Ushauri: Ukweli umeshaanza kujulikana, ni vizuri tupunguze malumbano

Ushauri: Ukweli umeshaanza kujulikana, ni vizuri tupunguze malumbano

joto la jiwe

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2017
Posts
26,117
Reaction score
46,617
Ni wazi kwamba kwa muda mrefu tumekua tukilinganisha na kutunishiana misuli kati ya Kenya na Tanzania kwa kulinganisha maeneo mbalimbali ya kimaendeleo, kisiasa, kijamii na kimichezo.

Sasa hivi kila mmoja wetu hapa JF na nje ya JF raia wa hizi nchi mbili anayefuatilia kwa makini yanayotokea, tayari amepata jibu la huu mnyukano unavyoelekea, na hali ilivyo kati ya Kenya na Tanzania.

Binadamu tumeumbwa na mapungufu mengi, hasa sisi waafrika tumeumbwa na mapungufu ya kutokubali kushindwa na kukiri hadharani, ndio sababu ukiachana na Nigeria, Ghana na South Africa, Hakuna nchi ambako walioshindwa kiti cha urais wamekiri na kuwapongeza walioshinda, japo baadae wanakiri kwamba kweli walishindwa.

Ombi langu kwa sasa, ni vizuri kupunguza malumbano ya kulinganisha kwa lengo la kishabiki ili kuonekana upande mmoja ni bora kuliko upande mwingine, badala yake kujaribu kuonyesha yale ambayo tunahisi upande wa pili unafanya vizuri ili upande mwingine uweze kujifunza.

Mimi binafsi ningependa sana kujua na kujifunza kwanini bandari ya Mombasa inapata na kupokea mizigo mingi kuliko bandari ya Dar es salaam wakati bandari ya Dar es Salaam inahudumia nchi nyingi kuliko Mombasa?

Karibuni wadau kuchangia?
 
Afu huo ukweli uliojulikana ni upi?
Huko ndiko nisikotaka kupekenyua, nimesema kwa kila mtu mwenye kufuatilia kwa undani, atagundua ukweli upo wapi kati ya hizi nchi mbili, hata wewe kama unafuatilia utagundua ukweli upo wapi? Au wewe ni mpaka mtu atangazwe na kunyenyuliwa mkono juu kama kwenye mchezo wa Ngumi?, hata huko kwenye mchezo wa ngumi pia watu wanapinga na kukataa matokeo hata baada ya bingwa kutangazwa na kunyenyuliwa mkono huu[emoji23][emoji23]
 
Huko ndiko nisikotaka kupekenyua, nimesema kwa kila mtu mwenye kufuatilia kwa undani, atagundua ukweli upo wapi kati ya hizi nchi mbili, hata wewe kama unafuatilia utagundua ukweli upo wapi?, au wewe ni mpaka mtu atangazwe na kunyenyuliwa mkono juu kama kwenye mchezo wa Ngumi?, hata huko kwenye mchezo wa ngumi pia watu wanapinga na kukataa matokeo hata baada ya bingwa kutangazwa na kunyenyuliwa mkono huu[emoji23][emoji23]
Huna data umeandika hisia huna ulichofatilia huna unacho kijua.
 
Huko ndiko nisikotaka kupekenyua, nimesema kwa kila mtu mwenye kufuatilia kwa undani, atagundua ukweli upo wapi kati ya hizi nchi mbili, hata wewe kama unafuatilia utagundua ukweli upo wapi?, au wewe ni mpaka mtu atangazwe na kunyenyuliwa mkono juu kama kwenye mchezo wa Ngumi?, hata huko kwenye mchezo wa ngumi pia watu wanapinga na kukataa matokeo hata baada ya bingwa kutangazwa na kunyenyuliwa mkono huu[emoji23][emoji23]
Uganda ndo jibu bado Uganda wana mazoea na Bandari ya Mombasa (over 90% of their cargo) na mpaka tutakapokuwa na Mabenki yetu Uganda na SGR kukamilika ndo tunaweza kushindana na Kunyaland vizuri ila so far bado na ukizingatia proximity kati ya Kampala na Nairobi!
 
