Ushauri: Viongozi wa CHADEMA mkamtembelee hospitali Abdul Nondo

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Pamoja na ukweli kuwa Abdulu Nondo na chama wake walikuwa hawawaungi mkono katika mapambano ya kupinga vitendo vya utekaji na uuaji, nawashauri muonyeshe ukomavu wa kwenda hospitali ya Aghakan kumtembelea Abdulu Nondo alielazwa hosptalini hapo baada ya kutekwa na kisha kujeruhiwa.

Kama viongozi wa Kamati Kuu bado mpa Dar-es-Salaam, nawashauri wote mfike kumjulia hali kabla ya kurudi mikoani. Mkifanya hivyo, mtakuwa mmefanya jambo la kiungwana na lenye kuonyesha ni namna gani mmekomaa kisiasa na zaidi itaonyesha kwa vitendo ni jinsi gani CHADEMA na viongozi wake wanaumizwa na kukerwa na vitendo hivi.

Isitoshe, mkimuona physically, itasaidia nyinyi na watu wengine kujiridhisha kuhusu yeye kujeruhiwa.

Pia, watanzania msishangae kuwaona Mwenyekiti na Katibu Mkuu wa CCM kwa nyakati tofauti wakienda kumjulia hali na kuahidi serikali itachukua hatua.

Nawasilisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…