Ushauri tafadhali....Siku za kujifungua zimepitiliza sana!

everlenk

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
11,628
Reaction score
15,027
Habari wana JF,Nina dada yangu ambaye ni mjamzito na mimba yake ina miezi 11,lakini cha ajabu yuko fiti kabisa na hana dalili zozote za kusikia uchungu, tumeenda hospitalini Madaktari wakaona afanyiwe upasuaji tu lakini imeshindikana kwani kila akitakiwa kufanyiwa presha inapanda sana na kupewa maji ya uchungu imeshindikana hayakufanya kazi ,Sasa ameambiwa arudi tu nyumbani mpaka pale atakapojisikia kuumwa,Hii ni mimba ya pili ingawaje hata ile ya mtoto wa kwanza ilipitiliza hivihivi ikabidi afanyiwe upasuaji na ilikuwa salama kabisa hakuwa anapandwa na presha kama sasahivi.Naombeni ushauri jamani hili ni tatizo gani na husababishwa na nini? Na tiba yake ni nini?Mungu awabariki.
 
Mkuu mimba under normal circumstance haizidi wiki 37, japo kuna nyingine zinaenda mpaka wiki 40. Cha msingi ni kumuuliza kama mtoto anacheza. Pia ni vizuri akaenda sehemu/hospitali ambayo wanafanya ultrasound kwani ina uwezo wa kuestimate age ya mimba na pia siku ya kujifungua.
 

Acha kudanganya kuna kigezo cha gestation period,development na conception ambacho kinafanya week kuwa tofauti kulingana na kigezo kitachoangaliwa katika hali ya kawaida inafika hadi week ya 42 baada ya hapo ndipo daktari anatakiwa kuchukua hatua
 
Ultrasound alipiga na ilionyesha mtoto yuko vizur kabisa na siku zimetimia kabisa kwan na mtoto keshakaa pozi la kutoka kabisa,mtoto anacheza kama kawaida na sista kazi zake anafanya kama kawaida.
 
Wangu alikuja na 40 weeks exactly. Kuna mdada alikuwa 42 weeks na aliambiwa arudi home hakuwa hata na dalili za kujifungua karibuni. Dilation ilikuwa bado hasa.
 
Acha kudanganya kuna kigezo cha gestation period,development na conception ambacho kinafanya week kuwa tofauti kulingana na kigezo kitachoangaliwa katika hali ya kawaida inafika hadi week ya 42 baada ya hapo ndipo daktari anatakiwa kuchukua hatua
Sasa hili ni tatizo gani? Maana baada ya kuona amepitiliza zaidi daktari akaona afanyiwe upasuaji, lakini presha inapanda sana ?
 

get your facts right. Some issues are too sensitive to allow room for absurdity.
 
Wangu alikuja na 40 weeks exactly. Kuna mdada alikuwa 42 weeks na aliambiwa arudi home hakuwa hata na dalili za kujifungua karibuni. Dilation ilikuwa bado hasa.

Mi mwenyewe alifikisha 40 weeks
 
Sasa hili ni tatizo gani? Maana baada ya kuona amepitiliza zaidi daktari akaona afanyiwe upasuaji, lakini presha inapanda sana ?

hebu jaribuni kwenda hospital kubwa zaidi kama muhimbili hili linaitaji wataalamu wenyewe
 

normal pregnancy ni wiki 40 inaweza kupungua au kuzidi mbili.
 

duh!! kumbe hili linawakuta wengi ee,mm wiki ya 42 inaingia sioni hata dalili.ooooh lord!
 
nduguyo bado hajashusha injini?
Bibie hujambo lakini The secretary inaonyesha bado hajashusha engine mkuu.@everlenk Mwambie ndugu yako ale tende inshallah atajifunguwa haraka iwezekanavyo ale tende kila siku. Utafiti umeonyesha kuwa tende husaidia kutanua misuli ya mji wa mimba wakati mwanamke anapokaribia kujifungua, hii husaidia kumfanya mwanamke asipoteze damu nyingi wakati wa kujifungua.

chanzo. https://www.jamiiforums.com/jf-doctor/282416-faida-za-tende-mwilini-mwako.html#post4109642
 
Last edited by a moderator:
Miezi 11 ni ki2 cha kawaida kabisa kwenye ukoo we2 ..na kwenye koo kama hizo ambazo mimba ni miezi 11 hao wa2 hula chumvi nyingi hasa
 
nduguyo bado hajashusha injini?
Ashushe wapi!! Yaani ndio anazidi kuwa fiti kama hana kiumbe,hana hata dalili ya uchungu. Nyumba zetu ziko jirani leo asbuhi wakat napita nimemkuta bize akiandaa maandalizi ya menu kwaajili ya New year nikabaki namshangaa tu!
 
Mungu muweza wa yote amsaidie ili ajifungue salama, mmemshirikisha tabibu wa karibu, tabibu wa ajabu, ingawa sijajua ni dini gani lakini kama ni mkristo yupo Tabibu wa kweli YESU, ombeni sana na Mungu ni mwema yeye atajibu na atajifungua salama.
 
Ashushe wapi!! Yaani ndio anazidi kuwa fiti kama hana kiumbe,hana hata dalili ya uchungu. Nyumba zetu ziko jirani leo asbuhi wakat napita nimemkuta bize akiandaa maandalizi ya menu kwaajili ya New year nikabaki namshangaa tu!
Au labda alokosea kuhesabu?ina maana hata ule uchungu fake huwa hausikii?pole zake mimi my firstborn nilikwenda mpaka 42 nikafanyiwa C section,wa pili nikajifungua at 38,ssa my no 3 nipo wk ya 36 natamani niende mpaka 40. ila miezi 11 ni mingi bwana labda kama alikosea mahesabu
 
Asante sana Dk wetu kwa ushauri na tutaufuatilia.
 
Last edited by a moderator:
Mungu muweza wa yote amsaidie ili ajifungue salama, mmemshirikisha tabibu wa karibu, tabibu wa ajabu, ingawa sijajua ni dini gani lakini kama ni mkristo yupo Tabibu wa kweli YESU, ombeni sana na Mungu ni mwema yeye atajibu na atajifungua salama.
Binafsi nalitambua hilo na ninamuombea kila siku, sista alikuja olewa na muislam lakini huwa tunafanya maombi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…