public servant
Member
- Jun 22, 2013
- 21
- 6
Nawasalimu wadau wote wajukwaa hili ambalo limekuwa msaada kwa watu wengi ikiwemo mimi na niwapongeze kwa kazi nzuri mnayoifanya, Hivi karibuni kumejitokeza wimbi kubwa la dada zetu kuvutiwa na rangi nyeupe hata kufikia hatua ya kutumia madawa ya Kikongo na Kichina kwa lengo la kutaka kuwa weupe, katika pitapita zangu nimekutana na dada mmoja ambaye ni muathirika wa tatizo hili na anaomba msaada wa namna bora yakuweza kuachana na matumizi ya dawa hizi kwani ameshindwa kuacha kwa sababu tu eti akiacha ngozi yake inaharibika na anakuwa kama BIBI wa miaka 60 hivyo imemlazimu kuendele kutumia dawa hizo ili asiathirike, kwa mnaoelewa msaada tafadhali