Uchaguzi 2020 Ushauri wangu kwa Magufuli na CCM: IKiwa Magufuli ataacha kupiga kampeni atapata kura nyingi kuliko anavyoendelea kupiga kampeni

Uchaguzi 2020 Ushauri wangu kwa Magufuli na CCM: IKiwa Magufuli ataacha kupiga kampeni atapata kura nyingi kuliko anavyoendelea kupiga kampeni

dikteta2020

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2018
Posts
595
Reaction score
3,991
Huu ni ushauri wangu wa dhati na wa kweli kwa Rais Magufuli na CCM wote. Magufuli aache kupiga kampeni.

Nasema hivyo kwa sababu naamini kuwa kadiri anavyozidi kupiga kampeni wapo wapiga kura lukuki anawapoteza kirahisi kabisa. Nasema ukweli na ndivyo ulivyo.

Aidha kama atalazimika kuendelea kupiga kampeni basi asionyeshwe live! Kumuonyesha live kunapoteza kura nyingi sana ambazo angezipata kwa watu kutokusikiliza baadhi ya maneno kutoka kwake ambayo kimsingi yanavunja moyo.

Mzaha anaofanya kwenye kampeni huku akijua fika kuwa wapo walioumizwa na utawala wake kunazidisha kutokukubalika na kutakuwa na madhara makubwa kwenye sanduku la kura.

Huu ni ushauri wangu japo ni mfupi ila mwenye macho na auone, mwenye masikio na ausikie na mwenye mikono aufanyie kazi.
 
kwa hiyo unataka kutuambia kwamba kadri siku zinazozidi kufikia 28th Oct. Mzee ndiyo anazidi kuharibu siyo!!
 
Ushauri wako ni mzuri sana kama watazingatia... Ushahidi mdogo huu hapa kuonesha anavyojichanganya:


Screenshot_20200929-120211.png
Screenshot_20200929-120305.png


Kwa wenye akili wanajua kuwa akusharudi madarakani ataanza kutekeleza mengi yenye madhara kwa wananchi tofauti na Ilani anayojitembeza nayo...
 
Wewe akili yako ni matope, amekaa kimya sku nne timu makelele wakaanza kujiapisha , kampeni sku ya pili Leo , nyuzi za Lissu zimezimika ghafla alaf unasema tukae kimya , wananchi wanatusubir huko tutatue kero ....aliyekutuma amekudanganya
 
Back
Top Bottom