Ushauri na unabii wangu kwa mitume na manabii wa leo kuhusu uchumba na ndoa kwa vijana wa leo

Ushauri na unabii wangu kwa mitume na manabii wa leo kuhusu uchumba na ndoa kwa vijana wa leo

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Kuliko mabinti, wasichana na wananawake pekee kujaza makanisa na masinagogi wakitafuta wenza na wachumba kwa maombi na maombezi kwenye nyumba za ibada,

Uko umuhimu wa kufanya kongamano la kitaifa na mikesha maalumu kwa vijana wa miaka 18-40, wa kike na kiume, ambao bado hawajaoa wala kuolewa, ili kuwapa mwangaza na maono ya kinabii ya namna ya kukutana na wachumba zao, pamoja na watu ambao Mungu amekusudia kuwaunganisha nao ili hatimae waishi kama familia takatifu kwa ndoa.

Kwanza wawakutanishe vijana wa kiume peke yao na kuwafunda namna ya kiMungu na ya baraka jinsi ya kumtambua na kupata mwenza wa kuishi nae katika maisha ya ndoa yenye upendo, furaha na amani. Halafu tena wakutane na vijana wa kike nao vilevile wafundwe vyema namna ya kutambua mume mwema na jinsi ya kuishi kwa furaha katika ndoa yao na watoto wao Mungu akiwafanikisha.

Halafu sasa, baadae lifanyike,
kongamano na mkesha maalumu wa pamoja, kwa vijana wote wa kike na kiume, na tahmini ya mafanikio na matokeo ya makongamano na mikesha hiyo ifanyike mwisho wa mwaka, kwa ndoa maalumu takatifu za makundi ya pamoja kwa ambao Mungu atakua amewaunganisha kupitia mikesha na makongamano hayo maalumu ya kiroho.

Napendekeza maombi na maombezi ya kinabii namna hii yawe yanafanyika kila mwanzo wa mwaka, na kisha tathmini ya matokeo yake vifanyike katikati na mwisho wa mwaka kwa ndoa takatifu za makundi ya pamoja kufanyika.

Hii hali ya kujaza wanawake na wasichana pekee makanisani itakua na maana tu, endapo patakuwepo na kampeni maalumu ya kiroho na kinabii, kuhakikisha na vijana wa kiume pia wanajaza makanisa. Kwa kufanya hivi, manabii na mitume watakua wamesaidia sana hii kasumba ya kutangatanga miongoni mwa vijana wasio oa wala kuolewa kwenye makanisa mabalimbali ya kiroho.

Neema, Baraka na Upendo wa Yesu Kristo wa Nazareth viwe nanyi nyote, sasa, daima na milele, Aimen. :JustClap:
 
Dada zetu walokole wanatamaa, wanasema Mungu huwezi muomba samaki akakupa nyoka au mkate akakupa jiwe hivyo hawataki wanaume wenye mapungufu kama ufukara, ulevi, kazi duni au ujobless sasa wote wanagombania 1% ya wanaume waliotoboa ambao kimsingi hao wanaume hawataki mabinti wa namna hiyo hivyo inakuwa mtafutano, sipingi hilo andiko wanalosimamia la mkate na jiwe ila uhalisia wa maisha mabinti wengi wanaolewa na machinga, vinyozi, boda, vibarua, wauza uduvi na kazi nyingine duni pia kwa sababu ya umaskini na kukosa exposure vijana wetu wana tabia mbovu kama kuvuta fegi, pombe, kubeti nk na hivuo kuonekana hawafai hawana future. Sasa church girls wanaishia kutoka na waume za watu na mwisho kuwa single maza na kuishia depression. Wachungaji nao wana mistari yao ya kuwafariji Kuwa Mungu hawahi wala hachelewi wakati sahihi Bwana atawapa waume hata kama wana miaka 65 hivyo kwa ahadi hizo wanaendelea kutulia kwenye comfort zone mwisho wengine mpaka menopause imewakuta bila mme wala mtoto ila wanaliwa kwa siri magetoni na magestini kimya kimya kulinda ushuhuda. Suluhisho ni kuwaeleza uhalisia wa maisha waachane na matarajio makubwa ambayo hayatimiagi
 
