GARETHBALE
Member
- Dec 22, 2013
- 76
- 333
Hii tuanze tu hata bila kusalimiana wala kuzingatia itifaki maana sasa kila mwananchi ana maswali mengi kuliko majibu hivyo salamu na itifaki hazisaidii kutafuta majibu ya maswali vichwani wa wananchi.
Tujiulize; Bashiru anashauri Membe ajiunge na upinzani na huko akagombee urais. Sasa kwa ushauri huu tunahitaji ushahidi gani zaidi kwamba kilichomfanya Membe afukuzwe CCM ni nia yake ya kugombea urais ndani ya CCM? Bashiru kwamaneno mengine anahalalisha alichokisema Membe kwa 100%. Anachotuambia Bashiru kwamba ukipingana na bosi wake na kutaka kugombea kiti cha bosi wake utafukuzwa.
Tujiulize pia; Bashiru anashauri Membe akate rufaa na kwamba peni Bashiru imejaa wino tayari kumruhusu arudi. Ili tujue anachotaka Bashiru tujue tujiulize swali moja la msingi: Je Membe ameulalamikia uamuzi mahala popote kwamba haukuwa wa haki? Hii washawasha ya Bashiru kumshauri Membe akate rufaa inatoka wapi? Inatokana na wasiwasi gani?
Tuendelee kujiuliza; Bashiru anashauri Membe ajiunge na upinzani na huko agombee urais. Sasa hapa inabidi utumie ubongo wa ziada kujua lengo hasa la Bashiru katika ushauri huu. Tuanze. Musiba alimtuhumu Membe kuhujumu uongozi wa juu, Membe kimya. Musiba hakuishia hapo, akapendekeza Membe afukuzwe chama, Membe kimya. Bashiru huyu huyu akajitika madafu ya Musiba na kumtaka Membe ajieleze, Membe akamtafuta Bashiru lakini Bashiru akaingia mitini akapotea Membe kimyaa.
Kisha Bashiru akasikika mara kadhaa akisema ni ruhusa mtu kuhama CCM. Kitendo cha propaganda kikatumia muda mwingi kupiga propaganda za Membe kuhamia ACT. Membe kimyaa. Mtego wa Bashiru kumtaka Membe ahame chama ukabaki ukibadirishwa chambo tu. Sasa nadhani hadi hapa tunajuwa maana ya ushauri wa Bashiru kumtaka Membe aende upinzani.
Nisimalize hapa bila kujiuliza kile ambacho Membe alihoji na waandishi wakashindwa kumhoji Bashiru jana. Membe "alikatwa" au "kupata kura chache" NEC mwaka 2015. Haki yake ya kupiga na kupigiwa kura kwa mujibu wa katiba alipewa. CCM sasa inashindwa wapi, inaogopa nini, inakosa nini, au inatatizo gani "kumpiga ngwala" tena Membe kwenye uchaguzi wa ndani CCM? Swali hili kwa undani wake katika majibu yake ndio chanzo cha mtafaruku ndani ya chama hiki kikongwe. Ni chama kinachoathirika na virusi vya korona kwa kasi ya ajabu.
Nitarudi baadaye kidogo.
By Maarifa Kupapasa-Maarifa Kutomasa.
Tujiulize; Bashiru anashauri Membe ajiunge na upinzani na huko akagombee urais. Sasa kwa ushauri huu tunahitaji ushahidi gani zaidi kwamba kilichomfanya Membe afukuzwe CCM ni nia yake ya kugombea urais ndani ya CCM? Bashiru kwamaneno mengine anahalalisha alichokisema Membe kwa 100%. Anachotuambia Bashiru kwamba ukipingana na bosi wake na kutaka kugombea kiti cha bosi wake utafukuzwa.
Tujiulize pia; Bashiru anashauri Membe akate rufaa na kwamba peni Bashiru imejaa wino tayari kumruhusu arudi. Ili tujue anachotaka Bashiru tujue tujiulize swali moja la msingi: Je Membe ameulalamikia uamuzi mahala popote kwamba haukuwa wa haki? Hii washawasha ya Bashiru kumshauri Membe akate rufaa inatoka wapi? Inatokana na wasiwasi gani?
Tuendelee kujiuliza; Bashiru anashauri Membe ajiunge na upinzani na huko agombee urais. Sasa hapa inabidi utumie ubongo wa ziada kujua lengo hasa la Bashiru katika ushauri huu. Tuanze. Musiba alimtuhumu Membe kuhujumu uongozi wa juu, Membe kimya. Musiba hakuishia hapo, akapendekeza Membe afukuzwe chama, Membe kimya. Bashiru huyu huyu akajitika madafu ya Musiba na kumtaka Membe ajieleze, Membe akamtafuta Bashiru lakini Bashiru akaingia mitini akapotea Membe kimyaa.
Kisha Bashiru akasikika mara kadhaa akisema ni ruhusa mtu kuhama CCM. Kitendo cha propaganda kikatumia muda mwingi kupiga propaganda za Membe kuhamia ACT. Membe kimyaa. Mtego wa Bashiru kumtaka Membe ahame chama ukabaki ukibadirishwa chambo tu. Sasa nadhani hadi hapa tunajuwa maana ya ushauri wa Bashiru kumtaka Membe aende upinzani.
Nisimalize hapa bila kujiuliza kile ambacho Membe alihoji na waandishi wakashindwa kumhoji Bashiru jana. Membe "alikatwa" au "kupata kura chache" NEC mwaka 2015. Haki yake ya kupiga na kupigiwa kura kwa mujibu wa katiba alipewa. CCM sasa inashindwa wapi, inaogopa nini, inakosa nini, au inatatizo gani "kumpiga ngwala" tena Membe kwenye uchaguzi wa ndani CCM? Swali hili kwa undani wake katika majibu yake ndio chanzo cha mtafaruku ndani ya chama hiki kikongwe. Ni chama kinachoathirika na virusi vya korona kwa kasi ya ajabu.
Nitarudi baadaye kidogo.
By Maarifa Kupapasa-Maarifa Kutomasa.