Ushauri wangu kwa Zuberi Zitto Kabwe


umeandika vizuri lakini hiyo point ya kwanza nadhani hujamtendea haki maana huu ni wakati wa bunge na yuko dodoma, hayo mengine sina comment atajua mwenyewe kama hiyo roho ya unafiki ni kweli anayo
 
zito ana kiburi kwa kufikiri wale bongoflavour wake watampeleka ikulu unahitaji baraka za chama sio za kikwete
Huyu angeweza kupuuzwa, lakini kwa mapesa aliyokusanya toka ndani na nje ya nchi ili kutimiza ndoto zake, huyu si hatari kwa CDM tu, ni hatari kwa ustawi wa taifa hili. Hawa wanaompa mapesa toka nje wana malengo gani? Atawarushiaje mapesa yao? Think twice.
 
Point ya kwanza hata mi najiulizaga.. Mbona zitto hatumuoni kwenye mikutano yao wanayofanya. Hivi zitto hajui kua chadema ikishinda uchaguzi haitakua kwa sababu yake yeye bali itakua ni kwa sababu ya mbowe nasarri slaa na kina lema maana hap ndio wamekua wanazunguka nchi nzima kitafuta wanachama na kueneza sera zao wakati huo zitto ye yuko marekani na kukaa na wanamuziki. Yeye anaonekana zaidi na viongozi wa ccm kuliko chadema wenzake..baadhi ya hoja hapo juu ni za kweli huyu jamaa ataisambaratisha cdm na sitashangaa kikwete na ccm wakitaka zitto
Agombee kwa cdm coz wanajua kama zitto akishinda basi interests za viongozi wa ccm zitalindwa... Leo hii ni bora lowassa kua rais kuliko zitto coz at least tunajua lowasa ni mchapa Kazi ana experience na nchi haitayumba kama inavyoyumba sasa chini ya JK
 

Safi? Haha haha hah haaaaaaa!!!!! Imekula kwa boss sisi hatudanganyiki
 
mimi nina malalamiko kwa moderators wa jukwaa hili, yaelekea nyie mna nia moja na hawa watu wenye nia ya kumchafua mh Zitto, kwanza kwa nini mumeunganisha thread ya Mkandara na huu upuuzi wa watoto? Pili inakuwaje out of nowhere mtu anaanzisha tu thread ya kumtukana Zitto as if kuna jambo jipya nanyi mnaziacha thread kama hizi? kama si kumchafua Zitto ni nini? mumeona imepita wiki sasa hakuna jambo toka kwa Zitto then watu wanaanza kumpaka matope nanyi mnaachia tu? huu ni upuuzi na kama mtaacha hawa watoto wanaotumwa kufarakanisha watu kwenye chama basi tutajua na nyinyi mnahusika

kuweni mods werevu bwana!!!!
 

Hivi wewe unaamini kabisa kuwa kuna mtu tajiri wa kweli Tanzania? Hawa mafisdi haki ya Mungu wangeletwa na familia na ndugu zao wa karibu hadharani wakionyesha makazi na vyakula wanavyokula ungeachwa hoi kwa mshangao juu ya umasikini walio nao. Unayoona ni ulimbukeni na ulafi tu. Mafanikio ya dhati hayapatikani kwa ulaghai ndugu yangu. Uadilifu ni silaha ya ajabu natulisisitize hili katika maisha yetu, jamaa, ndugu na marafiki. Mungu ingilia kati badili mtazamao wetu tukuangalie wewe tu. Mungu ibariki Tanzania
 
Mwanzoni nilidhani una nia kweli ya kumshauri zito ila baada ya post hii naanza kutilia shaka kama nia yako ilikuwa ni kumshauri zito au ulitaka kupima upepo kama imani ya watu imepotea kwa zito.
Nakushangaa kwamba bado unamtetea zito kuwa anapakwa matope wakati vituko vya zito vinaoneka wazi katika matamko yake. Hata mbumbumbu hapati shida kuelewa anachokifanya zito ktk matamko yake. Kama una nia njema na zito ungana na sie tunaosema wazi kwamba zito anatumiwa na ccm. CCM wanajua kuwa hawana njia nyingine ya kuiyumbisha chadema zaidi ya kumtumia Zito, wanajua kuwa chadema wakimchukulia hatua zito basi ile zana ya ukabila na udini wanayojaribu kuipandikiza itapata nguvu. Bahati nzuri viongozi wa chadema wanalijua hilo na wako makini, wamemwacha zito aendelee kuropoka wakijua wakati utafika ambapo zito atajiangusha mwenyewe na hapo ndio atagundua CCM ni nani.
 
