Ushauri: Serikali ianzishe hardship allowances kwa Walimu wanaofundisha Vijijini

Ushauri: Serikali ianzishe hardship allowances kwa Walimu wanaofundisha Vijijini

Man from cuba

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2021
Posts
571
Reaction score
1,394
Waziri mpya wa TAMISEMI na Waziri mpya wa Elimu wanatakiwa kulichukulia kwa uzito suala la walimu wanaofundisha vijijini kwa kuwapa motisha mbalimbali ili maombi ya uhamisho wa walimu ipungue.

Imekuwa mtihani mkubwa kwa watumishi hawa wa elimu kukaa vijijini ambako huduma hazipatikani,changamoto ya usafiri,ushirikina etc.

Walimu wengi wamekuwa wakipambana kwa njia yoyote kuhama hadi waziri wa TAMISEMI aliyekuwepo kusitisha uhamisho lakini tukija kwenye uhalisia hakuna mtumishi anayependa kubaki kwenye mazingira mabaya kama hayo.

Nimemsikia mbunge wa Makete akilalamika ukosefu wa Waalimu wa kike jimboni kwake kitu kinachowapa ugumu wanafunzi wa kike hasa wanapovunja ungo, lakini ukiliangalia kwa undani suala hilo sio kweli kwamba serikali haipeleki walimu huko lakini wote wanahama hasa walimu wanawake hivyo serikali ingeanzisha posho na hardship allowances kwa walimu wanaofundisha vijijini ili angalau kuwatofautisha na wa mijini.

Serikali ikifanya hivyo pamoja na upungufu mkubwa wa walimu ukilinganisha na idadi ya wanafunzi angalau itakuwa imetibu changamoto ya upungufu wa walimu wa kike vijijini tofauti na hapo yatakuwa kama ya kata moja kigoma ambayo ina mwalimu mmoja tu wa kike kata nzima.
 
Hata mjini, juzi nilienda kumsalimia rafkiangu katika shule moja kigamboni kwakweli niliona jinsi walimu wanavyo fanya kazi katika mazingira magumu.

Duuh shule inawatoto wengi utazani mchanga, kelele kama sokoni tabu sana kwa walimu.
Wapewe tu hiyo kitu.
 
Tangu UHURU ualimu ndio kada inayotoa viongozi wa kada zote kuanzia Rais, Waziri mkuu,mawaziri, wabunge lakini kama ilivyo asili ya mswahili akishiba hakumbuki nyuma, wakipata madarakani ya ngazi za uamuzi huwa awawakumbuki walimu.
 
N kwel yaa kuna maticha wana life gumu balaaa ni bora anayeendesha boda.

But shida n nn?? Walimu wanateswaa na mikopo, wanakopa bilaa kuwa na plan, mwalim akiajiriwaa tuu lazma aoe au aolewe hii ni burden kubwaa watu hawaongei.

Another point walimu 99% wanatoka familia masikin sana so lazma aaze kulipa fadhila kwa kina anko child waliomsaidia ada....
What to do.

Walimu acheni kujiingiza kwenye mikopo isiyo na tija au kwa kufata mkumbo..vile vile achen kuowa mapema wkat hamjajipanga.
Last but not least walimu wenye elimu ndogo kama certificate,UPE, diploma mjiendeleze kielimu mpandishiwe mshahara..
 
Hata mjini, juzi nilienda kumsalimia rafkiangu katika shule moja kigamboni kwakweli niliona jinsi walimu wanavyo fanya kazi katika mazingira magumu.

Duuh shule inawatoto wengi utazani mchanga, kelele kama sokoni tabu sana kwa walimu.
Wapewe tu hiyo kitu.
Kigamboni hapo mjini njooni huku Kyanyamsana shule ya Msingi mjionee wenyewe
 
Walisema Mwalimu anayeajiriwa sasa anapelekwa maeneo ya pembezon, hvyo awe tayar ..tatizo huwa mnafkr ni wanatania
 
Magufuli na mke wake walikuwa walimu, majaliwa na mke wake walikuwa walimu, ndalichako alikuwa Mwalimu, bashiru alikuwa Mwalimu, mwakyembe alikuwa Mwalimu baada ya kupata nafasi walisahau msoto wa ualimu na kuwafungia vipi walimu wenzao.

Hawa ndio ilipaswa wawe watetezi wa walimu sababu wameuishi ualimu nao pi walilalamika maslai duni kabla awajapata madaraka.
 