Dada zetu walokole wanatamaa, wanasema Mungu huwezi muomba samaki akakupa nyoka au mkate akakupa jiwe hivyo hawataki wanaume wenye mapungufu kama ufukara, ulevi, kazi duni au ujobless sasa wote wanagombania 1% ya wanaume waliotoboa ambao kimsingi hao wanaume hawataki mabinti wa namna hiyo hivyo inakuwa mtafutano, sipingi hilo andiko wanalosimamia la mkate na jiwe ila uhalisia wa maisha mabinti wengi wanaolewa na machinga, vinyozi, boda, vibarua, wauza uduvi na kazi nyingine duni pia kwa sababu ya umaskini na kukosa exposure vijana wetu wana tabia mbovu kama kuvuta fegi, pombe, kubeti nk na hivuo kuonekana hawafai hawana future. Sasa church girls wanaishia kutoka na waume za watu na mwisho kuwa single maza na kuishia depression. Wachungaji nao wana mistari yao ya kuwafariji Kuwa Mungu hawahi wala hachelewi wakati sahihi Bwana atawapa waume hata kama wana miaka 65 hivyo kwa ahadi hizo wanaendelea kutulia kwenye comfort zone mwisho wengine mpaka menopause imewakuta bila mme wala mtoto ila wanaliwa kwa siri magetoni na magestini kimya kimya kulinda ushuhuda. Suluhisho ni kuwaeleza uhalisia wa maisha waachane na matarajio makubwa ambayo hayatimiagi
Ndugu yangu umeongea pointi kubwa mno, natamani hii ndio ingekuwa uzi husika au iwafikie wengi .
 
Waoaji wapo. Ukiona mwanamke anasema hakuna waoaji ujue huyo anataka mwanaume ambae sio wa level yake.

Ni rahisi kumpata mwanaume mwenye gari kama na mwanamke uyo pia ana gari kwa sababu watakutana tu kwenye muingiliano wa maisha inaweza kuwa parking, garage, duka la spear parties n.k

Ni rahisi mwanamke kumpata mwanaume ambae ni boss kama na mwanamke uyo ni boss pia kwa sababu watakutana tu inaweza kuwa kwenye vikao vya ofisi, kwenye ndege n.k

Lakini unakuta mwanamke hajui hata kubadilisha wallpaper ya kompyuta halafu anataka mwanaume ambae ni software engineer, hapo lazima kuwe na ugumu.
 
ni muhimu sana wasaka wachumba na wenza wa ndoa kukutanaishwa pamoja,
hii ya jinsia moja kujaza nyumba ya ibada, ni kujaribu kupeana moyo tu, bila kua na suluhisho la hakika la sababu ya kusanyiko hilo :NoGodNo:
Wanaume huenda bar, vibanda vya kutazama soka na vijiwe vya kubeti nk. Wadada ukitoa saloon hawana mikusanyiko mingi ya kijamii na kumbuka binadamu yeyote ni social being hivyo wanakutanika katika majumba ya ibada, mabinti huvaa vizuri na kufanya hiyo kama mtoko wa yeye pia kukutana na wanajamii na hicho ndo chanzo cha jamii moja kujazana majumba ya ibada
 
Wanaume huenda bar, vibanda vya kutazama soka na vijiwe vya kubeti nk. Wadada ukitoa saloon hawana mikusanyiko mingi ya kijamii na kumbuka binadamu yeyote ni social being hivyo wanakutanika katika majumba ya ibada, mabinti huvaa vizuri na kufanya hiyo kama mtoko wa yeye pia kukutana na wanajamii na hicho ndo chanzo cha jamii moja kujazana majumba ya ibada
Iyo kweli mkuu hata ukifatilia trend ya wanaofunga ndoa utaona wanawake wanaotembelea tembelea bar wana ndasi kubwa zaidi kuliko hawa church girls kwa sababu uko bar ndipo anakutana na wanaume wengi mabachelor.

Vijana ambao wapo kwenye age ya kuoa ni wachache sana wana mahudhurio mazuri uko kwenye nyumba za ibada. Wanaume utakaowakuta kanisani ni wazee na wababa tu
 
Mwanzoni, katikati na mwisho wa mwaka halafu sadaka utatoa wewe mkuu?

Kwa umuhimu kabisa tambua kuwa kipaumbele namba moja kwa wachungaji ni sadaka, vinafuatia vingine kama umaarufu nk, kisha hizo ndoa za hao mabinti waumini wao ni kati ya vipaumbele vya mwisho mwisho huko.

Mibinti yenyewe haijitambui hata hao wachungaji wanajipigia tu na waganga pia hawako nyuma wanapitia, si bora kuichuma sadaka tu angalau visikosekane vyote.

Hizo ibada ziongezwe, ikiwezekana iwe kushinda na kukesha kila siku. Vijana tupo busy kuimarisha chama chetu cha KATAA NDOA ambacho kwanza bado kipya
 
Back
Top Bottom