Nakuelewa kabisa, na unachoongelea ni ndivyo inavyopaswa kuwa lakini kiuhalisia haiko hivyo! Na mimi nimejaribu tu kuelezea hali halisi ilivyo kwamba katika mazingira yetu ili ufanikiwe kisiasa unahitaji pesa tena sio pesa tu bali pesa nyingi na ndio maana unaona pamoja na kashfa zote za ufisadi na mengine bado akina Chenge na Lowasa ni wabunge wakuchaguliwa na kuwashinda ni kazi ngumu, wewe leo ukienda Bariadi unataka kugombea utaongea mpaka uanguke hata kama ni kweli kiasi gani lakini mwisho wa siku hata wasikilizaji watakuwa wachache lkn akija Chenge watajaa utashangaa!

Sasa nilichomaanisha tu ni kwamba hao akina Zito & Co. wanalijua hilo kwamba wanahitaji pesa sasa watazipata wapi na kwao hamna? Ndipo Ufisadi unapokuja hapo. Mfano tu mdogo angalia hata hiyo concert ya Kigoma ambayo labda ilikuwa ni ya kujijenga kisiasa sina uhakika,ila bila pesa ndefu isingewezekana sasa, pesa atapata wapi na kwao maskini? na ndio maana kila siku kuna suprises!
 
The journey to the presidency is not an easy one, there are rivers to xross and mountains to climb; some rivers with crocodiles and hippos...but for ambitious ones, it is worth a journey to pursue....Go ZZK! Go

Huu ni upepo tu na utapita!
Hapa ndipo panaponishangaza mimi....yaani watu wa ccm wote wanamsapoti Zitto. kazi kweli kweli
 
Ushauri mzuri sana na mtoa mada kamfunua vilivyo kaeleza mapungufu ya zitto ambae amekuwa kero badala ya hero kama tulivodhani kwenye jamii. Nasikitika mtoa hoja kachelewa kumshauri kijana Huyu ambae niliamini angeiridhi mikoba ya Dr slaa baada ya 2025-2035 Kama angekuwa Ana play Kama mpinzani tofauti na anavo play sasa Kama mtawala. Pia Nasikitika kuwa mtoa hoja kapoteza muda wake japo anania nzuri na zitto kwani zitto nimjuaye Mimi hata pokea ushauri Huu Kama changamoto Bali atajisemea Kama kiranja mkuu (ni upepo tuu Huu utapita) bila kujali nini hasara zake. Tamaa, ulimbukeni wa kisiasa na kutofahamu majukumu ya upinzani Ndio vitamponza kijana Huyu machachari zitto mfano. Anajua kikatiba 2015 hatoweza kugombea urais kwa kigezo cha umri tuu lakini yeye bila kutambua Hilo na Nina Amini hakosi copy ya katiba nyumbani au ofisini kwake tayari kashatangaza nia au kujitangazia urais. Sidhani kama utahitaji PHD kuona mapungufu yako zitto naamini itachukua karne nzima kurudisha Imani yangu kwako na sio miaka 2 iliyo bakia. Kumbuka wapiga kura wako wa kigoma walikupigia kura sio sababu ya uwakilishi wako, mtizamo wall sura yako Bali walikuchagua sababu ya chama chako/chao chadema Watanzania wa sasa ata ukiwawekea jiwe na ccm watachagua jiwe. Angalia usijekosa hata uo ubunge 2015 achilia mbali na urais unaouota. Ee Mungu wanusuru wanasiasa vijana waepukane na zimwi limsumbuae kijana zuberi zitto Kabwe. Ameni
 
Bora umemwongelea kwani intia kinyaa.Hivi alipofikia alitumia sh. Ngapi? Azma yake ipi hiyo?Umasikini wake ndio unamponza ajipime na walionazo?sasa ya nini kununua magari ya kifahari.
 
Mtoa mada na kundi lake haawajielewi,kuwa mpinzani sio kupinga kila sera ya chama tawala. Mawazo mgando kama hayo ckutegemea kuyaona kwa mtu kama we ulowahi kwenda hata shule.

Tunajua wazi kwamba baby slaa anautaka sana urais,sio vema akautafuta kwa kuwapaka watu matope huku vijana mkitumika vibaya kiasi hicho.