Nani anajali, walim waliambiwa hata huko vijijin kuna watanzania
 
Kuwa mwalimu Afrika ni wito
Watumishi wote nchi hii maisha yao kulingana na vipato vilivyo hayana tofauti.

Tatizo la walimu sijui ni nani alowaroga, aisee.

Muda wote mi kulalamika kama kenge.

Tatizo kubwa la walimu ni kukopq kopa kipumbavu na kuishi maisha ya kuigana bila sababu za msingi.

Ukitoa kada za Afya, Advocate ( Wakili ) na Engineering. Mwalimu ndiye mfanyakazi mwenye mshahara mkubwa zaidi.

Mwalimu wa Shahada anachukua basic Tsh 716,000 kwa mwezi. Mwalimu wa science anaanza na Tsh 750,000 kwa mwezi.

Kila wanafunzi wakifunga shule na yeye anafunga.

Lakini kada nyingine zote kama Wahasibu, maafisa maendeleo, mipango, mazingira, HR, Weo, afisa Utumishi, Veo, shahada mishahara yao basic ni Tsh 710,000 na huwezi kuwasikia wakilialia kama mbwa koko kama hawa walimu.

Tena hawa likizo zao ni siku 28 tu mara moja kwa mwaka.

Very stupid.

Mtu kukaa kimya haina maana kuwa ana maisha mazuri sana.
 
Watumishi wote nchi hii maisha yao kulingana na vipato vilivyo hayana tofauti.

Tatizo la walimu sijui ni nani alowaroga, aisee...

Hahahaaa kuwa na adabu mkuu, hiyo "VERY STUPID" yako usinge ijua kama sio walimu.
 
Tangu UHURU ualimu ndio kada inayotoa viongozi wa kada zote kuanzia Rais, Waziri mkuu,mawaziri, wabunge lakini kama ilivyo asili ya mswahili akishiba hakumbuki nyuma, wakipata madarakani ya ngazi za uamuzi huwa awawakumbuki walimu.
Watumishi wote nchi hii maisha yao kulingana na vipato vilivyo hayana tofauti.

Tatizo la walimu sijui ni nani alowaroga, aisee...
Sidhan kama utakuwa unawatendea haki watu waliokuwa na mchango mkubwa hadi ukajua kuandika hapa jf
 
N kwel yaa kuna maticha wana life gumu balaaa ni bora anayeendesha boda.

But shida n nn?? Walimu wanateswaa na mikopo, wanakopa bilaa kuwa na plan, mwalim akiajiriwaa tuu lazma aoe au aolewe hii ni burden kubwaa watu hawaongei...
Kwa mshahara wa laki tatu lazima mwalimu akope
 
Watumishi wote nchi hii maisha yao kulingana na vipato vilivyo hayana tofauti.

Tatizo la walimu sijui ni nani alowaroga, aisee.

Muda wote mi kulalamika kama kenge.

Tatizo kubwa la walimu ni kukopq kopa kipumbavu na kuishi maisha ya kuigana bila sababu za msingi.

Ukitoa kada za Afya, Advocate ( Wakili ) na Engineering. Mwalimu ndiye mfanyakazi mwenye mshahara mkubwa zaidi.

Mwalimu wa Shahada anachukua basic Tsh 716,000 kwa mwezi. Mwalimu wa science anaanza na Tsh 750,000 kwa mwezi.

Kila wanafunzi wakifunga shule na yeye anafunga.

Lakini kada nyingine zote kama Wahasibu, maafisa maendeleo, mipango, mazingira, HR, Weo, afisa Utumishi, Veo, shahada mishahara yao basic ni Tsh 710,000 na huwezi kuwasikia wakilialia kama mbwa koko kama hawa walimu.

Tena hawa likizo zao ni siku 28 tu mara moja kwa mwaka.

Very stupid.

Mtu kukaa kimya haina maana kuwa ana maisha mazuri sana.
Mbona povu kiongozi

Walimu wanajisemea mambo yao na wewe kamisaa wangu jisemee mambo yako

Sasa mwandamizi kama huwezi kujisemea mambo yako tulia walimu wanapambania haki zao muheshimiwa
 
Mbona povu kiongozi

Walimu wanajisemea mambo yao na wewe kamisaa wangu jisemee mambo yako

Sasa mwandamizi kama huwezi kujisemea mambo yako tulia walimu wanapambania haki zao muheshimiwa
Huyu huenda Ana hasira kali na walimu huenda alikuwa mtoro akapigwa mboko za kutosha
 
Back
Top Bottom