Ushauri: Ninamtaji wa milioni 3 lakini sijui nifanye biashara gani

Kuku kwiyoyo

Member
Joined
May 7, 2020
Posts
29
Reaction score
17
Habari wanaJamiiForums

Nirudi kwenye Mada husika. Mimi ni mwanachuo kilichopo Dodoma nipo mwaka wa kwanza. Sasa hapa nilipo nilikuwa nina milioni tatu lakini natamani zijizalishe ili nitakapomaliza masomo niwe na mtaji mkubwa lakini sijajua nifanye biashara gani ambayo haitoniaribia ratiba ya masomo

Nimeamua kuja kwenu muweze kunishauri

NAWASILISHA
 
Sijakuelewa unataka kuzitunza ufanye biashara ukimaliza chuo au sasa?
 
Chuo gani hapo Dodoma ili nikushauri vizuri? udom, cbe, mipango, st john au chuo cha madini?
 
Kwa haraka haraka hapo lazima utafute mtu wa kusimamia hiyo biashara.
hapo unaweza fanya biashara kama zifuatazo:
1)Car wash ya magari na bodaboda.
2)Mtafute kijana mwenye ujuzi wa kuziba pancha bodaboda na magari.
3)Mtafute kijana atakae simamia biashara ya kijiwe cha chipsi.
4)Mpesa,Tigo pesa ila utakae mwachia awe makini sana na wezi wa mpesa.
5)Nunua brenda ya juisi na friji kisha mtafute binti afungue kijiwe cha vinywaji baridi.maji,soda,juisi n.k.

Mwisho kabisa kwa biashara ya kufanya wewe mwenyewe huku ukiwa unasoma nunua kwenye maduka ya machimbo bidhaa zifuatazo na uuze kwa cash na mkopo ambao mteja anatanguliza kwanza 50% ya bei yako unayouza.
1)Boksa za kiume na chupi za kike,
2)Ndala za kimasai za kiume na za kike.ila za kike ziwe nyingi kuliko za kiume.
3)body spray na pafume pamoja na kuchukua oda za wateja kwa bidhaa watakazo hitaji.
4)Makava ya simu ya kisasa pamoja na hear phones za kijanja memory card,flash n,k.

Kumbuka hii biashara unaweza fanya kwa part time unaweka kwenye begi bidhaa zako unaingia ofisi kwa ofisi mlango kwa mlango.pia unaweza kujitangaza kwenye mitandao na ukauza kiroho safi.wateja wako wa kwanza ni wanafunzi wenzio ambao naamini kabisa ndo watakao kuinua kimtaji kwa kukuunga mkono.
Mungu akubariki mkuu.
 
Andaa proposal za ku-invite brand mbalimbali chuoni kuja kujitangaza, kwa kufanya events kama mechi, bonanza waweke mzigo mezani | watumie ma superstar wa chuo.

Nenda Nyerere square pita njia ya kuelekeza Sido upande wa kushoto kuna Juice point inaitwa TAMU unhea nae uweke mashine za Kuosha gari hapo Boom.

Nunua mashine za rambaramba tengeneza vijana wapeleke shule za msingi saa 2-8, the Town (Nyerere square, stands nk) saa 8-jioni.

Fungua Juice point iliyo na uwezo wa ku-move (movable), simple kasogeze nyererw square upige delivery kisawasawa kwa raia zinazo kula upepo mule.

Kula bata nyamachoma msalato.
 
Nakushukuru ndg yangu kwa ushaur wako mungu akubarik pia
 
Ongea na wale mama Ntilie vizur wwnaozunguka chuo from Camp D, Kikuyu stendi na Kule Maeneo ya Kigambon wauzie mchele kwa bei nzuri!!
 
Japo ni la kishenzi.
Unaweza ukapanga chumba ukakipamba kiana, ukawa unakodisha wahuni kupigana miti, u
Ila tu mwenye nyumba anatakiwa awe mbali na eneo lake.

Changamoto ni uwe na geto nyingine uwe na mashine ya kufulia mashuka.

2m inatosha, ila lazima uwe muhuni kidogo kufahimiana na wahuni
 
Mkuu kama hutojali nunua piki piki 2500,000 kama huna kipindi unakuwa unapiga boda boda wakati mwingine unaachia day waka. Itakulipa mno mkuu
 
Kwahiyo unasoma vyuo viwili kwa mpigo?

Sent from my TECNO CX Air using JamiiForums mobile app
 
Bhaghosha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…