najuta kwa nini nmechelewa ku2mbukia. Baada ya hayo nmeamini wa2 humu are very sereous for helping each other. Lets move pamoja regadless ya tofauti ze2 kifikra... Aksanteni.
 
wadau wa ujasiriamali poleni kwa majukumu ya kujenga uchumi wenu na taifa bila kusahau mafisadi.
Nimechukua hatua ya kuandika uzi huu baada ya kuona jambo hili linajirudia mara kwa mara na watu pengine hawajagundua kuwa ni TATIZO.
Nimekutana na post nyingi karibu kila mwezi post mpya yenye kichwa NINA MTAJI WA TSH .... NISHAURINI NIFANYE BIASHARA/KITU GANI?
Kiukweli hili swali si swali la kuulizwa na mjasiriamali.
Kwa nini?
Kwa sababu mjasiriamali yeyote mtaji si fursa ila wazo la nini cha kufanya ndiyo deal. kutKatika ujasiriamali watu hawaanzi afuta mtaji kwanza wanaanza na wazo la biashara yenyewe:
je ni biashara ya aina gani?

Hapo ndipo ilipo tofauti ya mjasiriamali wa kweli na anaye-copy na kupaka. Aliyeona fursa na kuitafutia mtaji huwa hakati tamaa, ila aliye na mtaji kisha akakutana na changamoto za kufa mtu, hukata tamaa, au hurukia biashara nyingine kwa kusikia simulizi za walio fanikiwa, asijue kila aliyefanikiwa kwa haki kapita changamoto kibao.
 
Hii thread ni ya ukweli lakini cha ajabu watu hawataki changia ila yote hii inatokana na michango yenu kwenda kinyume na wanavyotarajia au kuona wao..kiukweli ujasiriamali si kitu simple na ina taka moyo sana aisee big up wakuu..
 
Wadau, kwanza me nadeclare interest; me ndo kwanza mgeni humu lakini najuta kwa nini nmechelewa ku2mbukia. Baada ya hayo nmeamini wa2 humu are very sereous for helping each other. Lets move pamoja regadless ya tofauti ze2 kifikra... Aksanteni.

karibu mkuu, tujifunze ujasiriamali na biashara. Kumbuka biashara si mtaji ila idea ya biashara
 
wadau wa ujasiriamali poleni kwa majukumu ya kujenga uchumi wenu na taifa bila kusahau mafisadi.
Nimechukua hatua ya kuandika uzi huu baada ya kuona jambo hili linajirudia mara kwa mara na watu pengine hawajagundua kuwa ni TATIZO.
Nimekutana na post nyingi karibu kila mwezi post mpya yenye kichwa NINA MTAJI WA TSH .... NISHAURINI NIFANYE BIASHARA/KITU GANI?
Kiukweli hili swali si swali la kuulizwa na mjasiriamali.
Kwa nini?
Kwa sababu mjasiriamali yeyote mtaji si fursa ila wazo la nini cha kufanya ndiyo deal. kutKatika ujasiriamali watu hawaanzi afuta mtaji kwanza wanaanza na wazo la biashara yenyewe:
je ni biashara ya aina gani?

Hapo ndipo ilipo tofauti ya mjasiriamali wa kweli na anaye-copy na kupaka. Aliyeona fursa na kuitafutia mtaji huwa hakati tamaa, ila aliye na mtaji kisha akakutana na changamoto za kufa mtu, hukata tamaa, au hurukia biashara nyingine kwa kusikia simulizi za walio fanikiwa, asijue kila aliyefanikiwa kwa haki kapita changamoto kibao.

food of thought Malila, biashara haindeshwi na pesa ila wazo. Natamani watu waelewe changamoto kubwa ya biashara si mtaji ila wazo/mbinu za biashara yenyewe
 
Hii thread ni ya ukweli lakini cha ajabu watu hawataki changia ila yote hii inatokana na michango yenu kwenda kinyume na wanavyotarajia au kuona wao..kiukweli ujasiriamali si kitu simple na ina taka moyo sana aisee big up wakuu..

mkuu lymber watanzania tuna tabia ya kukimbia ukweli kwa kuona kama kuna mtu anataka kutufunga spidi ganana ktk harakati zetu.
Ukimshauri mtu kufanya research kabla ya kuanza biashara anakuchukia, ukimwomba mchanganuo wa biashara yake anaona kama unamchunguza! Mwisho wa siku tunabaki kulaumu na kulaumu biashara ngumu, wamenipga ndumba n.k
 
food of thought Malila, biashara haindeshwi na pesa ila wazo. Natamani watu waelewe changamoto kubwa ya biashara si mtaji ila wazo/mbinu za biashara yenyewe

Hapa tuko pamoja, wazo kwanza. Chambua wazo vizuri,fanya upembuzi na ikibidi lipia gharama ili kupata mtiririko sahihi wa jambo lako. Weka action plan inayotekelezeka,kisha ingia mzigoni.
 
Mjasiliamali anauza wazo kwa jamii akitumia umiliki wa rasilimali kama nyezo za kufikia malengo. Pesa(mtaji) ni moja ya rasilimali. Kwakua soko letu si pana na la kutabirika vema. Aina ya ujasiliamali wa kutumia rasilimali chache ni mgumu m.f. Kuwekeza mtaji kwa mtu mwenye mawazo (m.f NICO). Hapo ndo tunazalisha wajasiliamali wanaoomba mawazo ya biashara. Yote-ya-yote kunakili pia ni BIASHARA.
 
Back
Top Bottom