Ushauri Serikali sitisheni machine za kamari kwa manufaa ya umma

Ushauri Serikali sitisheni machine za kamari kwa manufaa ya umma

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
7,823
Reaction score
10,857
Nilienda Bagamoyo Kidomole kuangalia shamba langu. Wakati nasubiri wafanyakazi wangu waje njia panda nikaona gari lina park na wachina wawili wakashuka wakaenda kwenye kibanda na kurudi na mfuko.

Nilishangaa kuona wachina wako huko. Nilivyo uliza watu wa pale wakasema ni wamiliki wa machine za kamari na pesa nyingi za bodaboda zinaishia huko. Cha ajabu ni kwamba wachina wanapita kukusanya pesa sio kuweka pesa!.

Hii ni biashara ambayo haina faida yoyote na hiyo kodi wanayopata serikali ni ndogo ukilinganisha na pesa zinazotoka kwenye hizi jamii masikini.

Mfanyakazi wangu alienda kuweka reheni pikipiki yangu ya laki tisa kwa laki moja na nusu ili wampe pesa za kamari.

Ushauri wangu ni kwa serikali kusitisha kamari zote ambazo hazihusu wageni. Yaani kamari zibaki kwenye hotel za wageni wa nje maana hizo pesa zinakuja nchini lakini kamari kwenye vijiji na mijini zisitishwe mapema.

Kamari hazisaidii llolote kwa watu wala serikali. kamari haziongezi pato la taifa, haziongezi ujuzi, hazileti kazi wala uwekezaji. Serikali fanyeni hili mapema sana


 
Hizo kamari za Wachina zimewatia umaskini mkubwa vijana wa vijijini. Wengine mpaka wamegeuka vibaka ili wapate pesa za kwenda kucheza kamari.

Fikiria kijana amelima mahindi yake na kuyahudumia, na mavuno ni mara mpja kwa mwaka, hela anaenda kuchezea kamari akifikiria atapata zaidi, halafu hela inapotea yote, na familia inaishi kwa mateso kwa mwaka mzima.

Kwa nia ya kuwasaidia watu wa vijijini, hakika naunga mkono kufutwa kwa michezo ya kamari inayoendeshwa huko vijijini. Nilienda huko Iringa vijijini, baadhi ya vijana baada ya kucheza na kupoteza pesa zao zote, huku wakishuhudia hakuna aliyebahatisha hata mmoja miongoni mwao, walichukia, wakaenda wakazivunjavunja mashine hizo za Wachina, na Wachina hawakuonekana tena kijijini hapo. Hiyo kwa namna fulani ikawa imewaokoa na kuendelea kuibiwa.
 
Tunahitaji watu wenye uwezo wa fikra za kudhibiti wageni na kuwatumia kwa faida ya wananchi na siyo kinyume chake.

Hata hivyo, kwa sababu zile zile zilizoingiza jamii za kiafrika utumwani, serikali zetu huwakaribisha wageni wakiwaita wawekezaji.

Tofauti ni maendeleo ya wakati huu kidunia, lakini umangungo wa fikra uko pale pale kwa baadhi ya watendaji wa serikali.

Ukifanyika utafiti rasmi kwa kuangalia mienendo ya wageni/wawekezaji dhidi ya watumishi/viongozi wa serikali utathibitisha hilo kwa kiwango cha kutosha kuhitaji hatua kuchukuliwa.
 
Nilienda Bagamoyo Kidomole kuangalia shamba langu. Wakati nasubiri wafanyakazi wangu waje njia panda nikaona gari lina park na wachina wawili wakashuka wakaenda kwenye kibanda na kurudi na mfuko. Nilishangaa kuona wachina wako huko. Nilivyo uliza watu wa pale wakasema ni wamiliki wa machine za kamari na pesa nyingi za bodaboda zinaishia huko. Cha ajabu ni kwamba wachina wanapita kukusanya pesa sio kuweka pesa!.
Hii ni biashara ambayo haina faida yoyote na hiyo kodi wanayopata serikali ni ndogo ukilinganisha na pesa zinazotoka kwenye hizi jamii masikini. Mfanyakazi wangu alienda kuweka reheni pikipiki yangu ya laki tisa kwa laki moja na nusu ili wampe pesa za kamari.
Ushauri wangu ni kwa serikali kusitisha kamari zote ambazo hazihusu wageni. Yaani kamari zibaki kwenye hotel za wageni wa nje maana hizo pesa zinakuja nchini lakini kamari kwenye vijiji na mijini zisitishwe mapema.
Kamari hazisaidii llolote kwa watu wala serikali. kamari haziongezi pato la taifa, haziongezi ujuzi, hazileti kazi wala uwekezaji. Serikali fanyeni hili mapema sana



Acha wajinga waliwe tu
 
Kamari zilipaswa kuachwa kwenye mahoteli makubwa na casinos basi.
 
Nilienda Bagamoyo Kidomole kuangalia shamba langu. Wakati nasubiri wafanyakazi wangu waje njia panda nikaona gari lina park na wachina wawili wakashuka wakaenda kwenye kibanda na kurudi na mfuko. Nilishangaa kuona wachina wako huko. Nilivyo uliza watu wa pale wakasema ni wamiliki wa machine za kamari na pesa nyingi za bodaboda zinaishia huko. Cha ajabu ni kwamba wachina wanapita kukusanya pesa sio kuweka pesa!.
Hii ni biashara ambayo haina faida yoyote na hiyo kodi wanayopata serikali ni ndogo ukilinganisha na pesa zinazotoka kwenye hizi jamii masikini. Mfanyakazi wangu alienda kuweka reheni pikipiki yangu ya laki tisa kwa laki moja na nusu ili wampe pesa za kamari.
Ushauri wangu ni kwa serikali kusitisha kamari zote ambazo hazihusu wageni. Yaani kamari zibaki kwenye hotel za wageni wa nje maana hizo pesa zinakuja nchini lakini kamari kwenye vijiji na mijini zisitishwe mapema.
Kamari hazisaidii llolote kwa watu wala serikali. kamari haziongezi pato la taifa, haziongezi ujuzi, hazileti kazi wala uwekezaji. Serikali fanyeni hili mapema sana


[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
 
Nilienda Mlangali nikaona vijana anadownlodiwa pesa na mchina kibaya zaidi wengine wameshakuwa na uraibu nalo. Mchana anafanya kazi ngumu za kupakia na kusomba mbao, jioni anampelekea mchina.
 
jamani kodi muhimu haya ndio maisha yalivyo. kufa kufaana.
 
Hizi mashine nimezikuta wilaya ya mfindi ktk jijini vya usokame, mapanda na shogo nikaona huruma sana vijana wengi wa vijijini wameharibika kazi awafanyi ni kucheza kamari tu.
 
Nani anakula rushwa ya wachina kwasababu hai make sense. Nasikia hata kodi wanataka kuwasamehe!
 
Back
Top Bottom