Ushauri:Serikali itoe chchote kwa atakaejitangaza hadharani kuwa ni mgonjwa wa corona baada ya mtu huyo kupimwa na kuthibitika

Ushauri:Serikali itoe chchote kwa atakaejitangaza hadharani kuwa ni mgonjwa wa corona baada ya mtu huyo kupimwa na kuthibitika

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Nashauri serikali ije na mikakati ya muda mfupi wa kudhibiti ugonjwa huu na mkakati mmojawapo uwe ni kutoa chochote(fedha,cheti maalumu,n.k) kwa yeyote atakaepimwa na kugundulika na corona na kisha akaamua kujitangaza mwenyewe hadharani au akaruhusu atangazawe hadharani na mamlaka husika na picha zake kusambazwa kwenye vyombo vya habari.

Kwa mfano,serikali inaweza kuwapa vyeti maalumu vya kutambua mchango wao katika mapambano dhidi ya corona, na watu hawa wanaweza pia kupewa kipaumbele na serikali katika maswala mbalimbali kama vile utoaji wa ajira kwa walio na sifa,kupewa mialiko katika matukio yoyote yanayohusiana na ugonjwa huu,n.k.

Moja ya faida ya kufanya hivi,ni kuwa,mbali na kupambana na ugonjwa huu,pia itasaidia sana kupunguza kama sio kuondoa kabisa unyanyapa dhidi ya wote watakaothibitika kuugua ugonjwa huu ambao ni ugonjwa tu kama magonjwa mengineyo.

Hata hivyo.hatua hii itakuwa na maana katika kipindi hiki ambacho wagonjwa ni wachache kwani wagonjwa wakiwa wengi sana, inaweza ikapoteza maana.

Hivyo,kwakuwa hatujaamua kuthibiti mikusanyiko kama wenzetu huku wagonjwa wakiwa bado ni wachache,nadhani huu ndio wakati muafaka wa kutumia mbinu kama hizi ingawa kuna wachache wanaweza kuzitumia vibaya fursa za aina hii.

Kuwajua wagonjwa tofauti na kuwasikia(hata kama watakuwa wamewekwa kwenye karantini), kuna impact kubwa sana hasa kwa wanaodharau huu ugonjwa wakiamini wao ni vijana,n.k.

Watu hawa pia wanaweza kutumika kama mabalozi katika mapambano dhidi ya corona ikiwemo kuhamasisha michango pamoja na mambo mengineyo yanayohusiana na ugonjwa huu.

Ni ushauri tu.
 
Naunga mkono hoja, kwa serikali ku encourage watu wapime na kujitangaza ili kuhamasisha upima na watoe incentive ya kujitangazs huko, ila incentive hiyo iwe ni certificate of recognition.

Kwa mujibu wa maadili ya kidakitari, hairuhusiwi kutangaza mambo yoyote ya tiba, ikiwemo hairuhusiwi matangazo ya tiba, madawa au huduma, na hairuhusiwi mtu kupata manufaa yoyote ya Kiuchumi kupitia tiba, damu ni bure, viungo ni bure hairuhusiwi kuuza damu au figo, hivyo watu hawaruhusiwi kupewa pesa ili kuhamasisha kupima na kujitangaza.
P
 
Naunga mkono hoja, kwa serikali ku encourage watu wapime na kujitangaza ili kuhamasisha upima na watoe incentive ya kujitangazs huko, ila incentive hiyo iwe ni certificate of recognition.

Kwa mujibu wa maadili ya kidakitari, hairuhusiwi kutangaza mambo yoyote ya tiba, ikiwemo hairuhusiwi matangazo ya tiba, madawa au huduma, na hairuhusiwi mtu kupata manufaa yoyote ya Kiuchumi kupitia tiba, damu ni bure, viungo ni bure hairuhusiwi kuuza damu au figo, hivyo watu hawaruhusiwi kupewa pesa ili kuhamasisha kupima na kujitangaza.
P
Hilo la pesa sio lazima ila ni iwapo itaonekana inafaa kama taratibu zinaruhusu.
 
Inawezekana wewe ndiyo mjinga, umeshindwa kuelewa lengo la mleta uzi.
Akili ni nywele kila mtu ana zake.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyo kachangia kwa kuangali ID ya mleta mada na sio alichoandika ndio maana nimempuuza.

Siku serikali ikisema inatoa vyeti maalumu vya kuwatambua wagonjwa wa corona waliojitangaza,mtu kama huyu usishangae kumuona ndio kawa wa kwanza kutoa pongezi kwa serikali kupitia hapa JF.
 
Moja ya faida ya kufanya hivi,ni kuwa,mbali na kupambana na ugonjwa huu,pia itasaidia sana kupunguza kama sio kuondoa kabisa unyanyapa dhidi ya wote watakaothibitika kuugua ugonjwa huu ambao ni ugonjwa tu kama magonjwa mengineyo.
Hapa tutasambaza zaidi
 
Maradhi yanayoambukiza si maradhi ya kukurupuka kujitangaza. Ukijigundua jitenge, jitibu, usiambukize wengine.
Unyanyapaa kwenye jamii kwa wagonjwa wenye maradhi ya kuambukiza bado upo mkubwa tu wakigundulika.
We furahia cheti halafu njoo mtaani ndio utaelewa somo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sioni point yoyote katika kumzawadia mtu cheti!!
Wenzetu wanawaza kinga/dawa sisi tunawaza vyeti??
Wenzetu wanawaza usalama wa wauguzi sisi vyeti kweli?
Wenzetu wanawaza karantini isiyoharibu uchumi wa wahusika...
Wanawaza kusafisha mitaa kutoa vifaa vya kujilinda bure wewe unawaza vyeti!!
Tunawaza vifaa tiba na hospitali ziongezwe wewe...
Wazungu wanatuwazia waafrika hatuna hela yakutusaidia tupate wataalamu wakutosha na vifaa wewe unawaza vyeti?
Waza mambo makubwa bloangu...
haraka omba mwenyewe moderators wafute haka kamauzi kabla sijakasirika...
 
Back
Top Bottom