Ushauri: Nina mil 150 niwekeze katika nini?

Hi wapendwa kwa rehma zake mwenyezi Mungu, nimepata haka kamzigo naomba ushauri ili kesho yangu iwe na kheri niwekeze katk biashara gani na mtaji huu

asanteni kwa maoni
Export business ndio Habari ya mujini. Nina export mazao ya biashara nchini za nje . nahitaji partner . tuwasiane 0655308308.
 
Nunua vipande katika mfuko wa umoja kama Wekeza au Jikimu uwe unapata gawio kila baada ya miezi 3 huku mtaji wako ukizidi kuongezeka
wako wenye testimony za kufanikiwa kupitia hii biashara ya vipande?
 
Hizo M 150 ulizipata wapi? Wekeza ulikozipata hizo...
 
inafanyikaje hii ndugu, au ndio hadi tuonane face to face?
 
Hi wapendwa kwa rehma zake mwenyezi Mungu, nimepata haka kamzigo naomba ushauri ili kesho yangu iwe na kheri niwekeze katk biashara gani na mtaji huu

asanteni kwa maoni
Usifanye biashara za kuumiza kichwa na kulaumiana na watu,tafuta uwanja mkubwa na ujenge apartiment tu basi...utatumia hiyo pesa wewe mpaka wajukuu zako
 
Fanya ulichokifanya mpaka kupata hzo pesa au njoo huku Mbeya tufanye uchenjuaji wa madini
 
Mkuu, hongera sana. Nenda pale TATA, kawaone wakuuzie mabasi mawili... Unalipa advance kama mia arobaini na nyingine utamalizia. Ukinunua zile basi zinaweza kukaa miaka mitano zikapiga kazi fresh tu. Ila kabla hujazitia barabarani, hakikisha unazikatia BIMA kubwa...
Kwa siku gari inaleta laki mbili, so kwa mwezi unahesabu milioni sita kwa basi moja na kwa mwaka ni milioni 72 (Toa gharama nyingine unabaki na kama 50M) kwa mwaka. Kwa miaka mitano unagenerate kama M 250 kwa basi moja.
 
Nawashukuru wakuu nimepata mwanga sana na naiona njia
 
moja linauzwa tsh ngapi?
 
Hivi kuna mtu mwenye hizo hela afu hajui afanye nini?
Au mmeuza nyumba ya urithi?
Unajivika umajinuni kwa nn? Chanzo kimoja wapo ni hicho mtu kauza mali yake ya halali ya urithi, mtu kapata fidia nzuri mahali, mtu kacheza m-bet kapata mzigo, kwann asiulize wachumi cha kufanya?
 
Hi wapendwa kwa rehma zake mwenyezi Mungu, nimepata haka kamzigo naomba ushauri ili kesho yangu iwe na kheri niwekeze katk biashara gani na mtaji huu

asanteni kwa maoni
Umeokota au umerithi? Ingekua umetafuta kwa jasho usingeshindwa kujua uzifanyie nini
 
Nenda Iringa au Morogoro, nunua Shamba ekari kama mia moja hivi, panda miti ya mbao. Baada ya miaka 10 utakuwa Bakherssa mdogo.
Hii itakugharimu si zaidi ya million 70 kuanza kununua Shamba, kununua miche, upandaji , utunzaji mpaka kuvuna.

Fedha inayobaki tafuta biashara Nyingine itakayokulinda ili usiuze Shamba lako mapema
 
WEKEZA KATIKA VIWANJA NA NYUMBA.HAPO UNQ NYUMBA KAMA SITA HIVI ZA KITANZANIA ZILIZO BORA.HUU NDO UTAJIRI USIO NA HASARA
Biashara hii inahitaji uwe umeshapumzika kutafuta pesa.
 
Samahani mkuu, kwa mfano ukiweka mil 5 kwenye hiyo fixed deposit kwa mwezi unapata return bei gani?
Juzi nimepita Access bank FDR account ya 5M unapata return ya 11.2% kwa 30days na 11.5% kwa 60days 11.8% for 90days kwa miezi sita na kumi na mbili sikumbuki vizuri unaweza kuwafuatilia kama uko serious naweza kupa namba zao ukawatafuta
 
Me nakushauri wekeza katika fixed deposit utapata 21,000,000 kama retun ambapo ukiongea nao vizuri utapata 1,750,000 kila mwezi hiyo ni retun tuu apo nazungumzia return ya 14% na unaweza pia chukua hiyo 21 milion up front ukitaka for 1 year
Huu ni uoga wa kufanya biashara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…