Ushauri wa biashara ya maziwa na fresh foods kwa jijini mbeya

HAZOLE

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2011
Posts
1,551
Reaction score
713
Ninampango wa kufunguwa duka la kuuza maziwa fresh, mgando kwa jumla na rejareja pia samaki wabichi kwa hapa mbeya mjini.
Naomba nijue yafuatayo kwa uzoefu wako ktk hii tasnia ya fresh foods.
1. Location iweje
2. Usimamizi pale unapoweka MTU wa kuuza
3. Changamoto zake mfano wateja, muuzaje aweje, bidhaa kuharibika n.k.
4. Faida ipoje.
5. Nini nifanye kuboresha
: Lengo nije kuwa mfugaji hasa fish. Kwahiyo hii itakuwa motivation kubwa ya ufugaji huuπŸ™πŸΏπŸ™πŸΏπŸ™πŸΏ
 
Huwez anzisha biashara akati hujui lolote.. fanya research physical...
 
Changamoto mbeya ni Ubinafsi&Ushirikina
Nasikia unaweza kua unauza TV wateja wakija wanaona ni duka la chupi za watoto. Mwingine alikua na pick up wateja wakija wanaona kumetolewa tyre kinatengenezwa
 
Mkuu kwa kukushauri tu utafute sehemu yenye idadi kubwa ya watu...pale kabwe mwanjelwa kuna sehemu zinapaki bajaji nyingi ukipata chumba maeneo yale itapendeza...wateja wengi wa maziwa fresh wakati wa jioni mara nyingi wanakuwaga ni watu wanaofanya manual work...location nyingine chuo cha t.i.a or mzumbe ukipata chumba sehemu nzuri kwenye hivyo vyuo utafanya biashara...mwambene stand pia naona pamechangamka unaweza fanya iyo biashara ya maziwa fresh na mgando+vitafunwa....kama uko serious nicheki pm nikakuoneshe mtu anaefanya biashara kama iyo unaweza jifunza kitu
 
Nasikia unaweza kua unauza TV wateja wakija wanaona ni duka la chupi za watoto. Mwingine alikua na pick up wateja wakija wanaona kumetolewa tyre kinatengenezwa
Mbeya,ukifika ,tii msemo unasema uliza wenyeji
 
Hivi kwanini wabongo mmekariri kufanya biashara lazima upange fremu?

Ushauri wangu

Ni bora ujichange au ukodishe kirikuu uwe unatembeza maeneo mbali mbali hpo mbeya

Ukipanga fremu unakuwa km unajikaba mwenyewe maana utakuwa umejilimit wateja wa kuwahudumia

Usisubiri wateja wakufate ulipo wafate huko huko walipo.
 
Vipi upo serious kufanya biashara ya kuuza maziwa ya ngo'mbe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…