Ushauri na muongozo wa kiusalama kwa raia, hususan Pemba

Ushauri na muongozo wa kiusalama kwa raia, hususan Pemba

MrFroasty

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2009
Posts
1,195
Reaction score
595
Asalam aleykum,

Nilishawahi kutoa ushauri huu awali na wala sio wazo jipya nchini, nishauri wananchi wajipange na kuunda vikosi vya kujilinda kwenye vitongoji au vijiji vyao. Hili wazo ni sawa na lile la Sungusungu miaka ya zamani. Si jipya na wala halihitaji leseni ya serekali.

Nashauri wananchi wakaunda vikundi/vikosi vya kulinda maeneo yao wanayoishi na kueka muda wa wageni kuingia maeneo hayo kuwa mwisho maghrib. Zaidi ya hapo lazima mtu awe ametoa taarifa kwa Sheha na kuiwasilisha kwa viongozi wa vikosi hivi.

Wazo hili ni vyema likafanyiwa kazi haraka, nakumbuka miaka ya zamani ilifika hadi watu wa Pemba wakawa wanakimbia makaazi yao. Nadhani msimu huu hautakuwa na tofauti.

Sababu kuu ni hizi zifuatazo:
  1. Jeshi la polisi na vikosi vya SMZ ndio watuhumiwa wakubwa wa uhalifu na uonezi katika vitongoji na vijiji. Kuna hadi video youtube, askari akimuibia raia. Jeshi limejivunjia heshima na hadhi ya kulinda raia na mali bila ya ubaguzi.
  2. Wananchi wameshaanza kuwa na khofu juu ya vitendo vya kuvamiwa usiku watuhumiwa wakiwa vyombo vya usalama.
Nimalize kufupisha, ikishindikana hivi basi japo wananchi mkigongewa milango pigianeni simu. Wingi wenu na umoja wenu pamoja na imani zenu dhidi ya Allah ndio kinga yenu kubwa. Nimeona youtube waliopigwa wote walikuwa wakijihami peke yao as invidividual?

Umoja wenu uko wapi ? Mtu arushe tuu txt kwenye watssup-group ya ulinzi wa kiraai nao wafike kumuokoa mwenzao. Vyengivyo familia na watoto wetu watateseka sana kama hakutakuwa na umoja.

Wasalaam
 
ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE.
 
Back
Top Bottom