Ushauri wa bure kwa Diamond

Mayu

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2010
Posts
7,621
Reaction score
12,505
Ni ukweli ulio wazi kwamba umefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuvuka changamoto ya kuupeleka mziki wako ukubalike nje ya Tanzania. Hivi sasa mpenda muziki yeyote Africa anajua muziki wako na kukufatilia kwa karibu sana

Najua unatengeneza pesa nzuri kuliko msanii yeyote East Africa kwa sasa lakini binafsi naona bado hujafanikiwa kutengeneza pesa kulingana na jina lako na muziki ulijitengenezea

Najaribu kuangalia wasanii ambao upo nao level moja angalau kwa sasa wanvyopiga shows all over the Africa
Angalia Acc za Insta za P-square au Davido.

Sioni ukipiga matour ya maana ukiachilia Kenya, Uganda, Tz, Burundi, Rwanda. Natamani nikuone unajaza nyomi Cameroon au Ghana au Misri South Africa n.k.

Show za USA na UK zinalipa sawa lakini himaya yako ipo Africa wanakokutambua, wapige hela bana!

Hii ni changamoto kwa Fella na team yako yote. Tafuteni mapromota wa nchi husika mkapige hela bana! Shows za Tz Pekee hazitoshi, andaa tour moja matata Africa, huu ni wakati wako na hautakaa juu milele.

Ni hayo tu.. Naamini unakatiza mitaa hii kuchungulia na kama sio wewe basi wapambe wako!
 
Kwani haujaona tangazo la kwenda kupiga ma show nje walilorushaga zinakuja karibuni?

Pia nenda ukaone meneja wake mmoja yupo wapi jana na leo?

Wanapiga kazi kwa kweli.
 
davido chemelione fally pupa p.square huwezi kumlinganisha na baba levo bhana anaebebwa kwa skendo hao ni nouma angalia maisha yao magari manyumba na show gharama wanazolipwa ni kiboko sana daimond bado sana msituaminishe ujinga
 
davido chemelione fally pupa p.square huwezi kumlinganisha na baba levo bhana anaebebwa kwa skendo hao ni nouma angalia maisha yao magari manyumba na show gharama wanazolipwa ni kiboko sana daimond bado sana msituaminishe ujinga

Ningeona ajabu kama msinge jitokeza....mwenzako katoa ushauri wewe una ponda bila shaka una elements za uchawi ..!!
 
Trend yake sio mbaya, kashapita Congo, Burundi, Rwanda, Uganda, Kenya, so kwavile anazidi kutanua fanbase namtabiria mwakahuu kabla haujaisha atakuwa kapiga show za maana west na south Africa
 
davido chemelione fally pupa p.square huwezi kumlinganisha na baba levo bhana anaebebwa kwa skendo hao ni nouma angalia maisha yao magari manyumba na show gharama wanazolipwa ni kiboko sana daimond bado sana msituaminishe ujinga

Safari ni hatua
Ndio anashauriwa awafikie sasa, we unapinga nini
Level ya Diamond hao ndio wenzake wanamzidi kipato tu na ndio anashauriwa afanyaje awafikie

Alishauriwa atafute kolabo akafanikiwa kuiteka africa sasa kilichobaki ni kumake money tu
 
Kubali KUTOFAUTIANA.Sio mwenzio anapinga nawe unamvamia, simamia katika kile unachokiamini.
Hakuna aliyekulazimisha kukubaliana nae.
Inategemea unatofautiana vipi, sio unapinga tu kwakuwa humpendi mtu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…