Ushauri: Nimechoka kusotea ajira,nimedhamiria kilimo

Ushauri: Nimechoka kusotea ajira,nimedhamiria kilimo

Farmer82

Senior Member
Joined
Sep 15, 2013
Posts
183
Reaction score
39
Wadau habari!nimekuja kwenu kuomba ushauri,baada ya kuzunguka sana na vyeti vyangu kusaka ajira bila mafanikio,nimeamua kwa dhati kabisa kuwekeza kwenye kilimo,nimekuja hapa kuwaomba ushauri kwa wale wenye uzoefu,je ni kilimo gani kinafaa kufanyika kuati ya mwezi wa tatu katikati na mwezi wa nne?najua mahindi nitakua nimechelewa ila je ni kilimo cha mazao gani hata kama ya umuagiliaji (maana nimenunua machine ndogo ya kuvuta maji,na shamba halipo mbali na mto) yatafaa na yatatakiwa sokoni iwapo yatalimwa mwezi huo?nina shamba la heka mbili,nimenunua mkoani Morogoro,wilayani Kilosa!Mtaji wangu mpaka sasa ni shilingi laki nne (400,000/=) natanguliza shukrani kwenu wadau
 
Mkuu umeon mbali sana,na wazo lako ni zuri kupita kiasi,ila kwa vijana wa Kitanzania tulivyo na mitazamo hasi na kukosa dira juu ya kilimo sidhani kama watu watatokeza kukupa ushauri juu ya ilo!ushauri wangu mimi ni kua wewe endelea na ndoto zako na ukiwa na dhamira ya dhati na nia hasa kilimo wikl take you far!na maeneo ya karibu na mto ni vizuri zaidi ukafanya kilimo cha mboga mboga,na kipindi cha kiangazi kikali ukalima nyanya na mahindi ya kumuagilia!wenzetu Wakenya tayari kuna maeneo wamejipenyeza na wameanza kilimo in a small scale,kilichonifurahisha zaidi mpaka kina dada nao wamo,nina amini hawa watu watafanikiwa,kwa kua wako focused and determined!pia nakushauri wasiliana na wakuu Malila na Kubota,hawa wanaweza kukupa mawazo positive sana mkuu!kila la kheri
 
Ukiweza kulima kitunguu itakuwa poa zaid maana soko lake ni zuri, Kila la heri mkuu wahenga walisema "KAMA MNATAKA MALI MTAYAPATA SHAMBANI"
 
Ukiweza kulima kitunguu itakuwa poa zaid maana soko lake ni zuri, Kila la heri mkuu wahenga walisema "KAMA MNATAKA MALI MTAYAPATA SHAMBANI"

Ni wazo zuri ulilompa mkuu,na kwa Morogoro wilaya ya Kilosa kitunguu kinakubali,hofu yangu ni mtaji wake huo utatosha kweli?maana nasikia kitunguu kina changamoto sana
 
Back
Top Bottom