Ushauri: Nimeokota wallet yenye Tsh. 50,000 pamoja na risiti za miamala ya pesa nyingi nahofia kurudisha nahisi naweza bambikiwa kesi

Ushauri: Nimeokota wallet yenye Tsh. 50,000 pamoja na risiti za miamala ya pesa nyingi nahofia kurudisha nahisi naweza bambikiwa kesi

Kifulu

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2021
Posts
557
Reaction score
2,064
Nimeokota wallet ina pesa kiasi cha elf 50,000 ila ina risiti ya miamala ya Milioni 45 pamoja na Milioni 10m. Tarehe ni siku niliookota, ndani kuna pia kitambulisho cha bima, nk.

Nahofia kurudisha anaweza kunibambikia kesi ya kupoteza pesa zake!

Nahisi anaweza kusema wallet ilikuwa na pesa hizo.

Naombeni ushauri.
 
Nimeokota wallet Ina pesa 50k ila ina receipts ya miamala ya 45m na 10m

Tarehe ni siku niliookota, ndani Kuna id za bima nk

Naofia kurudisha anaweza kunibambikia kesi ya kupoteza pesa zake,!

Nahisi anaweza kusema wallet ilikuwa na pesa hizo

Naombeni ushauri
Wallet inakuwaje na mil 10?umeiokotea wapi ,katika mazingira gani?ni wewe tu umeiona?kama kweli msamalia mwema peleka polisi
 
Usipende kuokota okota kama usipo dakwa basi utarogwa. Nenda polisi itategemea busara za askari.
Hata akiipeleka polisi, hiyo hamsa polisi watatia kwapani kisha mwenyewe ataitwa aje kuchukua maratasi yake.

Muhimu hapo chukua hamsa yako, hiyo wallet mpe bodaboda wale wanaovaa ndala moja inaning'inia(vishandu) mwambie apite kituo cha polisi na ukali kisha aitupie kituoni halafu atembee na ukali.
 
Shida unaweza ukawa mwema kuripoti police ukadakwa wwe kesi ikabakia kwako.
Jamaa yangu juzi kaokota simu ya million moja mwenye simu akampigia kapokea akampa maelekezo alipo mwenye simu alipofika kesho yake kuchukua simu yke hata kusema neno Asante au kumuachia jamaa hata teni kapiga kimya.
 
Nimeokota wallet Ina pesa 50k ila ina receipts ya miamala ya 45m na 10m

Tarehe ni siku niliookota, ndani Kuna id za bima nk

Naofia kurudisha anaweza kunibambikia kesi ya kupoteza pesa zake,!

Nahisi anaweza kusema wallet ilikuwa na pesa hizo

Naombeni ushauri
Tenda wema. Mtafute mwenye navyo. Kama kuna business card mtafutie hiyohiyo.
 
Hata akiipeleka polisi, hiyo hamsa polisi watatia kwapani kisha mwenyewe ataitwa aje kuchukua risiti zake.

Muhimu hapo chukua hamsa yako, hiyo wallet mpe bodaboda wale wanaovaa ndala moja inaning'inia(vishandu) mwambie apite kituo cha polisi na ukali kisha aitupie kituoni halafu atembee na ukali.
daaah! asante😅
 
Back
Top Bottom