Ushauri: Ujenzi wa nyumba

Ushauri: Ujenzi wa nyumba

Rose Bud

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2013
Posts
252
Reaction score
256
Wakuu nimeamua kujenga, Mjini hakuna baba/mama mwenye gari ila baba/mama mwenye nyumba. Naomba ushauri juu ya mbinu na njia zote za kubana matumizi kuanzia hatua za kwanza za ujenzi hadi za mwisho. Nahitaji economical and efficient ways za kujenga nafuu. Karibuni
 
Kuna threads nyingi sana humu za ujenzi ... Fuatilia utajifunza mengi. Ila watakuja wajuvi kukupa ushauri zaidi.
 
Story live ila ya zamani: Baada ya kutoka JKT, best aliajiriwa Maji Ubungo. Akasaidiwa vijisenti na ndugu na kununua kiwanja Makongo. Enzi hizo hata usafiri kulikuwa hakuna hivyo alikuwa anasafiri kwa baisikeli kupitia Ardhi- UDSM mpaka kazini. Akajenga choo na chumba kimoja pembeni kabisa kiwanjani. Akitoka kazi au jioni mwenyewe anapiga tofari na kuchimba msingi. Zege na nondo alishonewa na kusaidiwa na ma technitian wa maji ambao walikuwa rafiki zake. Malipo ni bia za jioni pale kwake - palikuwa patupu bado. Obviosly, kila bidhaa alikuwa anaagiza na kupokea mwenyewe. Funzo: alikata cost za upangaji, cost za usafiri, vikao vya baa na sherehe zisizo na msingi, kula nyumbani, labour and specialists cost. Chukua uonalo linafaa.....
 
Kuna uzi humu ungejaribu kuupitia ungepata mwanga wapi kwa kuanzia...
 
Back
Top Bottom