Huna data umeandika hisia huna ulichofatilia huna unacho kijua
Swali nililouliza ambalo ndio lengo langu ni kuhusus bandari ya Mombasa, sasa huko unakosema wewe kuhusu data kunakujaje hapa?, huko unakotaka wewe ndiko ambako tunataka kuachana nako, au wewe unaulizia data gani?, labda sijakuelewa ujue.
 
Uganda ndo jibu bado Uganda wana mazoea na Bandari ya Mombasa (over 90% of their cargo) na mpaka tutakapokuwa na Mabenki yetu Uganda na SGR kukamilika ndo tunaweza kushindana na Kunyaland vizuri ila so far bado na ukizingatia proximity kati ya Kampala na Nairobi!
Iweje Uganda, South Sudan,na Kenya ambao ndio watumiaji wakubwa wa Bandari ya Mombasa wazidi Tanzania, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi na Easter DRC?
 
Iweje Uganda, South Sudan,na Kenya ambao ndio watumiaji wakubwa wa Bandari ya Mombasa wazidi Tanzania, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi na Easter DRC?
Yaani ina maana huna uwelewa kwamba nchi kama Zambia, Zimbabwe na Malawi ziko linked pia na Nacala, Beira, Port Elizabeth, Windhoek na Angola! Tumia muda wako kuangalia existing ports kwenye ramani!

Screen-Shot-2019-06-11-at-17.05.30.png
 
Swali nililouliza ambalo ndio lengo langu ni kuhusus bandari ya Mombasa, sasa huko unakosema wewe kuhusu data kunakujaje hapa?, huko unakotaka wewe ndiko ambako tunataka kuachana nako, au wewe unaulizia data gani?, labda sijakuelewa ujue.
Ila ni kama unatafuta mchawi nyumba ya Ibada tumia google utaona nchi kama Zambia zina alternatives zaidi ya nne! TPA ikiweza kuchukua 40% ya Ugandan cargo Mombasa ni sahau! Na ndo wanachokihangaikia!
 
Yaani ina maana huna uwelewa kwamba nchi kama Zambia ziko linked pia Beira, Windhoek na Angola! Tumia muda wako kuangalia existing ports kwenye ramani!

Screen-Shot-2019-06-11-at-17.05.30.png
Mbona hata Uganga 20% ya mizigo yao hupitia Tanzania, hata South Sudan baadhi ya mizigo hupitia bandari zingine.

Lakini zaidi ya 80% ya Mizigo ya Zambia, Malawi, Burundi, Rwanda na 60% ya mizigo ya DRC hupitia Tanzania.
 
Mbona hata Uganga 20% ya mizigo yao hupitia Tanzania, hata South Sudan baadhi ya mizigo hupitia bandari zingine.

Lakini zaidi ya 80% ya Mizigo ya Zambia, Malawi, Burundi, Rwanda na 60% ya mizigo ya DRC hupitia Tanzania.
Aisee maswali yako yanaenda nje ya logical thinking! I can't help u make use of google! hiyo 20% sijui umeipata wapi.
 
Ila ni kama unatafuta mchawi nyumba ya Ibada tumia google utaona nchi kama Zambia zina alternatives zaidi ya nne! TPA ikiweza kuchukua 40% ya Ugandan cargo Mombasa ni sahau! Na ndo wanachokihangaikia!
Kwahiyo kati ya Mombasa na Dar ni bandari gani unayodhani inahudumia nchi nyingi zaidi?
 
Uganda ndo jibu bado Uganda wana mazoea na Bandari ya Mombasa (over 90% of their cargo) na mpaka tutakapokuwa na Mabenki yetu Uganda na SGR kukamilika ndo tunaweza kushindana na Kunyaland vizuri ila so far bado na ukizingatia proximity kati ya Kampala na Nairobi!
Simple tu ni kwamba Kenya inaimport almost everything in its domestic market, hata ukiangalia asilimia kubwa ya mzigo wa Mombasa unaishia Kenya and most of it ni chakula tofauti na Tanzania ambayo importation rate yake ipo chini.
 
Kwahiyo kati ya Mombasa na Dar ni bandari gani unayodhani inahudumia nchi nyingi zaidi?
Check stats wacha "ku-politik" mambo! Ukiacha shaba na mafuta most of Zambian cargo inatoka other ports! Angalia surge ya cargo baada Dar Port kipindi cha lock down nchi ya SA na other SADC nations with seaports!
 
Back
Top Bottom