Ushauri wenu ni muhimu sana na nauhitaji mno katika hii azma yangu ya kutaka Kujiajiri kuliko Kuajiriwa Tanzania

Ushauri wenu ni muhimu sana na nauhitaji mno katika hii azma yangu ya kutaka Kujiajiri kuliko Kuajiriwa Tanzania

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Nafikiria kuanza kuwa nazungukia Ofisi za Taasisi mbalimbali nchini Tanzania hasa zile zenye ' Mabosi ' wakubwa wakubwa ( CEO's ) na ikibidi hata na Viongozi wa Serikali na Kitaifa ili niwe nawasaidia ' Kuwatunzia ' Mafaili yao mengi ambayo mengine huwa wanayaweka hadi Vitandani yakisubiriwa Kusainiwa.

Nitakachokifanya tu ni kwamba Mimi nitakuwa nayaendea huko huko hayo ' Mafaili ' na kuyachukua kuja kuyahifadhi Kwangu, kisha nayapanga vizuri na asubuhi hao ' Mabosi ' na ' Viongozi ' wakishaamka tu nawapelekea ili Kazi yao ya ' Kusaini ' ianze kuliko kulala nayo hapo hapo Kitandani halafu bahati mbaya labda waje ' wayakojolee ' au wayadondoshee ' Maudenda ' bure.

Na gharama yangu ya Kuyahifadhi hayo ' Mafaili ' itakuwa ni ndogo sana na nitayatunza vyema kabisa hadi wenyewe watafurahi. Lengo langu Kuu hapa ni kuwapa hao ' Mabosi ' na ' Viongozi ' muda mzuri wa Kupumzika na Wake zao kuliko muda mwingi hata usiku wa manane wao Kuwaza ' Kusaini ' tu ' Mafaili ' tena wakati mwingine wakiwa wamechoka au wana ' Stress ' zao nyingi halafu wakajikuta wanaharibu kila kitu.

Nitawashukuruni kama mtanishauri vyema katika hili wana JamiiForums wote ili nami GENTAMYCINE niweze sasa Kujiajiri au kuwa Mjasiriamali wa Kutunza ' Mafaili ' yanayotunzwa Vyumbani ama yasikojolewe au yasidondokewe hovyo na ' Maudenda ' yanayotokana na Mtu Kushikwa na Usungizi mzito.

Nawasilisha.
 
Phd
2018-11-01%2015.38.04.jpg
 
Back
Top Bottom