Ushawahi fanya figisu kuvuruga mahusiano ya watu ili awe wako?

Hii ishu sio yangu ila nilisimuliwa na dereva wa bodaboda jinsi madereva wajanja wa boda/bajaji/taxi wanavyofanya wakipata abiria wa kike pisi kali hususani akiwa ndo anaenda kwa mchizi mara ya kwanza.

Mchezo huwa unaanzia pale boda anapopewa simu ili apokee maelekezo kutoka kwa mchizi kuhusu njia ya kupita kumpeleka mrembo geto.

Dereva mjanja akishapokea simu kama hiyo tu, kichwani anakuwa ashapigia mstari kuwa hii ngoma anaigeuzia njiani (kama ngoma ameielewa inalipa).

Anachofanya ni kabla hajampa yule demu simu ni anablock ile namba ya mshkaji halafu anaweka simu airplane mode. Wako fasta sana katika hiyo kazi, demu anakuwa anaongeleshwaongeleshwa hashtukii.

Kama akiona demu kanogewa sana na stori anambadilishia kabisa namba ya mshkaji anaweka namba yake yeye halafu simu yake anaipiga silenti.

Basi wakifika sehemu fulani ya kuingilia sasa ndani ndani si inabidi wasimame kupata maelekezo zaidi, basi hapo ndo episode ya pili inaanza.

Kama namba ilibadilishwa kabisa basi hapo ndo demu anang'olewa kirahisi sana. Maana atapiga weeeee inaita tu inaita tu.

Jamaa hapo atachomekea kwamba jamaa atakuwa na demu. anaweza hata akanogesha stori kuwa hiyo sauti ya jamaa kwenye simu sio ngeni sana na anamjua jamaa kwa kuleta mademu kila siku.

Basi demu atanuna kidogo halafu atapiga tena inaita tu haipokelewi. Ikifika hapo ndo jamaa anakuwa ashapata chansi ya kuchomekea voko zake.

Unakuta demu kwa hasira ya alichofanyiwa na mshkaji anamkubalia jamaa waondoke kwenda anakotaka.
 
Nshawahi kupanga na mume wa jamaa amfukuze mkewe, mpango ulianzua gest Ili jamaa atukute kama fumanizi..Mzee nikamla kiserious)kikwelikweli.

Jamaa akaachana na mkewe.

Sintasahau dhambi ile
 
Kama ni kweli, litakukuta jambo hutakaa usahau, ogopa sana kitu kinaitwa fitina, sijui hii kitu utasafishaje mwamba!! kuna vitu vingi hatuvioni lakini kilio cha huyo jamaa kama kweli alikua akimpenda mpenz wake na wewe ukafanya hivyo kuyavunja makusudi huku ukiwa na mkeo, my friend utakuja kulia sana!! katubu na useme ukweli kuwarudisha tena pamoja
 
Nakutafuta nikumalize kumbe ndio ww.
 
DeePond una chembe chembe za ujasusi ila nimeipenda nitakuwa naomba ushauri kwako endapo nikihitaji kufanya linalofanana na hilo.
 
Kaka unajua ule msemo dúnia duara!!Sasa siku na wewe ukipigiwa tukio mkeo au binti yako i hope utakua mpole!!!!!
 
Ha ha ha ....[emoji2]
Ni survival for the fittest.

Binafs Hii tabia nmeanza tangu Niko sekondari, napenda sna mashindano hasa Aya ya kupindua meza[emoji2]
Kaka omba usikutane na wazee wa kangwiru kutoka ujiji visasi vyao waga vya ziwa tanganyika!!!Utajuta kupindua meza zao🤣🤣😂😂
 
Kaka mafia wanajitangaza jamii forum????Sema umekutana wanyonge afu hawana hela !!!Ukikutana na wazee wa pangusa upanguswe utaelewa namaanisha nini!!!Anyway story yako imenipa funzo kuhusu uanaume
 
Chai
 
Maisha haya hayawez kuisha changamoto

Me mwenyewe nilishawah kuwanyanganya masela mademu wakwanza alikuwa na manz wanapendana vizur tu ile urafiki akasema ngj akanitambulishe kwa shem ile tumeenda tunafika nakuta mali inalipa akanitambulisha pale BTW yule demu nilikuwa nafahamiana nae kdg tu alivyonitambulisha ndo tukafahamiana zaidi namba yake nilikuwa nayo sijui jini gan aliingia baada ya kutambuliswa tu nkaona huyo imnabd awe wangu siku hazikupita nyingi mwenye mali akawa shemeji nawashauri wanaume baada kwanza tutafute hela then tujarbu kutengeneza jina na vikazi vya kuzugia ofcn [emoji23]

wa pili huyu had now niko nae alikuwa na watu wake sio mmoja kama kawaida nilivyokuwa natoka kazini nampitia kwao tunapiga story kdg mida ya night akija mtu wake anakuta niko nae bas akaona nikama anampotezea sikufanya figisu kuwaachanisha nilimjaza maneno nae akajazika
Siku zikapta akahamia kwangu kabisa ingawa huwa wanaongea nikiwa sipo na hajui kama simu yake niliweka auto call record wakiwa wanaongea
[emoji23]!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…