Ushauri wakuu kozi ya kusoma mtoto ambaye hakufaulu kidato cha nne

professional ethics

Senior Member
Joined
Dec 24, 2023
Posts
108
Reaction score
350
Wakuu habari na dogo langu hapa (mtoto wa mama mdogo), Matokeo yake ya kidato Cha nne hayajawa mazuri sana kwani kapata division four.

Hivyo mama mdogo kanitafuta nitoe ushauri juu ya fani ipi dogo akasome veta, binafsi nimeona kozi ya fashion designing, sewing and cloth technology itamfaa sana, na binafsi nimeongea ane kasema anapenda mambo ya fashion na ushonaji..

Zaidi ya hapo nimefatilia kozi hiyo veta, wanasema Inachukua miaka mitatu na ada yake ni laki na 20 per Year.


Wakuu naomba kuuliza kwa anae ijuia vizuri hii kozi je inaweza msaidia dogo akajiajri na kuajirika. Jinsia yake ni ke
 



Hiyo fani nzuri anaweza kupata kazi katika viwanda vya nguo

Pia anaweza kujiajiri kwa kufungua workshop kushona suti. Nk.

Kila njia inatoka katika maisha kikubwa mfundishe kuwa awe humble na amtangulize Mungu kwa kila jambo.

Akae mbali na ngono ili atunze re-born and born
 
Shukrani mkuu
 
Hiyo fani ni nzuri, inampatia fursa ya kujiajiri mwenyewe pasipo mtaji mkubwa ( Mtaji wake ni ofisi na vitendea kazi baadhi).

Akiwa fundi mzuri na akajulikana ni biashara nzuri sana kwa maeneo yote, mjini na vijijini, ushuani na uswahilini.
 
Mfano ukimaliza NVA level three in ICT au lab assistant. Anaenda kusoma diploma
 
Nasikia DIT MWANZA CAMPUS wanapokea waliomaliza NVA level three waje kusoma science and laboratory diploma au IT diploma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…