Ushauri wenu jaman jinsi ya kutumia kalenda ili usipate ujauzito

mari mari

Member
Joined
Sep 25, 2014
Posts
55
Reaction score
5
Habar za humu ndan members naomben ushaur na msaada wenu jinsi yakutumia calender. Ili kuzunisipate mimba na kujua mzunguko wangu ni mrefu or mfup or wakawaida
Kuanza mwenz wa kumi na moja siku zangu niliziona tarehe 24-27 mwenz wa kumi na mbil siku zangu zili anza tarehe 25-28, mwenz wa kwanza tarehe 20-23 .msada wenu jaman naomben
 

Siku kubadirika badirika inasababishwa na mengi wala isikutishe saana…
Labda Mazingira tofauti ya hali ya hewa,au kama uliwahi kutoa ujauzito, msongo wa mawazo na vyakula!
Hizo ni moja ya sababu za mzunguko kubadirika badirika…
Ila yote kwa yote ili usikosee kalenda kama huwezi kuzi mantain tarehe za hatari basi
tumia condom mara kwa mara…
Mwambie mmeo/mpenzio awe anamwaga nje kabla ya kufika kileleni…
na hizo ni some scientific method… ukitaka zaidi hasa kujua tarehe vizuri… nimeku pm namba… hapa sikai online saana!
 
Asante sana kwa ushaur wako nita kutext watsap
 
Anza kuzihesabu toka siku ya kwanza ya MP moja hadi siku moja kabla ya MP nyingine. Huo ndo mzunguko mzima wa hedhi.

Kwa tarehe ulizoweka, mwezi wako mrefu ni siku 31 na mfupi ni siku 26. Lakini, unapaswa kurekodi mizunguko walau 6 kuwa na uhakika wa mwezi mrefu na mfupi.

Kujua siku za hatari, chukua mwezi wako mfupi toa siku 18 na mwezi wako mrefu toa siku 10.

26 - 18 = 8
31 - 10 = 21

Maana yake, siku ya 8 ya mzunguko wako wowote hadi ya 21 ni za hatari. Hivyo usifanye kabisa km hutaki ujauzito, au jikinge. Siku nje ya hizo, jiachie kwa raha zako.

Narudia, rekodi kwa umakini mizunguko yako kwa walau miezi 6 ndipo utapata uhakika wa mwezi mrefu na mfupi. Bila hivyo, hesabu hiyo hapo juu inaweza kukosea siku moja ikala kwako.

Sijui kwanini zinatumika siku 18 na 10!

Kwa hisani ya aliveprojects.com
 

sawa kabisa mkuu... ila kwa tahadhari wote wenye mzunguko mfupi njia hii siyo rafiki sana kwao.
 
sawa kabisa mkuu... ila kwa tahadhari wote wenye mzunguko mfupi njia hii siyo rafiki sana kwao.

Ni kweli. Tuchukulie mtu mwenye mzunguko wa siku 21 usiobadilikabadilika.

21 - 18 = 3
21 - 10 = 11

Siku za hatari itakua siku ya 3 mpaka ya 11.

Hata hivyo, mimba hutunga siku ya 14 hivi tangu hedhi kuanza (kwa wenye mzunguko wa siku 28 usiobadilika) na mbegu za kiume huweza kuishi hadi siku 5 ndani ya mwili wa mwanamke. Huenda wenye mizunguko mifupi na siku ya kutunga mimba pia huwa katikati ya mzunguko i.e. siku ya 10 hivi.

Vyovyote iwavyo, kama mwanamke hataki mimba muda huo na anahitaji kufanya ngono, bora kujikinga.
 
Kwa mizunguko yake kubadirika badirika, inahitaji umakini saana…
 
Nilikuwa mtaalamu sana wa kalenda,lakini iliniumbua mara kadhaa.mwanamke njia ya uhakika ni kijiti tu.haya mengine bahati nasibu.
 

Ni PM namba yako mkuu nami nina shida hiyo kwa mke wangu
 
Ni pm tafadadhal nami nahitaj msaada zaid kuhusu jinsi ya kutumia calenda. Na jinsi ya kupata mtoto wa kike au wa kiume
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…