Watanzania wote kwa ujumla tunaujua mchango mkubwa wa Mh.Zitto kwa Taifa hili. Hakilka hautasahaulika.
 
Mi binafsi katika wanasiasa safi kwenye kambi ya upinzani nilishamuengua Zitto kwani ni munafiki sana ila ajue sasa hivi watu wameshamudharau kulingana na kauli zake zisizokuwa na afya katika nyanja ya upinzani.
 
Hukuanza leo wala jana harakati zako kisiasa,najua na wananchi wanajua umefanya mengi ktk siasa za nchi yetu na ni mazuri tu. Mwanaharakati kama wewe si ajabu wala kashangaza unapokuwa na hamu ya kuwa Raisi mwisho wa siku.Na ninawasihi wanaCDM na wananchi kwa ujumla tusimnyooshee kidole kibaya Zitto coz ni hali ya kawaida kabisa na ni haki yake ya msingi kuwa na ambitions za uraisi na mwanasiasa yeyote aliyefikia mafanikio ya juu japo kidogo,hupenda kwenda zaidi ya alipo

Zitto tumekusikia, tumekuelewa na hatukukatazi, lakini naomba uchukue ushauri wangu brother.CHADEMA kiko safarini hivi sasa kuelekea kule vijijini na miji tata kujiimarisha,kinatizamwa kama Chama mbadala kwa sasa na wananchi waliowengi hata baadhi ya wanaCCM.
Unaifahamu mikakati ya Chama ni kwenda kwa kila raia na kueleza dhamira ya chama,kwanini usijikite,ukaungana na wazalendo wenzako ktk chama kupigana na adui kwanza, mkamtoa nyoka ndani ya nyumba,ndipo mkae kitako nani awe mkuu wa nyumba.

Kwa nini usijiunge katika ktk common goal hii! Si muda muafaka kuanza kugawana mali za baba wakati baba ni mgonjwa,yafaa tushukulikie uhai wake kwanza.Au unasahau tunajenga nyumba moja,na fito yako,ya Mbowe,ya Dr Slaa,ya Heche, ya Malya,ya kasulumbai,Msigwa na Sugu,ya Lisu Dr safari,Baregu,ama ya Halima,Wenje na hata Marehem Regia,zote zinahitajika kukamilisha ujenzi.
Tunahitaji fito sasa kwa sasa,sote tulete fito,ukileta rangi saa hizi haitafaa sana japo tutaihitaji baadae ila nahofia ita-expire kabla hatujafikia hatua hiyo.

Mbona muda wa kuzungumzia habari za Uraisi badoooo! Tutumie miaka hii kabla ya 2015 kukipatia ushindi chama mbele ya umma wa watz halafu utatumia nguvu ndogo sana kwenye hiyo dhamira yako ifikapo 2015.
By the way,unafahamu kabisa katiba ya sasa haikuruhusu kugombea,hilo pekee linatosha kukufanya uwe na kiasi na subira pia,lakini si neno.

Kuna Mchakato unaoendelea kuelekea Katiba mpya, mchakato ambao kwa hakika umefanikishwa kwa kiasi kikubwa na Chama chako, suala la umri ktk kuwania uraisi likiwa kipaumbele kwa CDM, hii ni kwa sababu ya imani ya chama kwa vijana wewe ukiwemo. Kwanini usikiweke chama mbele ili kipiganie mazingira ya kisiasa ambayo mwisho wa siku yatakua favor kwako?
Huoni kama unadhoofisha nguvu ya chama kwa kiasi kikubwa?
Usifanye hivyo brother usijeingia ktk historia mbaya kuzuia mabadiliko
 
zzk,nilimuamini sana bt kwa ss inanipa wakati mgum!mnafiki 2,halafu uzuri chama hata hakihangaiki nae mpaka atakapomaliza kuropoka
 
zzk,nilimuamini sana bt kwa ss inanipa wakati mgum!mnafiki 2,halafu uzuri chama hata hakihangaiki nae mpaka atakapomaliza kuropoka
 
mutatiana moto mwaka huu, CDM inaenda kuzimu hahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa patamuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu,
 
"bangusilo" hili neno nililisikia kwa mara ya kwanza kutoka kwa ibrahim msabaha alipokuwa anajitetea kwenye kashfa ya "richmond". Umenikumbusha mambo yale.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…