Ushauri: Nimeagiza Valeur ndogo nimeletewa Viceroy na nina buku 5 cash. Mhudumu ni pisi kali niliyokuja kuilia misele niombe namba

Ushauri: Nimeagiza Valeur ndogo nimeletewa Viceroy na nina buku 5 cash. Mhudumu ni pisi kali niliyokuja kuilia misele niombe namba

Marashi

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2018
Posts
2,877
Reaction score
4,522
Natokaje hapa, ndo ushauri ninaohitaji.

Hapa jirani kuna pub mpya imefunguliwa mwezi sasa, kuna pisi za hatari …. kuna hii moja juzi nilikuja ikanichekeachekea leo nilikuja mahsusu kwa ajili ya kuomba namba nikasema nizuge na Valeur ndogo nina buku tano tu. Sa kaleta Viceroy ndogo na nimechungulia menu hapa bei yake ni 10,000.

Sikujua, kanifungulia na nimeshapiga puff zangu kadhaa hapa ndo nashtuka. Serious, nahtaji ushauri wanangu. Sina issue na namba kabisa nishachanganyikiwa, nataka namna ya kutoka tu. Sina kitu kabisa
 
Pole weka simu Bondi mkuu
Jembe simu hapana. Michakato yangu yote ipo humu. Hapa natafta akili ya kuwatoka. Sina hela bila sim labda kesho nishinde ndani, ntakula wapi?
 

Attachments

  • image.jpg
    image.jpg
    361.5 KB · Views: 6
Kwamba unashindwa kupiga simu kwa mshkaji wako at mmoja akuokoe hapo
Nina majanga, mwez wa pili nimesimamishwa. Wanangu nishawakopa sana. Japo kesho nategemea kulipwa na mwajiri baadhi ya visenti ila sina uhakika. Kiukweli sion mtu wa kumkopa chap, ingekua mchana ningefanya kitu. … usiku huu naanzia wapi
 
Natokaje hapa, ndo ushauri ninaohitaji.
Hapa jirani kuna pub mpya imefunguliwa mwezi sasa, kuna pisi za hatari …. kuna hii moja juzi nilikuja ikanichekeachekea leo nilikuja mahsusu kwa ajili ya kuomba namba nikasema nizuge na Valeur ndogo nina buku tano tu. Sa kaleta Viceroy ndogo na nimechungulia menu hapa bei yake ni 10,000.

Sikujua, kanifungulia na nimeshapiga puff zangu kadhaa hapa ndo nashtuka. Serious, nahtaji ushauri wanangu. Sina issue na namba kabisa nishachanganyikiwa, nataka namna ya kutoka tu. Sina kitu kabisa
Toa namba nije na askari waliovaa sare tukubebe
 
Anzisha vurugu wamekupa kinywaji kimechakachuliwa, komaa hadi wakulipe fidia ya kukunywesha kinywaji feki fanya vurugu aidha watakuachia au mtapelekana polisi unaweza ukalala mahabusu jumatatu unatoka fresh tu bila kulipa chochote
Aaah we jamaa na joto la dar nikae mahabusu mzee daaah. Hakuna sehemu hua napawaza kama mahabusu japo wao mandata wakikusweka wanasema wamekuhifadhi mahali salama😂
 
Anahitaji namba ya huyo mhudumu wake, sasa akionekana anaandikisha simu kuwa bondi ya hiyo chang'aa si ndo atamkosa manzi mazima?

Apige simu kwa rafiki, ndugu au jamaa aokoe jahazi kwa muamala

Anahitaji namba ya huyo mhudumu wake, sasa akionekana anaandikisha simu kuwa bondi ya hiyo chang'aa si ndo atamkosa manzi mazima?

Apige simu kwa rafiki, ndugu au jamaa aokoe jahazi kwa muamala
Kiukweli kwa sasa nimesimama kazi nimeshakopa sana sioni mtu wa kumkopa. tena hela ya harakaharaka. Nakula kwa vibarua saidia fundi
 
Back
Top Bottom